Ufunuo 9 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 9:1-21

Tarumbeta Ya Tano

19:1 Ufu 8:10; Lk 8:31Malaika wa tano akaipiga tarumbeta yake, nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka toka angani hadi ardhini. Nyota hiyo ilipewa ufunguo wa lile Shimo.9:1 Yaani Abyss kwa Kiyunani; maana yake ni Kuzimu, yaani makao ya pepo wachafu. 29:2 Mwa 19:28; Kut 19:18; Yoe 2:2-10Alipolifungua hilo Shimo, moshi ukapanda kutoka humo kama moshi wa tanuru kubwa sana. Jua na anga vikatiwa giza na ule moshi uliotoka katika hilo Shimo. 39:3 Kut 10:12-15Ndipo katika ule moshi wakatoka nzige wakaenda juu ya nchi, nao wakapewa nguvu kama zile za nge wa duniani. 49:4 Ufu 7:2-3; 6:6; 8:7; Eze 9:4; Ufu 7:3Wakaambiwa wasidhuru nyasi ya nchi, wala mmea wala mti wowote, bali wawadhuru tu wale watu ambao hawana muhuri wa Mungu kwenye vipaji vya nyuso zao. 59:5 Ufu 9:3, 10Wakaruhusiwa kuwatesa kwa muda wa miezi mitano, lakini wasiwaue. Uchungu wa kuuma kwao ulikuwa kama ule wa mtu aumwapo na nge. 69:6 Ay 7:15; Ufu 6:16Katika siku hizo watu watatafuta kifo lakini hawatakiona, watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.

79:7 Yoe 2:4; Dan 7:8Wale nzige walikuwa na umbo kama la farasi waliotayarishwa kwa ajili ya vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji za dhahabu na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu. 89:8 Yoe 1:6Walikuwa na nywele kama za wanawake, na meno yao yalikuwa kama ya simba. 99:9 Yoe 2:5Walikuwa na dirii kama za chuma, na sauti za mabawa yao zilikuwa kama ngurumo za farasi wengi na magari mengi yakikimbilia vitani. 109:10 Ufu 9:3, 5, 19Walikuwa na mikia yenye miiba ya kuumia kama nge. Nguvu yao ya kutesa watu kwa huo muda wa miezi mitano ilikuwa katika hiyo mikia yao. 119:11 Ufu 9:1, 2; Lk 8:31; 16:16; Ay 26:6; 28:22Walikuwa na mfalme wao, ambaye ni malaika wa lile Shimo, ambaye jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani ni Apolioni.9:11 Abadoni au Apolioni maana yake ni Mharabu, yaani Yule aharibuye.

129:12 Ufu 8:13Ole ya kwanza imepita, bado nyingine mbili zinakuja.

Tarumbeta Ya Sita

139:13 Kut 30:1-3; Ufu 8:3Malaika wa sita akaipiga tarumbeta yake, nami nikasikia sauti ikitoka katika zile pembe za madhabahu ya dhahabu iliyoko mbele za Mungu. 149:14 Ufu 16:12Ile sauti ikamwambia yule malaika wa sita mwenye tarumbeta, “Wafungulie wale malaika wanne waliofungwa kwenye ule mto mkubwa Frati.” 159:15 Ufu 20:7; 8:7; 9:12Basi wale malaika wanne, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ajili ya saa hiyo, na siku hiyo, na mwezi huo, na mwaka huo ili wawaue theluthi ya wanadamu wakafunguliwa. 169:16 Ufu 5:11; 7:4Idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa 200,000,000. Nilisikia idadi yao.

179:17 Ufu 11:5Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika maono yangu: Wapanda farasi walivaa dirii vifuani zenye rangi nyekundu sana kama ya moto na yakuti samawi na kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vichwa vya simba, na moto, moshi na kiberiti vilitoka vinywani mwao. 189:18 Ufu 8:7; 9:15, 17Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo hayo matatu, yaani, huo moto, moshi na kiberiti, vilivyotoka kwenye vinywa vya hao farasi. 199:19 Isa 9:15Nguvu za hao farasi zilikuwa katika vinywa vyao na kwenye mikia yao, kwa sababu mikia yao ilikuwa kama nyoka, yenye vichwa ambayo waliitumia kudhuru.

209:20 Mik 5:13; Mdo 7:41; 1Kor 10:20; Dan 5:23Wanadamu waliosalia, ambao hawakuuawa katika mapigo hayo, bado walikataa kutubia kazi za mikono yao na hawakuacha kuabudu mashetani na sanamu za dhahabu, za fedha, za shaba, za mawe na za miti, ambazo haziwezi kuona, kusikia wala kutembea. 219:21 Ufu 2:21; 18:23; 17:2-5Wala hawakutubu na kuacha matendo yao ya uuaji, uchawi, uasherati wala wizi wao.

New International Version – UK

Revelation 9:1-21

1The fifth angel sounded his trumpet, and I saw a star that had fallen from the sky to the earth. The star was given the key to the shaft of the Abyss. 2When he opened the Abyss, smoke rose from it like the smoke from a gigantic furnace. The sun and sky were darkened by the smoke from the Abyss. 3And out of the smoke locusts came down on the earth and were given power like that of scorpions of the earth. 4They were told not to harm the grass of the earth or any plant or tree, but only those people who did not have the seal of God on their foreheads. 5They were not allowed to kill them but only to torture them for five months. And the agony they suffered was like that of the sting of a scorpion when it strikes. 6During those days people will seek death but will not find it; they will long to die, but death will elude them.

7The locusts looked like horses prepared for battle. On their heads they wore something like crowns of gold, and their faces resembled human faces. 8Their hair was like women’s hair, and their teeth were like lions’ teeth. 9They had breastplates like breastplates of iron, and the sound of their wings was like the thundering of many horses and chariots rushing into battle. 10They had tails with stings, like scorpions, and in their tails they had power to torment people for five months. 11They had as king over them the angel of the Abyss, whose name in Hebrew is Abaddon and in Greek is Apollyon (that is, Destroyer).

12The first woe is past; two other woes are yet to come.

13The sixth angel sounded his trumpet, and I heard a voice coming from the four horns of the golden altar that is before God. 14It said to the sixth angel who had the trumpet, ‘Release the four angels who are bound at the great river Euphrates.’ 15And the four angels who had been kept ready for this very hour and day and month and year were released to kill a third of mankind. 16The number of the mounted troops was twice ten thousand times ten thousand. I heard their number.

17The horses and riders I saw in my vision looked like this: their breastplates were fiery red, dark blue, and yellow as sulphur. The heads of the horses resembled the heads of lions, and out of their mouths came fire, smoke and sulphur. 18A third of mankind was killed by the three plagues of fire, smoke and sulphur that came out of their mouths. 19The power of the horses was in their mouths and in their tails; for their tails were like snakes, having heads with which they inflict injury.

20The rest of mankind who were not killed by these plagues still did not repent of the work of their hands; they did not stop worshipping demons, and idols of gold, silver, bronze, stone and wood – idols that cannot see or hear or walk. 21Nor did they repent of their murders, their magic arts, their sexual immorality or their thefts.