Ufunuo 7 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 7:1-17

Waisraeli 144,000 Watiwa Muhuri

17:1 Yer 49:36; Mt 24:31Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili kwamba pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote. 27:2 Ufu 9:4; Mt 16:16Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema, 37:3 Ufu 6:6; Eze 9:4; Ufu 22:4“Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.” 47:4 Ufu 9:16; 14:1-3Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: yaani 144,000 kutoka makabila yote ya Israeli.

5Kutoka kabila la Yuda 12,000 walitiwa muhuri,

kutoka kabila la Reubeni 12,000,

kutoka kabila la Gadi 12,000,

6kutoka kabila la Asheri 12,000,

kutoka kabila la Naftali 12,000,

kutoka kabila la Manase 12,000,

7kutoka kabila la Simeoni 12,000,

kutoka kabila la Lawi 12,000,

kutoka kabila la Isakari 12,000,

8kutoka kabila la Zabuloni 12,000,

kutoka kabila la Yosefu 12,000,

na kutoka kabila la Benyamini 12,000.

Umati Mkubwa Wa Watu Kutoka Mataifa Yote

97:9 Ufu 5:9; 13:7; 7:15; Rum 11:25; Ufu 3:5; 6:11; 7:4Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuuhesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao. 107:10 Za 3:8; Ufu 19:1Nao walikuwa wakipiga kelele kwa sauti kubwa wakisema:

“Wokovu una Mungu wetu,

yeye aketiye kwenye kiti cha enzi,

na Mwana-Kondoo!”

117:11 Ufu 4:4-10Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu, 127:12 Rum 11:36; Ufu 5:12-14wakisema:

“Amen!

Sifa na utukufu

na hekima na shukrani na heshima

na uweza na nguvu

viwe kwa Mungu wetu milele na milele.

Amen!”

137:13 Ufu 3:4; 7:9Kisha mmoja wa wale wazee ishirini na wanne akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?”

147:14 Ufu 22:14; Ebr 9:14; 1Yn 1:7Nikamjibu, “Bwana, wewe wajua.”

Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa. 157:15 Ufu 22:3; 11:19; Isa 4:5-6Kwa hiyo,

“Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu

na kumtumikia usiku na mchana

katika hekalu lake;

naye aketiye katika kile kiti cha enzi

atatanda hema yake juu yao.

167:16 Isa 49:10Kamwe hawataona njaa

wala kiu tena.

Jua halitawapiga

wala joto lolote liunguzalo.

177:17 Za 23:1; Yn 10:11; Isa 51:11; Ufu 21:3Kwa maana Mwana-Kondoo

aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi

atakuwa Mchungaji wao;

naye atawaongoza kwenda

kwenye chemchemi za maji yaliyo hai.

Naye Mungu atafuta kila chozi

kutoka macho yao.”

King James Version

Revelation 7:1-17

1And after these things I saw four angels standing on the four corners of the earth, holding the four winds of the earth, that the wind should not blow on the earth, nor on the sea, nor on any tree. 2And I saw another angel ascending from the east, having the seal of the living God: and he cried with a loud voice to the four angels, to whom it was given to hurt the earth and the sea, 3Saying, Hurt not the earth, neither the sea, nor the trees, till we have sealed the servants of our God in their foreheads. 4And I heard the number of them which were sealed: and there were sealed an hundred and forty and four thousand of all the tribes of the children of Israel. 5Of the tribe of Juda were sealed twelve thousand. Of the tribe of Reuben were sealed twelve thousand. Of the tribe of Gad were sealed twelve thousand. 6Of the tribe of Aser were sealed twelve thousand. Of the tribe of Nepthalim were sealed twelve thousand. Of the tribe of Manasses were sealed twelve thousand. 7Of the tribe of Simeon were sealed twelve thousand. Of the tribe of Levi were sealed twelve thousand. Of the tribe of Issachar were sealed twelve thousand. 8Of the tribe of Zabulon were sealed twelve thousand. Of the tribe of Joseph were sealed twelve thousand. Of the tribe of Benjamin were sealed twelve thousand. 9After this I beheld, and, lo, a great multitude, which no man could number, of all nations, and kindreds, and people, and tongues, stood before the throne, and before the Lamb, clothed with white robes, and palms in their hands; 10And cried with a loud voice, saying, Salvation to our God which sitteth upon the throne, and unto the Lamb. 11And all the angels stood round about the throne, and about the elders and the four beasts, and fell before the throne on their faces, and worshipped God, 12Saying, Amen: Blessing, and glory, and wisdom, and thanksgiving, and honour, and power, and might, be unto our God for ever and ever. Amen. 13And one of the elders answered, saying unto me, What are these which are arrayed in white robes? and whence came they? 14And I said unto him, Sir, thou knowest. And he said to me, These are they which came out of great tribulation, and have washed their robes, and made them white in the blood of the Lamb. 15Therefore are they before the throne of God, and serve him day and night in his temple: and he that sitteth on the throne shall dwell among them. 16They shall hunger no more, neither thirst any more; neither shall the sun light on them, nor any heat. 17For the Lamb which is in the midst of the throne shall feed them, and shall lead them unto living fountains of waters: and God shall wipe away all tears from their eyes.