Ufunuo 19 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 19:1-21

Shangwe Huko Mbinguni

119:1 Ufu 11:15; 7:10; 4:11Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,

219:2 Kum 32:43; Ufu 6:10kwa maana hukumu zake

ni za kweli na za haki.

Amemhukumu yule kahaba mkuu

aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake.

Mungu amemlipiza kisasi

kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”

319:3 Isa 34:10; Ufu 14:11Wakasema tena kwa nguvu:

“Haleluya!

Moshi wake huyo kahaba unapanda juu

milele na milele.”

419:4 Ufu 4:4-6; 5:14Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu:

“Amen, Haleluya!”

519:5 Za 134:1; Ufu 11:18Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema:

“Msifuni Mungu wetu,

ninyi watumishi wake wote,

ninyi nyote mnaomcha,

wadogo kwa wakubwa!”

619:6 Ufu 11:15Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.

719:7 Mt 25:10; Efe 5:32; Ufu 21:2, 9Tufurahi, tushangilie

na kumpa utukufu!

Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia

na bibi arusi wake amejiweka tayari.

819:8 Ufu 15:4; 19:14; 15:6; Isa 61:10; Eze 44:17; Zek 3:4Akapewa kitani safi, nyeupe

inayongʼaa, ili avae.”

(Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)

919:9 Ufu 1:19; Lk 14:15; Ufu 21:5; 22:6Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’ ” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”

1019:10 Ufu 22:8; Mdo 10:25, 26; Ufu 22:9; 12:17Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”

Aliyepanda Farasi Mweupe

1119:11 Ufu 6:2; 3:14; Kut 15:3Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita. 1219:12 Ufu 1:14; 6:2; 2:17Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe. 1319:13 Isa 63:2, 3; Yn 1:1Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.” 1419:14 Ufu 19:8; 3:4; 17:14Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri. 1519:15 Ufu 1:16; 12:5; 14:20; Isa 11:4; 2The 2:8; Za 2:9Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi. 1619:16 Ufu 17:14; 19:12; 1Tim 6:15Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili:

Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.

Mnyama Na Majeshi Yake Yashindwa

1719:17 Ufu 8:13; Eze 39:17Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu, 1819:18 Eze 39:18-20ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”

1919:19 Ufu 16:14, 16Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake. 2019:20 Ufu 16:13; 13:12; Dan 7:11; Ufu 21:8; 14:19Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. 21Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

啟示錄 19:1-21

天上的讚美

1這事以後,我聽見天上好像有一大群人在呼喊:「哈利路亞19·1 哈利路亞」意思是「要讚美上帝」。!救贖、榮耀和權能都歸於我們的上帝! 2因為祂的審判真實公義,祂懲罰了那用淫亂敗壞世界的大淫婦,為那些被她殺害的奴僕伸冤。」 3他們又歡呼說:「哈利路亞!焚燒大淫婦的煙不斷上騰,直到永永遠遠。」 4那二十四位長老和四個活物也俯伏敬拜坐在寶座上的上帝,說:「阿們!哈利路亞!」

5這時從寶座那裡發出聲音,說:「上帝所有的奴僕和一切敬畏祂的人,無論尊卑老少,都要讚美我們的上帝!」 6我聽見有聲音好像一大群人的呼喊聲,又像洪濤,也像雷鳴,說:「哈利路亞!因為我們的主——全能的上帝已經執掌王權了。 7我們應當歡喜快樂,歸榮耀給祂,因為羔羊的婚期到了,祂的新娘已預備妥當, 8獲准穿上光亮潔白的細麻衣。」這細麻衣代表聖徒的義行。

9天使吩咐我說:「你要寫下來,被邀請參加羔羊婚宴的人有福了!」他又說:「這是上帝親口說的,千真萬確。」 10我俯伏在他腳前要拜他,他卻說:「千萬不可!我和你並那些為耶穌做見證的弟兄姊妹同是上帝的奴僕。你要敬拜上帝,因為預言的真諦就是為耶穌做見證。」

白馬騎士

11我看見天開了,有一匹白馬出來,馬上的騎士名叫「誠信真實」,祂憑公義審判、作戰。 12祂的雙目如火焰,頭上戴了許多冠冕,寫著一個只有祂自己才明白的名字。 13祂穿著被鮮血浸透的衣服,祂的名字是「上帝的道」。 14眾天軍穿著潔白的細麻衣,騎著白馬跟隨祂。 15祂口中吐出一把利劍,可以攻擊列國。祂必用鐵杖統治他們,踩踏盛滿全能上帝之烈怒的榨酒池。 16祂的衣服和大腿上都寫著祂的名號:「萬王之王,萬主之主。」

17我又看見一位天使站在太陽裡,對空中飛翔的鳥大聲呼喚: 18「來吧!一起來參加上帝的盛宴,一同享用君王、將軍、勇士、馬匹、騎士、自由人、奴隸和尊卑老少的肉吧!」

19我看見那怪獸、地上的眾王及其軍隊聚集起來,要與白馬騎士和祂的軍隊作戰。 20後來,怪獸被俘虜了,在怪獸面前行奇蹟的假先知也一同被擒了。這假先知曾用奇蹟欺騙那些蓋了獸印、敬拜獸像的人。他和怪獸一同被活活地扔進硫磺火湖裡。 21怪獸的殘兵紛紛被白馬騎士口中的利劍所殺,飛鳥飽餐了他們的肉。