Ufunuo 19 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 19:1-21

Shangwe Huko Mbinguni

119:1 Ufu 11:15; 7:10; 4:11Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,

219:2 Kum 32:43; Ufu 6:10kwa maana hukumu zake

ni za kweli na za haki.

Amemhukumu yule kahaba mkuu

aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake.

Mungu amemlipiza kisasi

kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”

319:3 Isa 34:10; Ufu 14:11Wakasema tena kwa nguvu:

“Haleluya!

Moshi wake huyo kahaba unapanda juu

milele na milele.”

419:4 Ufu 4:4-6; 5:14Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu:

“Amen, Haleluya!”

519:5 Za 134:1; Ufu 11:18Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema:

“Msifuni Mungu wetu,

ninyi watumishi wake wote,

ninyi nyote mnaomcha,

wadogo kwa wakubwa!”

619:6 Ufu 11:15Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.

719:7 Mt 25:10; Efe 5:32; Ufu 21:2, 9Tufurahi, tushangilie

na kumpa utukufu!

Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia

na bibi arusi wake amejiweka tayari.

819:8 Ufu 15:4; 19:14; 15:6; Isa 61:10; Eze 44:17; Zek 3:4Akapewa kitani safi, nyeupe

inayongʼaa, ili avae.”

(Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)

919:9 Ufu 1:19; Lk 14:15; Ufu 21:5; 22:6Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’ ” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”

1019:10 Ufu 22:8; Mdo 10:25, 26; Ufu 22:9; 12:17Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”

Aliyepanda Farasi Mweupe

1119:11 Ufu 6:2; 3:14; Kut 15:3Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita. 1219:12 Ufu 1:14; 6:2; 2:17Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe. 1319:13 Isa 63:2, 3; Yn 1:1Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.” 1419:14 Ufu 19:8; 3:4; 17:14Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri. 1519:15 Ufu 1:16; 12:5; 14:20; Isa 11:4; 2The 2:8; Za 2:9Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi. 1619:16 Ufu 17:14; 19:12; 1Tim 6:15Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili:

Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.

Mnyama Na Majeshi Yake Yashindwa

1719:17 Ufu 8:13; Eze 39:17Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu, 1819:18 Eze 39:18-20ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”

1919:19 Ufu 16:14, 16Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake. 2019:20 Ufu 16:13; 13:12; Dan 7:11; Ufu 21:8; 14:19Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. 21Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

启示录 19:1-21

天上的赞美

1这事以后,我听见天上好像有一大群人在呼喊:“哈利路亚19:1 哈利路亚”意思是“要赞美上帝”。!救赎、荣耀和权能都归于我们的上帝! 2因为祂的审判真实公义,祂惩罚了那用淫乱败坏世界的大淫妇,为那些被她杀害的奴仆申冤。” 3他们又欢呼说:“哈利路亚!焚烧大淫妇的烟不断上腾,直到永永远远。” 4那二十四位长老和四个活物也俯伏敬拜坐在宝座上的上帝,说:“阿们!哈利路亚!”

5这时从宝座那里发出声音,说:“上帝所有的奴仆和一切敬畏祂的人,无论尊卑老少,都要赞美我们的上帝!” 6我听见有声音好像一大群人的呼喊声,又像洪涛,也像雷鸣,说:“哈利路亚!因为我们的主——全能的上帝已经执掌王权了。 7我们应当欢喜快乐,归荣耀给祂,因为羔羊的婚期到了,祂的新娘已预备妥当, 8获准穿上光亮洁白的细麻衣。”这细麻衣代表圣徒的义行。

9天使吩咐我说:“你要写下来,被邀请参加羔羊婚宴的人有福了!”他又说:“这是上帝亲口说的,千真万确。” 10我俯伏在他脚前要拜他,他却说:“千万不可!我和你并那些为耶稣做见证的弟兄姊妹同是上帝的奴仆。你要敬拜上帝,因为预言的真谛就是为耶稣做见证。”

白马骑士

11我看见天开了,有一匹白马出来,马上的骑士名叫“诚信真实”,祂凭公义审判、作战。 12祂的双目如火焰,头上戴了许多冠冕,写着一个只有祂自己才明白的名字。 13祂穿着被鲜血浸透的衣服,祂的名字是“上帝的道”。 14众天军穿着洁白的细麻衣,骑着白马跟随祂。 15祂口中吐出一把利剑,可以攻击列国。祂必用铁杖统治他们,踩踏盛满全能上帝之烈怒的榨酒池。 16祂的衣服和大腿上都写着祂的名号:“万王之王,万主之主。”

17我又看见一位天使站在太阳里,对空中飞翔的鸟大声呼唤: 18“来吧!一起来参加上帝的盛宴,一同享用君王、将军、勇士、马匹、骑士、自由人、奴隶和尊卑老少的肉吧!”

19我看见那怪兽、地上的众王及其军队聚集起来,要与白马骑士和祂的军队作战。 20后来,怪兽被俘虏了,在怪兽面前行奇迹的假先知也一同被擒了。这假先知曾用奇迹欺骗那些盖了兽印、敬拜兽像的人。他和怪兽一同被活活地扔进硫磺火湖里。 21怪兽的残兵纷纷被白马骑士口中的利剑所杀,飞鸟饱餐了他们的肉。