Ufunuo 16 – NEN & NSP

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 16:1-21

Mabakuli Saba Ya Ghadhabu Ya Mungu

116:1 Ufu 15:1; 11:19; 15:1; 16:2-21; Za 79:6; Sef 3:8Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mle Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, “Nendeni, mkayamwage duniani hayo mabakuli saba ya ghadhabu ya Mungu.”

216:2 Ufu 8:7; 13:15; 17; Kut 9:9-11Malaika wa kwanza akaenda akalimwaga hilo bakuli lake juu ya nchi. Majipu mabaya yenye maumivu makali yakawapata wale watu wote waliokuwa na chapa ya yule mnyama na walioabudu sanamu yake.

316:3 Kut 7:17-21; Ufu 6:11Malaika wa pili akalimwaga bakuli lake baharini, nayo ikabadilika kuwa damu kama ya mtu aliyekufa na kila kiumbe hai kilichokuwa ndani ya bahari kikafa.

416:4 Ufu 8:10Malaika wa tatu akalimwaga bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, nazo zikawa damu. 516:5 Ufu 15:3-4; 15:3; 1:4; 15:4; 6:10Ndipo nikamsikia malaika msimamizi wa maji akisema:

“Wewe una haki katika hukumu hizi ulizotoa,

wewe uliyeko, uliyekuwako, Uliye Mtakatifu,

kwa sababu umehukumu hivyo;

616:6 Isa 49:26kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu wako

na manabii wako,

nawe umewapa damu wanywe

kama walivyostahili.”

716:7 Ufu 9:6; 15:3; 19:2Nikasikia madhabahu ikiitikia,

“Naam, Bwana Mungu Mwenyezi,

hukumu zako ni kweli na haki.”

816:8 Ufu 8:12; 14:18Malaika wa nne akamimina bakuli lake kwenye jua, nalo likapewa nguvu za kuwaunguza watu kwa moto. 916:9 Ufu 2:21; 11:13Watu wakaunguzwa na hilo joto kali, wakalaani Jina la Mungu, aliyekuwa na uwezo juu ya mapigo haya, tena wakakataa kutubu na kumtukuza Mungu.

1016:10 Ufu 13:2; 9:2Malaika wa tano akamimina bakuli lake kwenye kiti cha enzi cha yule mnyama, nao ufalme wake ukagubikwa na giza. Watu wakatafuna ndimi zao kwa ajili ya maumivu, 1116:11 Ufu 11:13; 2:21; 16:9, 21wakamlaani Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu na majeraha yao, wala hawakutubu kwa ajili ya matendo yao maovu.

1216:12 Ufu 9:14; Isa 41:2Malaika wa sita akamimina bakuli lake kwenye mto mkubwa Frati, maji yake yakakauka ili kutayarisha njia kwa ajili ya wafalme watokao Mashariki. 1316:13 Ufu 12:3; 13:1; 19:20Kisha nikaona roho wachafu watatu waliofanana na vyura wakitoka katika kinywa cha lile joka na katika kinywa cha yule mnyama na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. 1416:14 1Tim 4:1; Ufu 17:14Hizo ndizo roho za pepo wachafu zitendazo miujiza. Nazo huwaendea wafalme wa ulimwengu wote na kuwakusanya tayari kwa ajili ya vita katika siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.

1516:15 Lk 12:3“Tazama, naja kama mwizi! Amebarikiwa yeye akeshaye na kuziweka tayari nguo zake ili asiende uchi na kuonekana aibu yake.”

1616:16 Ufu 9:11; Amu 5:19Ndipo wakawakusanya wafalme pamoja mahali paitwapo Armagedoni16:16 Armagedoni au Har-Magedoni ina maana Mlima Megido, mahali pa kinabii ambapo wafalme wote wa dunia watakusanyika kwa vita katika siku ya Mungu Mwenyezi. kwa Kiebrania.

1716:17 Efe 2:2; Ufu 14:15; 11:15; 21:6Malaika wa saba akamimina bakuli lake angani na sauti kubwa ikatoka mle hekaluni katika kile kiti cha enzi, ikisema, “Imekwisha kuwa!” 1816:18 Ufu 4:5; 6:12; Dan 12:1Kukawa na mianga ya umeme wa radi, ngurumo, radi na tetemeko kubwa la ardhi. Hapajawa kamwe na tetemeko la ardhi kama hilo tangu mwanadamu awepo duniani, hivyo lilikuwa tetemeko kubwa ajabu. 1916:19 Ufu 17:18; 18:5; 14:8Ule mji mkubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikaanguka. Mungu akaukumbuka Babeli Mkuu na kumpa kikombe kilichojaa mvinyo wa ghadhabu ya hasira yake. 2016:20 Ufu 6:14Kila kisiwa kikatoweka wala milima haikuonekana. 2116:21 Eze 13:13; Kut 9:23-25Mvua kubwa ya mawe yenye uzito wa talanta moja16:21 Talanta moja ni kama kilo 34. ikashuka kutoka mbinguni, ikawaangukia wanadamu. Nao wanadamu wakamlaani Mungu kwa ajili ya hayo mapigo ya mvua ya mawe, kwa sababu pigo hilo lilikuwa la kutisha.

New Serbian Translation

Откривење 16:1-21

1Онда сам чуо снажан глас из храма како говори седморици анђела: „Идите и излијте седам здела Божијег гнева на земљу!“ 2Први анђео оде и изли своју зделу на земљу. Тада избише болни и злоћудни чиреви на људима који су имали жиг Звери и који су се клањали њеном кипу.

3Други анђео изли своју зделу у море, те се оно претвори у крв као у мртваца, те угину свако живо биће у мору.

4Трећи анђео изли своју зделу на реке и на водене изворе, те се и они претворише у крв. 5Онда сам чуо анђела задуженог за воде како говори:

„Праведан си ти који јеси и који си био,

Свети, што си овако пресудио.

6Они су пролили крв светих и пророка,

и зато си им дао крв да пију;

то су заслужили!“

7Тада сам чуо жртвеник како говори:

„Да, Господе Боже, Сведржитељу,

истинити и праведни су твоји судови!“

8Четврти анђео изли своју зделу на сунце, коме је дата моћ да пали људе ватром. 9Паљени великом јаром, људи су проклињали име Бога који има власт над овим злима. Ипак, нису се покајали и дали му славу.

10Пети анђео изли своју зделу на престо Звери. Његово царство утону у таму, а људи од муке почеше да гризу своје језике, 11и да проклињу Бога небеског због својих мука и чирева. Ипак, нису се покајали за своја дела.

12Шести анђео изли своју зделу на велику реку Еуфрат. Његова вода пресахну, припремајући пут за цареве који долазе са истока. 13Онда сам видео како из уста Аждаје, из уста Звери и из уста лажног пророка излазе три нечиста духа, који су личили на жабе. 14То су зли духови који чине знаке. Они иду к царевима света да их окупе на рат за велики дан Бога Сведржитеља.

15„Ево, долазим као лопов! Блажен је онај који бдије и чува своју одећу! Такав, наиме, неће ићи го, и неће се јавно осрамотити.“

16Они окупише цареве на место које се на јеврејском зове „Армагедон“.

17Седми анђео изли своју зделу у ваздух. Тада се из храма, са престола, зачу громки глас, говорећи: „Свршено је!“ 18Уто севну муње, проломи се грмљавина и прасну громови, те настане велики земљотрес каквог није било откада је људи на земљи. Био је то земљотрес огромних размера. 19Велики град расцепи се на три дела, а градови народа се распадоше. Бог се сетио великог Вавилона, те му даде чашу вина свога јаросног гнева. 20Сва острва ишчезнуше, а од гора не оста ни трага. 21Тада се на људе сручи огроман град са неба, и сваки је тежио по талант16,21 Око 34 kg.. Људи су проклињали Бога због зла од града, јер је ово зло било веома велико.