Ufunuo 13 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 13:1-18

113:1 Dan 7:1-6; Ufu 16:13; 12:3; Dan 11:36; Ufu 17:3Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari.

Mnyama Kutoka Baharini

Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru. 213:2 Dan 7:6; 7:5; 7:4; Ufu 16:10Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa. 313:3 Ufu 17:8Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama. 413:4 Kut 15:11Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”

513:5 Dan 11:36; 2The 2:4; Ufu 11:2Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili. 613:6 Ufu 12:12Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni. 713:7 Dan 7:21; Ufu 11:7; 5:9Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa. 813:8 Ufu 3:10; 3:5; 20:12; Mt 25:34Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

913:9 Ufu 2:7Yeye aliye na sikio na asikie.

1013:10 Yer 15:2; 43:11; Hes 6:12; Ufu 14:12Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka,

atachukuliwa mateka.

Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga,

atauawa kwa upanga.

Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.

Mnyama Kutoka Dunia

1113:11 Ufu 13:1, 2Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka. 1213:12 Ufu 19:20; 20:4Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona. 1313:13 Mt 24:24; 2Fal 1:10; Lk 9:54Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi. 1413:14 2The 2:9, 10; Ufu 12:9Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi. 1513:15 Dan 3:3-6Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa. 1613:16 Ufu 19:5; 14:9Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso, 1713:17 Ufu 14:9; 14:11; 15:2ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.

1813:18 Ufu 17:9; 15:2; 21:17Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.

New International Version

Revelation 13:1-18

The Beast out of the Sea

1The dragon13:1 Some manuscripts And I stood on the shore of the sea. And I saw a beast coming out of the sea. It had ten horns and seven heads, with ten crowns on its horns, and on each head a blasphemous name. 2The beast I saw resembled a leopard, but had feet like those of a bear and a mouth like that of a lion. The dragon gave the beast his power and his throne and great authority. 3One of the heads of the beast seemed to have had a fatal wound, but the fatal wound had been healed. The whole world was filled with wonder and followed the beast. 4People worshiped the dragon because he had given authority to the beast, and they also worshiped the beast and asked, “Who is like the beast? Who can wage war against it?”

5The beast was given a mouth to utter proud words and blasphemies and to exercise its authority for forty-two months. 6It opened its mouth to blaspheme God, and to slander his name and his dwelling place and those who live in heaven. 7It was given power to wage war against God’s holy people and to conquer them. And it was given authority over every tribe, people, language and nation. 8All inhabitants of the earth will worship the beast—all whose names have not been written in the Lamb’s book of life, the Lamb who was slain from the creation of the world.13:8 Or written from the creation of the world in the book of life belonging to the Lamb who was slain

9Whoever has ears, let them hear.

10“If anyone is to go into captivity,

into captivity they will go.

If anyone is to be killed13:10 Some manuscripts anyone kills with the sword,

with the sword they will be killed.”13:10 Jer. 15:2

This calls for patient endurance and faithfulness on the part of God’s people.

The Beast out of the Earth

11Then I saw a second beast, coming out of the earth. It had two horns like a lamb, but it spoke like a dragon. 12It exercised all the authority of the first beast on its behalf, and made the earth and its inhabitants worship the first beast, whose fatal wound had been healed. 13And it performed great signs, even causing fire to come down from heaven to the earth in full view of the people. 14Because of the signs it was given power to perform on behalf of the first beast, it deceived the inhabitants of the earth. It ordered them to set up an image in honor of the beast who was wounded by the sword and yet lived. 15The second beast was given power to give breath to the image of the first beast, so that the image could speak and cause all who refused to worship the image to be killed. 16It also forced all people, great and small, rich and poor, free and slave, to receive a mark on their right hands or on their foreheads, 17so that they could not buy or sell unless they had the mark, which is the name of the beast or the number of its name.

18This calls for wisdom. Let the person who has insight calculate the number of the beast, for it is the number of a man.13:18 Or is humanity’s number That number is 666.