Ufunuo 13 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 13:1-18

113:1 Dan 7:1-6; Ufu 16:13; 12:3; Dan 11:36; Ufu 17:3Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari.

Mnyama Kutoka Baharini

Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru. 213:2 Dan 7:6; 7:5; 7:4; Ufu 16:10Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa. 313:3 Ufu 17:8Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama. 413:4 Kut 15:11Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”

513:5 Dan 11:36; 2The 2:4; Ufu 11:2Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili. 613:6 Ufu 12:12Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni. 713:7 Dan 7:21; Ufu 11:7; 5:9Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa. 813:8 Ufu 3:10; 3:5; 20:12; Mt 25:34Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

913:9 Ufu 2:7Yeye aliye na sikio na asikie.

1013:10 Yer 15:2; 43:11; Hes 6:12; Ufu 14:12Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka,

atachukuliwa mateka.

Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga,

atauawa kwa upanga.

Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.

Mnyama Kutoka Dunia

1113:11 Ufu 13:1, 2Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka. 1213:12 Ufu 19:20; 20:4Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona. 1313:13 Mt 24:24; 2Fal 1:10; Lk 9:54Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi. 1413:14 2The 2:9, 10; Ufu 12:9Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi. 1513:15 Dan 3:3-6Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa. 1613:16 Ufu 19:5; 14:9Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso, 1713:17 Ufu 14:9; 14:11; 15:2ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.

1813:18 Ufu 17:9; 15:2; 21:17Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

啟示錄 13:1-18

兩隻怪獸

1我又看見一隻怪獸從海中上來,有七頭十角,每隻角上都戴著一個冠冕,每個頭上都寫著褻瀆上帝的名號。 2牠看起來像豹,卻有熊的腳和獅子的口。巨龍將自己的能力、王位和大權柄都交給了怪獸。 3我看見怪獸的一個頭似乎受了致命傷,這傷卻復原了。全世界的人都驚奇地跟從了牠。 4他們拜巨龍,因為巨龍將自己的權力給了怪獸。他們又拜怪獸,說:「有誰比得上這獸呢?誰能與牠對抗呢?」 5巨龍又使怪獸說狂妄、褻瀆的話,並給牠權柄,可以任意妄為四十二個月。 6怪獸開口褻瀆上帝的名、上帝的居所和一切居住在天上的。 7牠又獲准去攻打聖徒,征服他們,並得到權柄制伏各民族、各部落、各語言族群、各國家。 8凡住在地上的人,就是從創世以來名字沒有記在被殺羔羊的生命冊上的,都會崇拜怪獸。

9凡有耳朵的都應當聽。

10該被擄的人必被擄,

該被刀殺的必被刀殺。

因此,聖徒需要堅忍和信心。

11我又看見另一隻怪獸從地裡竄出來,牠的兩隻角像羔羊的角,說話卻像龍, 12在頭一隻怪獸面前行使頭一隻怪獸的一切權柄。牠命令世上的人拜曾受了致命傷但已復原的頭一隻怪獸, 13又行大奇蹟,當眾叫火從天降到地上。 14牠在頭一隻怪獸面前獲准行奇蹟,欺騙了普世的人,並吩咐他們為受了刀傷卻仍然活著的頭一隻怪獸塑像。 15牠又獲准給怪獸的塑像生命氣息,使牠不但能說話,還能使所有不敬拜那像的人遭害。 16牠又強迫所有的人,不論老少、尊卑、貧富、自由人或奴隸,都在右手或額上接受印記。 17凡沒有蓋上怪獸印記的,就是沒有怪獸的名字或代號的,都不能做買賣。 18這裡藏有玄機,聰明的人可以計算那怪獸的代號,因為那是一個人的代號,是「六百六十六」。