Ufunuo 1 – NEN & SNC

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 1:1-20

Utangulizi Na Salamu

11:1 Ufu 22:16; Dan 2:28, 29; Yn 12:49; 17:8, 19; Ufu 22:6Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo ni lazima yatukie hivi karibuni. Alijulisha mambo haya kwa kumtuma malaika wake kwa Yohana mtumishi wake, 21:2 1Kor 1:6; Ufu 6:9; Ebr 4:12; Ufu 12:17; 19:10ambaye anashuhudia kuhusu kila kitu alichokiona, yaani, Neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo. 31:3 Lk 11:28; Ufu 22:7; Rum 13:11Amebarikiwa yeye asomaye maneno ya unabii huu, na wamebarikiwa wale wanaoyasikia na kuyatia moyoni yale yaliyoandikwa humo, kwa sababu wakati umekaribia.

Salamu Kwa Makanisa Saba

41:4 Isa 11:2; Rum 1:7; Ufu 4:8; 11:17; 3:1; 4:5; 5:6Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia:

Neema na amani iwe kwenu kutoka kwake aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, na kutoka kwa wale roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi, 51:5 Isa 55:4; Kol 1:18; Ufu 17:14na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni yule shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, mtawala wa wafalme wa dunia.

Kwake yeye anayetupenda na ambaye ametuweka huru kutoka dhambi zetu kwa damu yake, 61:6 1Pet 2:5; Rum 11:36akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, tumtumikie Mungu wake ambaye ni Baba yake. Utukufu na uwezo ni vyake milele na milele! Amen.

71:7 Dan 7:13; Zek 12:10Tazama! Anakuja na mawingu,

na kila jicho litamwona,

hata wale waliomchoma;

na makabila yote duniani

yataomboleza kwa sababu yake.

Naam, ndivyo itakavyokuwa! Amen.

81:8 Ufu 22:6; 4:8; 21:6; 22:13; 15:3; Kut 3:14; Isa 41:4; Ufu 21:6“Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.”

Maono Ya Kristo

91:9 Mdo 14:22; 2Tim 2:12Mimi, Yohana, ndugu yenu ninayeshiriki pamoja nanyi mateso katika Yesu na katika ufalme na uvumilivu katika saburi, nilikuwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu. 101:10 Ufu 17:3; 3:1Katika siku ya Bwana, nilikuwa katika Roho na nikasikia sauti kubwa kama ya baragumu nyuma yangu 111:11 Ufu 2:8; 22:13; Mdo 18:19; Kol 2:1; Mdo 16:14ikisema, “Andika kwenye kitabu haya yote unayoyaona, kisha uyapeleke kwa makanisa saba, yaani: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”

121:12 Zek 1:2; Ufu 3:1Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Nami nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu, 131:13 Eze 1:26; Ufu 14:14; Dan 10:5; Ufu 15:6na katikati ya vile vinara vya taa, alikuwamo mtu kama Mwana wa Adamu, akiwa amevaa joho refu, na mkanda wa dhahabu ukiwa umefungwa kifuani mwake. 141:14 Dan 7:9; Ufu 19:12Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji, nayo macho yake yalikuwa kama mwali wa moto. 151:15 Eze 1:7; 43:2; Ufu 2:18; 19:6Nyayo zake zilikuwa kama shaba inayongʼaa, katika tanuru ya moto, nayo sauti yake ilikuwa kama mugurumo ya maji mengi. 161:16 Ufu 3:1; Isa 1:20; Ebr 4:12Katika mkono wake wa kuume alishika nyota saba, na kinywani mwake ulitoka upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa kama jua likingʼaa kwa nguvu zake zote.

171:17 Eze 1:28; Dan 8:17, 18; Isa 48:12; Ufu 22:13Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama aliyekufa. Ndipo akauweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope, Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho. 181:18 Rum 6:9; Kum 32:40; Ufu 9:1Mimi ni Yeye Aliye Hai, niliyekuwa nimekufa, na tazama, ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu.1:18 Kuzimu linalotokana na neno Hades la Kiyunani au Sheol kwa Kiebrania; maana yake ni mahali pa mateso kwa watu waliopotea.

191:19 Ufu 1:11; Hab 2:2“Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yale yatakayotukia baada ya haya. 201:20 Zek 4:2; Mt 5:14, 15Kuhusu siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume na vile vinara saba vya taa vya dhahabu ni hii: Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, navyo vile vinara saba ni hayo makanisa saba.

Slovo na cestu

Zjevení 1:1-20

Úvodní slovo

1V této knize je zapsáno, co Bůh svěřil Ježíši Kristu o budoucích událostech a co Ježíš odhalil svému služebníku Janovi prostřednictvím anděla. 2Jan dosvědčuje, že to všechno viděl a zachytil jako Boží slovo sdělené Ježíšem Kristem. 3A tak, jestliže čteš nebo posloucháš toto proroctví, uděláš dobře, když se podle něho zařídíš; začne se totiž plnit už brzo.

Pozdravy a chvály

4Já, Jan, chci nejprve pozdravit adresáty, sedm křesťanských sborů v Malé Asii: Přeji vám potěšení a pokoj od Boha, který je, který byl a který přijde; od Ducha svatého, který zastupuje před Božím trůnem každý váš sbor; 5od Ježíše Krista, který za všemi následujícími slovy věrně stojí. Ten, který jako první vstal z mrtvých a je vládcem všech pozemských panovníků, ten nás miluje a prolil svou krev, aby odčinil naše provinění. 6Tak nás povýšil na spoluvládce svého království a kněze Boha Otce; jemu patří veškerá sláva a moc až na věky. Amen.

7On přijde a ujme se vlády nad celou zemí,

takže ho všichni uvidí a zděsí se, dokonce i ti,

kteří ho zabili.

Tak to bude.

8Tento Pán říká: „Já jsem začátek i konec – žiji, žil jsem od prvopočátku a bude mi patřit i závěr dějin, protože mám všechnu moc.“

Vidění Ježíše Krista

9Já, váš bratr Jan, spolu s vámi pronásledovaný a s vámi očekávající Kristovo království, byl jsem vyhnán na ostrov Patmos, protože jsem hlásal Boží slovo a svědčil o Ježíši Kristu. 10A zde jsem byl v duchu přenesen do událostí posledního dění.

Zezadu na mne volal hlas, zvučný jako polnice: 11„Co uvidíš a uslyšíš, zapiš do knihy a pošli to sedmi sborům v Malé Asii – do Efezu, Smyrny, Pergama, Tyatiry, Sard, Filadelfie a Laodiceje.“

12Otočil jsem se za tím hlasem a uviděl jsem sedm zlatých svícnů. 13Mezi nimi stála postava podobná Ježíši Kristu, oblečená do dlouhého pláště, sepnutého přes prsa zlatou šerpou. 14Jeho obličej svítil jako polední slunce a vlasy jako sněhobílá vlna. Oči mu zářily jako oheň 15a také jeho nohy žhnuly jako rozpálená mosaz. Jeho hlas hřměl jako mořský příboj. 16V pravé ruce držel sedm hvězd a v ústech měl ostře nabroušený meč.

Kristus a církev patří k sobě

17Když jsem ho uviděl, ulekl jsem se a padl před ním na zem. Ale on na mne položil ruku a řekl mi: „Neboj se! To jsem já, První i Poslední. 18Jsem živ; i když jsem zemřel, teď žiji na věčné věky. Mám klíče od smrti i hrobu. 19Zapiš všechno, co vidíš a co ti ještě ukáži. 20Abys dobře rozuměl tomu, co vidíš: Sedm svícnů je sedm sborů; sedm hvězd jsou ti, kteří za ně přede mnou nesou odpovědnost a jsou pod mou ochranou.“