Tito 1 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Tito 1:1-16

11:1 Rum 1:1; 1Tim 2:4Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa: 21:2 2Tim 1:1; 1:9imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, 31:3 1Tim 1:6; 2Tim 1:10; 1Tim 1:11; Lk 1:47naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:

41:4 2Kor 2:13; 1Tim 1:2; Rum 1:7; 1:12; 2Kor 4:13; Gal 2:3Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote:

Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.

Kazi Ya Tito Huko Krete

51:5 Mdo 27:7; 11:30Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza. 61:6 1Tim 3:2; 3:12; 4; 1The 3:13Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi. 71:7 1Tim 3:1; 1Kor 4:1; 1Tim 3:3, 8Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali. 81:8 1Tim 3:2; 2Tim 3:3Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake. 91:9 1Kor 16:13; 1Tim 1:10Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.

Walimu Wa Uongo

101:10 1Tim 1:6; Mdo 11:2Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara. 111:11 2Tim 3:6; Tit 3:6; Yn 10:12; 1Pet 5:2Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu. 121:12 Mdo 17:28; 2:11Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.” 131:13 2Kor 13:10; Tit 2:2Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani, 141:14 1Tim 4:7; 1:4; Kol 2:22; 2Tim 4:4ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli. 151:15 Rum 14:14, 23; Za 18:26; Mt 7:14-19; Mdo 10:9-16Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka. 161:16 1Yn 2; 4; Yer 5; 2; 12:2; Hos 8:2, 3Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

提多书 1:1-16

问候

1保罗做上帝的奴仆和耶稣基督的使徒,是为了使上帝拣选的人有信心、明白真理,从而过敬虔的生活, 2有永生的盼望。这永生是从不说谎的上帝在亘古以前应许的。 3祂在所定的时候,借着人的传扬将自己的道显明出来。我奉我们救主上帝的命令传扬这道。

4提多啊,我写信给你,就我们共同的信仰来说,你是我真正的儿子。

愿父上帝和我们的救主基督耶稣赐给你恩典和平安!

长老的资格

5当初,我把你留在克里特岛,是要你完成未办完的事工,并照我的指示在各城选立长老。 6做长老的必须无可指责,只有一位妻子,儿女都信主、没有放荡不羁的行为。 7身为上帝的管家,做监督的必须无可指责,不傲慢,不暴躁,不酗酒,不好斗,不贪财。 8他必须好客、乐善、自制、正直、圣洁、自律, 9持守所领受的真道,以便能够以纯正的教导劝勉人,驳倒那些反对的人。

10因为有许多悖逆之人喜欢空谈,善于欺骗,尤其是那些奉行割礼的人。 11你一定要堵住他们的口,因为他们为了不义之财教不该教的,误导了别人全家。 12克里特人自己的一位先知说:“克里特人说谎成性,邪恶如兽,好吃懒做。” 13这话是真的。因此你要严正地斥责他们,使他们有纯正的信仰, 14不理会犹太人荒诞的传说和那些违背真理之人的诫律。 15对洁净的人而言,一切都是洁净的;对污秽不信的人而言,什么都不洁净,连他们的思想和良心都是污秽的。 16他们自称认识上帝,在行为上却否认祂。他们令人可憎,悖逆成性,一无是处。