Ruthu 4 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ruthu 4:1-22

Boazi Amwoa Ruthu

14:1 Mwa 18:1; 23:10; Rut 2:20; 3:12Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.

24:2 Kut 3:16; 18:21, 22; Kum 16:18; 17:9; 29:10; 25:7; 1Fal 21:8; Za 82:2; Mit 31:21, 23Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi. 34:3 Law 25:25; Rut 1:2Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki. 44:4 Law 25:25; Rum 12:17; 2Kor 8:21; Flp 4:8; Mwa 23:18; Yer 32:7-8Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.”

Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”

54:5 Rut 1:22; 3:13; Mwa 38:8; Kum 25:5-6; Mt 22:24Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”

64:6 Law 25:25; Rut 3:13; Kum 25:7Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”

74:7 Law 25:24; Isa 8:1-2, 16-20; Kum 25:7-9(Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)

84:8 Kum 25:9Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.

94:9 Isa 8:2; Yer 32:10, 44Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni. 104:10 Rut 1:22; Kum 25:5-6; Yos 24:22Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”

114:11 Mwa 4:19; 23:10; 29:16; 35:16; Kum 25:9; Rut 1:19; Za 127:3Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu. 124:12 1Nya 2:4; Mt 1:3; 1Sam 2:20; Mwa 38:6, 24, 29Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”

Wazao Wa Boazi

134:13 Mwa 8:1; 29:31-32; 33:5; 30:6; Lk 1:57Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume. 144:14 Lk 1:58; Rum 12:15; Mwa 24:27; Rut 2:20Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote! 154:15 Mwa 11:31; Isa 1:8; 2:5; Ay 1:2Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”

16Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake. 174:17 1Sam 16:1, 13, 18; 17:12, 17, 58; 1Nya 2:12-15; Za 72:20Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.

184:18 Mwa 38:29; Hes 26:21Hivi ndivyo vizazi vya Peresi:

Peresi alimzaa Hesroni,

194:19 Kut 6:23Hesroni akamzaa Ramu,

Ramu akamzaa Aminadabu,

204:20 Hes 1:7; 7:12Aminadabu akamzaa Nashoni,

Nashoni akamzaa Salmoni,

214:21 Rut 1:2; Mt 1:21Salmoni akamzaa Boazi,

Boazi akamzaa Obedi,

22Obedi akamzaa Yese,

na Yese akamzaa Daudi.

King James Version

Ruth 4:1-22

1Then went Boaz up to the gate, and sat him down there: and, behold, the kinsman of whom Boaz spake came by; unto whom he said, Ho, such a one! turn aside, sit down here. And he turned aside, and sat down. 2And he took ten men of the elders of the city, and said, Sit ye down here. And they sat down. 3And he said unto the kinsman, Naomi, that is come again out of the country of Moab, selleth a parcel of land, which was our brother Elimelech’s: 4And I thought to advertise thee, saying, Buy it before the inhabitants, and before the elders of my people. If thou wilt redeem it, redeem it: but if thou wilt not redeem it, then tell me, that I may know: for there is none to redeem it beside thee; and I am after thee. And he said, I will redeem it.4.4 I thought…: Heb. I said, I will reveal in thine ear 5Then said Boaz, What day thou buyest the field of the hand of Naomi, thou must buy it also of Ruth the Moabitess, the wife of the dead, to raise up the name of the dead upon his inheritance.

6¶ And the kinsman said, I cannot redeem it for myself, lest I mar mine own inheritance: redeem thou my right to thyself; for I cannot redeem it. 7Now this was the manner in former time in Israel concerning redeeming and concerning changing, for to confirm all things; a man plucked off his shoe, and gave it to his neighbour: and this was a testimony in Israel. 8Therefore the kinsman said unto Boaz, Buy it for thee. So he drew off his shoe.

9¶ And Boaz said unto the elders, and unto all the people, Ye are witnesses this day, that I have bought all that was Elimelech’s, and all that was Chilion’s and Mahlon’s, of the hand of Naomi. 10Moreover Ruth the Moabitess, the wife of Mahlon, have I purchased to be my wife, to raise up the name of the dead upon his inheritance, that the name of the dead be not cut off from among his brethren, and from the gate of his place: ye are witnesses this day. 11And all the people that were in the gate, and the elders, said, We are witnesses. The LORD make the woman that is come into thine house like Rachel and like Leah, which two did build the house of Israel: and do thou worthily in Ephratah, and be famous in Beth-lehem:4.11 do thou…: or, get thee riches, or, power4.11 be famous: Heb. proclaim thy name 12And let thy house be like the house of Pharez, whom Tamar bare unto Judah, of the seed which the LORD shall give thee of this young woman.

13¶ So Boaz took Ruth, and she was his wife: and when he went in unto her, the LORD gave her conception, and she bare a son. 14And the women said unto Naomi, Blessed be the LORD, which hath not left thee this day without a kinsman, that his name may be famous in Israel.4.14 left…: Heb. caused to cease unto thee4.14 kinsman: or, redeemer 15And he shall be unto thee a restorer of thy life, and a nourisher of thine old age: for thy daughter in law, which loveth thee, which is better to thee than seven sons, hath born him.4.15 a nourisher of: Heb. to nourish4.15 thine…: Heb. thy gray hairs 16And Naomi took the child, and laid it in her bosom, and became nurse unto it. 17And the women her neighbours gave it a name, saying, There is a son born to Naomi; and they called his name Obed: he is the father of Jesse, the father of David.

18¶ Now these are the generations of Pharez: Pharez begat Hezron, 19And Hezron begat Ram, and Ram begat Amminadab, 20And Amminadab begat Nahshon, and Nahshon begat Salmon,4.20 Salmon: or, Salmah 21And Salmon begat Boaz, and Boaz begat Obed, 22And Obed begat Jesse, and Jesse begat David.