Obadia 1 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Obadia 1:1-21

11:1 Mwa 25:14; Isa 1:1; 21:11; Yoe 3:19; Mal 1:3; Eze 25:12-14; Yer 6:4-5; 49:7-22; Isa 11:14; 18:2; 34:11Maono ya Obadia.

Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu:

Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana:

Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema,

“Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”

2“Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa,

mtadharauliwa kabisa.

31:3 Isa 14:13; 16:6; 2Fal 14:7; 2Nya 25:11-12; Ufu 18:7Kiburi cha moyo wako kimekudanganya,

wewe unayeishi katika majabali ya miamba

na kufanya makao yako juu,

wewe unayejiambia mwenyewe,

‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’

41:4 Isa 10:14; 14:13; 14:14, 15; Ay 20:6; Amo 9:2; Yer 49:16; Hab 2:9Ingawa unapaa juu kama tai

na kufanya kiota chako kati ya nyota,

nitakushusha chini kutoka huko,”

asema Bwana.

51:5 Isa 24:13; Kum 4:27; 24:21“Ikiwa wevi wangekuja kwako,

ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku:

Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea:

je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?

Kama wachuma zabibu wangekuja kwako,

je, wasingebakiza zabibu chache?

6Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa,

jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!

71:7 Yer 30:14; Za 41:9Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani,

rafiki zako watakudanganya na kukushinda,

wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego,

lakini hutaweza kuugundua.

81:8 Ay 5:12; Isa 29:14“Katika siku hiyo,” asema Bwana,

“je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu,

watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?

91:9 Mwa 36:11, 34; Amo 2:16; Za 76:5; Yer 49:22; Nah 3:13Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu,

kila mmoja katika milima ya Esau

ataangushwa chini kwa kuchinjwa.

101:10 Yoe 3:19; Amo 1:11-12; Za 137:7; Mwa 47:21; Eze 35:5, 15; Mal 1:4; Eze 25:12-14; 35:9Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo,

aibu itakufunika;

utaangamizwa milele.

111:11 Ay 6:27; Nah 3:10; Eze 24:6Siku ile ulisimama mbali ukiangalia

wakati wageni walipojichukulia utajiri wake

na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake

wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu,

ulikuwa kama mmoja wao.

121:12 Eze 25:6; 35:15; Mit 17:5; 24:17; Mik 4:11; Ay 31:29Usingemdharau ndugu yako

katika siku ya msiba wake,

wala kufurahia juu ya watu wa Yuda

katika siku ya maangamizi yao,

wala kujigamba sana

katika siku ya taabu yao.

131:13 Eze 35:5Usingeingia katika malango ya watu wangu

katika siku ya maafa yao,

wala kuwadharau katika janga lao

katika siku ya maafa yao,

wala kunyangʼanya mali zao

katika siku ya maafa yao.

14Usingengoja kwenye njia panda

na kuwaua wakimbizi wao,

wala kuwatoa watu wake waliosalia

katika siku ya shida yao.

151:15 Yer 46:10; 50:29; Hab 2:8; Amu 1:7; Za 137:8; Eze 35:15; Yoe 2:31; 3:7-8; Eze 30:3; Amo 5:8“Siku ya Bwana iko karibu

kwa mataifa yote.

Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo,

matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.

161:16 Yer 25:15; 49:12; Mao 4:21-22; Isa 51:17; Kut 15:17; Eze 25:12-14Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu,

vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo,

watakunywa na kunywa,

nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.

171:17 Za 69:35; 74:2; Isa 14:1-2; Amo 9:11-15; Zek 8:12Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo

na wale watakaookoka;

nao utakuwa mtakatifu,

nayo nyumba ya Yakobo

itamiliki urithi wake.

181:18 Zek 12:6; Yer 49:10; Isa 1:31Nyumba ya Yakobo itakuwa moto,

na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto;

nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu,

nao wataiwasha moto na kuiteketeza.

Hakutakuwa na watakaosalimika

kutoka nyumba ya Esau.”

Bwana amesema.

191:19 Isa 11:14; Sef 2:7; Yer 31:5; Hes 1:36Watu kutoka nchi ya Negebu

wataikalia milima ya Esau,

na watu kutoka miteremko ya vilima

watamiliki nchi ya Wafilisti.

Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria,

naye Benyamini atamiliki Gileadi.

201:20 Lk 4:26; Yer 33:13; 1Fal 17:9-10Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani

watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta.

Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu

watamiliki miji ya Negebu.

211:21 Dan 2:24, 44; Ufu 11:15; Zek 14:9; Isa 19:20; Amu 3:9; Za 22:28; 47:9Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni

kutawala milima ya Esau.

Nao ufalme utakuwa wa Bwana.

New International Reader’s Version

Obadiah 1:1-21

Obadiah’s Vision

1This is the vision about Edom that Obadiah had.

Here is what the Lord and King says about Edom.

We’ve heard a message from the Lord.

A messenger was sent to the nations.

The Lord told him to say,

“Get up! Let us go and make war against Edom.”

2The Lord says to Edom,

“I will make you weak among the nations.

They will look down on you.

3You live in the safety of the rocks.

You make your home high up in the mountains.

But your proud heart has tricked you.

So you say to yourself,

‘No one can bring me down to the ground.’

4You have built your home as high as an eagle does.

You have made your nest among the stars.

But I will bring you down from there,”

announces the Lord.

5“Edom, suppose robbers came to you at night.

They would steal only as much as they wanted.

Suppose grape pickers came to harvest your vines.

They would still leave a few grapes.

But you are facing horrible trouble!

6People of Esau, everything will be taken away from you.

Your hidden treasures will be stolen.

7All those who are helping you

will force you to leave your country.

Your friends will trick you and overpower you.

Those who eat bread with you

will set a trap for you.

But you will not see it.”

8Here is what the Lord announces. “At that time

I will destroy the wise men of Edom.

I will wipe out the men of understanding

in the mountains of Esau.

9People of Teman, your soldiers will be terrified.

Everyone in Esau’s mountains

will be cut down by swords.

10You did harmful things to the people of Jacob.

They are your relatives.

So you will be covered with shame.

You will be destroyed forever.

11Outsiders entered the gates of Jerusalem.

They cast lots to see what each one would get.

Strangers carried off its wealth.

When that happened, you just stood there and did nothing.

You were like one of them.

12That was a time of trouble for your relatives.

So you shouldn’t have been happy about what happened to them.

The people of Judah were destroyed.

So you should not have been happy about it.

You should not have laughed at them so much

when they were in trouble.

13You should not have marched

through the gates of my people’s city

when they were in trouble.

You shouldn’t have been happy about what happened to them.

You should not have stolen their wealth

when they were in trouble.

14You waited where the roads cross.

You wanted to cut down those who were running away.

You should not have done that.

You handed over to their enemies

those who were still left alive.

You should not have done that.

They were in trouble.

15“The day of the Lord is near

for all the nations.

Others will do to you

what you have done to them.

You will be paid back

for what you have done.

16You Edomites made my holy mountain of Zion impure

by drinking and celebrating there.

So all the nations will drink

from the cup of my anger.

And they will keep on drinking from it.

They will vanish.

It will be as if they had never existed.

17But on Mount Zion some of my people will be left alive.

I will save them.

Zion will be my holy mountain once again.

And the people of Jacob

will again receive the land as their own.

18They will be like a fire.

Joseph’s people will be like a flame.

The nation of Edom will be like straw.

Jacob’s people will set Edom on fire and burn it up.

No one will be left alive

among Esau’s people.”

The Lord has spoken.

19Israelites from the Negev Desert

will take over Esau’s mountains.

Israelites from the western hills

will possess the land of the Philistines.

They’ll take over the territories

of Ephraim and Samaria.

Israelites from the tribe of Benjamin

will possess the land of Gilead.

20Some Israelites were forced to leave their homes.

They’ll come back to Canaan and possess

it all the way to the town of Zarephath.

Some people from Jerusalem were taken

to the city of Sepharad.

They’ll return and possess

the towns of the Negev Desert.

21Leaders from Mount Zion will go

and rule over the mountains of Esau.

And the kingdom will belong to the Lord.