Nehemia 6 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nehemia 6:1-19

Upinzani Zaidi Wakati Wa Ujenzi

16:1 Neh 2:10-19; 3:1-3Habari zilipofika kwa Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu, na adui zetu wengine kwamba nimejenga tena ukuta na hakuna nafasi iliyobakia ndani mwake, ingawa mpaka wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango, 26:2 1Nya 8:12; Mit 26:24; Neh 11:25, 35; Za 12:2; Mit 26:24Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Njoo, tukutane katika mojawapo ya vijiji katika nchi tambarare ya Ono.”

Lakini walikuwa wakikusudia kunidhuru. 36:3 Mit 14:15Kwa hiyo niliwatuma wajumbe kwao na majibu haya: “Kazi ninayoifanya ni kubwa sana, siwezi kuja. Kwa nini niiache kazi isimame nije kwenu?” 46:4 Mit 1:10Mara nne walinitumia ujumbe wa namna iyo hiyo, na kila mara niliwapa jibu lile lile.

56:5 Neh 2:10Basi, mara ya tano, Sanbalati akamtuma msaidizi wake kwangu akiwa na ujumbe wa aina ile ile, naye alikuwa amechukua mkononi mwake barua isiyofungwa, 66:6 Neh 2:19; Yer 9:3iliyokuwa imeandikwa:

“Habari imeenezwa miongoni mwa mataifa, naye Geshemu anasema kwamba ni kweli, kuwa wewe na Wayahudi mnafanya hila ya kuasi, ndiyo sababu mnajenga ukuta. Zaidi ya hayo, kufuatana na taarifa hizi, karibuni utakuwa mfalme wao, 76:7 1Tim 5:20; Za 15:5; Mt 27:5; 15:17na hata umewateua manabii wafanye tangazo hili kukuhusu wewe huko Yerusalemu: ‘Yuko mfalme katika Yuda!’ Sasa taarifa hii itarudishwa kwa mfalme. Basi njoo, tufanye shauri pamoja.”

86:8 Ay 13:4; Isa 59:4; Dan 11:27Nilimpelekea jibu hili: “Hakuna jambo kama hilo unalosema linalofanyika. Unalitunga tu kwenye kichwa chako.”

96:9 Kum 33:25; Za 56:3; Isa 41:10; 2Kor 12:9Wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakifikiri hivi: “Mikono ya watu italegea kiasi kwamba hawataweza kufanya kazi, nayo haitakamilika.”

Lakini niliomba, “Ee Mungu, sasa nitie mikono yangu nguvu.”

106:10 Hes 18:7Siku moja nilikwenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, ambaye alikuwa amefungwa ndani ya nyumba yake. Akasema, “Tukutane katika nyumba ya Mungu, ndani ya Hekalu, na tufunge milango ya Hekalu, kwa sababu watu wanakuja kukuua. Naam, wanakuja usiku kukuua.”

116:11 Mit 28:1Lakini nikasema, “Je, mtu kama mimi akimbie? Au mtu kama mimi aende Hekaluni kuokoa maisha yake? Sitakwenda!” 126:12 Eze 13:22-23; Neh 2:10Nilitambua kwamba Mungu hakumtuma, bali alitabiri dhidi yangu kwa sababu Tobia na Sanbalati walikuwa wamemwajiri. 136:13 Yer 20:10Alikuwa ameajiriwa kunitisha ili kwa kufanya jambo hili nitende dhambi, kisha waweze kuniharibia jina langu na kuniaibisha.

146:14 Neh 13:29; Kut 15:20; Yer 23:9-40; Zek 13:2-3; Ufu 2:20Ee Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati kwa sababu ya yale waliyotenda. Pia kumbuka nabii mke Noadia na manabii wengine ambao wamekuwa wakijaribu kunitisha.

Kukamilika Kwa Ukuta

15Basi ukuta ukakamilika siku ya ishirini na tano mwezi wa Eluli,6:15 Eluli ni mwezi wa sita kwenye kalenda ya Kiyunani; katika kalenda yetu ni Agosti/Septemba. kazi ambayo ilichukua siku hamsini na mbili. 166:16 Neh 2:10; 4:1; 6:1; Za 126:2Adui zetu wote waliposikia kuhusu hili, mataifa yote yaliyotuzunguka yakaogopa na kupoteza ujasiri, kwa sababu yalitambua kuwa kazi hii imefanyika kwa msaada wa Mungu wetu.

176:17 2Sam 9:7; 1Fal 18:19Pia katika siku hizo wakuu wa Yuda walikuwa wakituma barua nyingi kwa Tobia, nayo majibu yaliyotoka kwa Tobia yaliendelea kuwajia. 18Kwa kuwa watu wengi katika Yuda walikuwa wamemwapia Tobia, kwani alikuwa mkwewe Shekania mwana wa Ara, na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti wa Meshulamu mwana wa Berekia. 19Zaidi ya hayo, walikuwa wakiniarifu jinsi Tobia alivyo mtu mwema, nao walimwambia kila kitu nilichosema. Naye Tobia alituma barua za kunitisha.

New Russian Translation

Неемия 6:1-19

Дальнейшее противодействие строительству стены

1Когда Санбаллату, Товии, арабу Гешему и прочим нашим врагам донесли, что я отстроил стену и в ней не осталось ни одного незаделанного пролома (хотя к тому времени я еще не поставил двери ворот), 2Санбаллат и Гешем послали сказать мне:

– Давай встретимся в одном из селений на равнине Оно.

Но они замышляли причинить мне зло, 3и я послал к ним вестников с таким ответом:

– Я занят важной работой и не могу прийти. Зачем останавливать работу из-за того, чтобы пойти к вам?

4Четыре раза они присылали ко мне с этим посланием, и четыре раза я давал им этот ответ. 5Тогда в пятый раз Санбаллат отправил ко мне с этим же посланием своего слугу. В руке у него было незапечатанное письмо, 6в котором было написано:

«Среди народов ходит слух, и Гешем6:6 Евр.: «Гашму». говорит, что ты и иудеи замышляете восстать, и поэтому ты строишь стену. По этим слухам ты собираешься стать их царем 7и даже назначил пророков, чтобы возвещать о себе в Иерусалиме: „В Иудее есть царь!“ Этот слух дойдет до царя. Итак, приходи, давай вместе посоветуемся».

8Я послал ему ответ: «Нет никакой правды в том, что ты говоришь. Все это ты выдумываешь сам».

9Все они старались запугать нас, думая: «Их руки очень ослабнут, чтобы делать эту работу, и она не будет завершена».

Но я молился:

– Укрепи мои руки.

10Однажды я пришел в дом Шемаи, сына Делаи, внука Мегетавела, который заперся в своем доме. Он сказал:

– Давай встретимся в доме Божьем, внутри храма, и запрем храмовые двери, потому что тебя придут убить, и придут ночью!

11Но я сказал:

– Разве такой человек, как я, может бежать? Может ли такой, как я, пойти в храм, чтобы спасти свою жизнь? Не пойду!

12Я понимал, что Бог не посылал его, и он пророчествовал против меня, потому что его наняли Товия и Санбаллат. 13Его наняли запугать меня, чтобы я согрешил, сделав так, а они бы лишили меня доброго имени и упрекали бы меня.

14Вспомни, Боже мой, Товию и Санбаллата по их делам; вспомни еще и пророчицу Ноадию и прочих пророков, которые пытались меня запугать.

Завершение восстановления стены

15Стена была завершена в двадцать пятый день месяца элула6:15 2 октября 445 г. до н. э., за пятьдесят два дня. 16Когда об этом услышали все наши враги, все окрестные народы испугались6:16 Другое чтение: «увидели». и потеряли свою самоуверенность, потому что поняли, что эта работа была сделана с помощью нашего Бога.

17Еще в те дни знать Иудеи посылала много писем Товии, а письма Товии приходили к ним. 18Ведь многие в Иудее были связаны с ним клятвой, потому что он был зятем Шекании, сына Араха, а его сын Иоханан женился на дочери Мешуллама, сына Берехии. 19Они даже говорили при мне о его добрых делах, а после пересказывали ему то, что я сказал. А Товия присылал письма, чтобы меня запугать.