Nehemia 6 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nehemia 6:1-19

Upinzani Zaidi Wakati Wa Ujenzi

16:1 Neh 2:10-19; 3:1-3Habari zilipofika kwa Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu, na adui zetu wengine kwamba nimejenga tena ukuta na hakuna nafasi iliyobakia ndani mwake, ingawa mpaka wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango, 26:2 1Nya 8:12; Mit 26:24; Neh 11:25, 35; Za 12:2; Mit 26:24Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Njoo, tukutane katika mojawapo ya vijiji katika nchi tambarare ya Ono.”

Lakini walikuwa wakikusudia kunidhuru. 36:3 Mit 14:15Kwa hiyo niliwatuma wajumbe kwao na majibu haya: “Kazi ninayoifanya ni kubwa sana, siwezi kuja. Kwa nini niiache kazi isimame nije kwenu?” 46:4 Mit 1:10Mara nne walinitumia ujumbe wa namna iyo hiyo, na kila mara niliwapa jibu lile lile.

56:5 Neh 2:10Basi, mara ya tano, Sanbalati akamtuma msaidizi wake kwangu akiwa na ujumbe wa aina ile ile, naye alikuwa amechukua mkononi mwake barua isiyofungwa, 66:6 Neh 2:19; Yer 9:3iliyokuwa imeandikwa:

“Habari imeenezwa miongoni mwa mataifa, naye Geshemu anasema kwamba ni kweli, kuwa wewe na Wayahudi mnafanya hila ya kuasi, ndiyo sababu mnajenga ukuta. Zaidi ya hayo, kufuatana na taarifa hizi, karibuni utakuwa mfalme wao, 76:7 1Tim 5:20; Za 15:5; Mt 27:5; 15:17na hata umewateua manabii wafanye tangazo hili kukuhusu wewe huko Yerusalemu: ‘Yuko mfalme katika Yuda!’ Sasa taarifa hii itarudishwa kwa mfalme. Basi njoo, tufanye shauri pamoja.”

86:8 Ay 13:4; Isa 59:4; Dan 11:27Nilimpelekea jibu hili: “Hakuna jambo kama hilo unalosema linalofanyika. Unalitunga tu kwenye kichwa chako.”

96:9 Kum 33:25; Za 56:3; Isa 41:10; 2Kor 12:9Wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakifikiri hivi: “Mikono ya watu italegea kiasi kwamba hawataweza kufanya kazi, nayo haitakamilika.”

Lakini niliomba, “Ee Mungu, sasa nitie mikono yangu nguvu.”

106:10 Hes 18:7Siku moja nilikwenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, ambaye alikuwa amefungwa ndani ya nyumba yake. Akasema, “Tukutane katika nyumba ya Mungu, ndani ya Hekalu, na tufunge milango ya Hekalu, kwa sababu watu wanakuja kukuua. Naam, wanakuja usiku kukuua.”

116:11 Mit 28:1Lakini nikasema, “Je, mtu kama mimi akimbie? Au mtu kama mimi aende Hekaluni kuokoa maisha yake? Sitakwenda!” 126:12 Eze 13:22-23; Neh 2:10Nilitambua kwamba Mungu hakumtuma, bali alitabiri dhidi yangu kwa sababu Tobia na Sanbalati walikuwa wamemwajiri. 136:13 Yer 20:10Alikuwa ameajiriwa kunitisha ili kwa kufanya jambo hili nitende dhambi, kisha waweze kuniharibia jina langu na kuniaibisha.

146:14 Neh 13:29; Kut 15:20; Yer 23:9-40; Zek 13:2-3; Ufu 2:20Ee Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati kwa sababu ya yale waliyotenda. Pia kumbuka nabii mke Noadia na manabii wengine ambao wamekuwa wakijaribu kunitisha.

Kukamilika Kwa Ukuta

15Basi ukuta ukakamilika siku ya ishirini na tano mwezi wa Eluli,6:15 Eluli ni mwezi wa sita kwenye kalenda ya Kiyunani; katika kalenda yetu ni Agosti/Septemba. kazi ambayo ilichukua siku hamsini na mbili. 166:16 Neh 2:10; 4:1; 6:1; Za 126:2Adui zetu wote waliposikia kuhusu hili, mataifa yote yaliyotuzunguka yakaogopa na kupoteza ujasiri, kwa sababu yalitambua kuwa kazi hii imefanyika kwa msaada wa Mungu wetu.

176:17 2Sam 9:7; 1Fal 18:19Pia katika siku hizo wakuu wa Yuda walikuwa wakituma barua nyingi kwa Tobia, nayo majibu yaliyotoka kwa Tobia yaliendelea kuwajia. 18Kwa kuwa watu wengi katika Yuda walikuwa wamemwapia Tobia, kwani alikuwa mkwewe Shekania mwana wa Ara, na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti wa Meshulamu mwana wa Berekia. 19Zaidi ya hayo, walikuwa wakiniarifu jinsi Tobia alivyo mtu mwema, nao walimwambia kila kitu nilichosema. Naye Tobia alituma barua za kunitisha.

La Bible du Semeur

Néhémie 6:1-19

Tentatives d’intimidation

1Lorsque Sanballat, Tobiya, Guéshem l’Arabe et le reste de nos ennemis apprirent que j’avais fini de rebâtir la muraille et qu’il n’y restait plus de brèche – sauf les portes dont je n’avais pas encore posé les battants à cette époque – 2Sanballat et Guéshem m’envoyèrent un message pour me dire : Viens et ayons ensemble une entrevue à Kefirim, dans la vallée d’Ono6.2 Kefirim: localité inconnue, dans la plaine de Saron, au nord de Lydda, dans la partie la plus à l’ouest de la région occupée par les rapatriés (Né 7.37 ; 11.35)..

Ils avaient l’intention de me faire du mal.

3Je leur envoyai des messagers pour leur répondre : J’ai un grand travail à exécuter et il m’est impossible de me rendre auprès de vous. Je n’ai pas de raison d’interrompre l’ouvrage en l’abandonnant pour aller vous rencontrer.

4A quatre reprises, ils me firent transmettre la même proposition, et je leur retournai la même réponse. 5Une cinquième fois, Sanballat m’envoya ce même message par son serviteur qui tenait à la main une lettre ouverte. 6Il y était écrit :

« Le bruit se répand parmi les peuples des régions environnantes que toi et les Juifs, vous projetez une révolte. Guéshem me l’a d’ailleurs confirmé. Ce serait pour cela que tu reconstruis la muraille. On dit même que tu veux devenir leur roi 7et que tu as déjà désigné des prophètes chargés de proclamer à Jérusalem que tu es devenu roi de Juda. Maintenant, des rumeurs de ce genre arriveront certainement aux oreilles de l’empereur. Viens donc en discuter avec nous ! »

8Je lui fis répondre : Rien de ce que tu affirmes n’est exact. Tout ceci est une pure invention de ta part !

9Tous ces gens, en effet, ne cherchaient qu’à nous faire peur ; ils espéraient que nous nous découragerions et que nous abandonnerions l’ouvrage !

Maintenant, ô Dieu, fortifie-moi pour ma tâche6.9 Les mots : ô Dieu ne sont pas dans l’hébreu. Mais il semble bien s’agir d’une courte prière. Les anciennes versions ont : Maintenant, je fortifierai mes mains. !

L’intervention d’un faux prophète

10Je me rendis chez Shemaya, fils de Delaya et petit-fils de Mehétabéel, qui s’était barricadé chez lui. Il s’écria : Allons tenir conseil dans le temple de Dieu, au fond du sanctuaire, et verrouillons-en les portes, car ils veulent te tuer : ils vont venir pendant la nuit pour t’assassiner.

11Mais je lui répondis : Comment un homme dans ma position prendrait-il la fuite ? D’ailleurs, quel homme comme moi pourrait pénétrer dans le Temple sans perdre la vie6.11 Nb 18.7 interdit à ceux qui n’étaient pas prêtres de pénétrer à l’intérieur du tabernacle et du Temple (voir 2 Ch 26.16-21). ? Non, je n’irai pas !

12J’avais bien compris que ce n’était pas Dieu qui l’envoyait. Mais il avait prononcé cette prophétie pour moi parce que Sanballat et Tobiya l’avaient soudoyé. 13Ils avaient agi ainsi pour me faire peur, et pour qu’en suivant son conseil, je commette un péché. Alors ils auraient pu me faire une mauvaise réputation et me discréditer.

14Mon Dieu, ne laisse pas Sanballat et Tobiya impunis pour leurs actes, ni Noadia la prophétesse, ni les autres prophètes qui ont cherché à me faire peur.

La confusion des ennemis

15La muraille fut achevée en cinquante-deux jours, le vingt-cinq du mois d’Eloul6.15 Le 3 octobre 445 av. J.-C. (ou fin septembre selon certains). L’assemblée solennelle du peuple fut tenue cinq jours plus tard (8.1-2). La dédicace de la muraille est décrite en 12.27-47.. 16Lorsque tous nos ennemis l’apprirent, tous les peuples étrangers qui nous entouraient furent saisis de crainte et profondément humiliés à leurs propres yeux, car ils reconnurent qu’un tel ouvrage n’avait pu être mené à bonne fin qu’avec l’aide de notre Dieu.

17Durant toute cette période, des notables de Juda entretenaient une abondante correspondance avec Tobiya. 18En effet, beaucoup de Judéens étaient liés à lui par serment parce qu’il était le gendre de Shekania, fils d’Arah, et que son propre fils Yohanân avait épousé la fille de Meshoullam, fils de Bérékia. 19Ils avaient même l’audace de vanter ses mérites en ma présence, et ils lui rapportaient mes paroles. C’était ce Tobiya qui envoyait des lettres pour m’intimider.