Nehemia 3 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nehemia 3:1-32

Wajenzi Wa Ukuta

13:1 Yer 31:38; Ezr 10:24; Neh 12:39; Za 48:12; Yn 5:2; Isa 58:2; Zek 14:10Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli. 23:2 Ezr 2:34; Neh 7:36Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.

33:3 2Nya 33:14; Neh 12:39; Sef 1:10; Neh 6:1Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo. 43:4 Ezr 8:33Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana. 53:5 Neh 3:27; 2Sam 14:2Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.

63:6 Neh 12:36Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo. 73:7 Yos 9:3; Neh 2:7-8Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati. 83:8 Neh 12:38Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana. 9Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia. 10Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia. 113:11 Neh 12:38; Ezr 2:32Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru. 123:12 Kut 15:25; Lk 8:3; Flp 4:3Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.

133:13 Neh 2:13; 2Nya 26:9; Yos 15:34Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.

143:14 Yer 6:1; Mik 1:11Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.

153:15 Yos 18:26; Amu 20:1-3; Isa 8:6; Yn 9:7Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi. 163:16 Yos 15:58; Wim 3:7; Mdo 2:29Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.

173:17 Yos 15:44Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake. 183:18 Yos 15:44; 1Sam 23:1Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila. 193:19 2Nya 26:9Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta. 203:20 Mhu 9:10; Rum 12:11Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu. 213:21 Ezr 8:33Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.

22Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji. 23Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake. 243:24 Yer 3:19; Ezr 8:33Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta. 253:25 Yer 32:2; 37:21; Ezr 2:3Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi, 263:26 Ezr 2:43; Neh 7:46; 2Nya 33:14; Neh 12:37; 8:1-3na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza. 273:27 Za 48:12; Neh 3:5Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.

283:28 2Nya 23:15; Yer 31:40; 2Fal 11:16Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake. 293:29 Yer 19:2Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati. 30Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi. 31Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu3:31 Yaani Wanethini. na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe. 323:32 Neh 12:39; Yn 5:2Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.

Swedish Contemporary Bible

Nehemja 3:1-32

Fördelning av arbetet

1Översteprästen Eljashiv och de andra prästerna började bygga upp Fårporten, helgade den och satte in dörrarna. Därefter fortsatte de ända bort till Hundradetornet och Hananeltornet3:1 Det är också möjligt att Hundradetornet och Hananeltornet var namn på ett och samma torn.. 2Bredvid dem byggde männen från Jeriko, och bredvid dem Imris son Sackur.

3Fiskporten byggdes av Hassenaas söner. De timrade upp den, gjorde i ordning bjälkarna och satte in dörrar, lås och bommar. 4Meremot, son till Uria och sonson till Hackos, arbetade bredvid dem, och sedan följde Meshullam, son till Berekja och sonson till Meshesavel, och bredvid dem Sadok, Baanas son. 5Bredvid dem arbetade män från Tekoa på nästa avsnitt, men de förnämsta bland dem ville inte böja sig för att tjäna sin herre.

6Jeshanaporten3:6 Eller Gamla porten. reparerades av Jojada, Paseachs son, och Meshullam, Besodejas son. De timrade upp den och satte in dörrar med lås och bommar. 7Intill dem arbetade Melatja från Givon och Jadon från Meronot, männen från Givon och Mispa, som lydde under ståthållaren i provinsen väster om Eufrat. 8Guldsmeden Ussiel, Harhajas son, arbetade bredvid dem, och bredvid honom Hananja, som var parfymtillverkare. De återuppbyggde Jerusalem ända fram till Breda muren3:8 Betydelsen av den sista delen av versen är osäker; möjligen kan den också tolkas som att man utelämnade eller avstod från en del av Jerusalem ända fram till Breda muren..

9Refaja, Hurs son, ledare för ena hälften av Jerusalems område, arbetade närmast dem. 10Jedaja, Harumafs son, arbetade därnäst, intill sitt eget hus, och bredvid honom Hashavnejas son Hattush. 11Malkia, Harims son, och Hashuv, Pachat Moabs son, arbetade på nästa mursträcka och på Ugnstornet. 12Shallum, Hallocheshs son, ledare för den andra hälften av Jerusalemområdet, arbetade bredvid dem tillsammans med sina döttrar.

13Dalporten reparerade Hanun och invånarna i Sanoach. De byggde upp den och satte in dörrar, lås och bommar. De reparerade också en halv kilometer av muren fram till Dyngporten.

14Dyngporten reparerades av Malkia, Rekavs son, ledare för Bet-Hackeremdistriktet. Han byggde upp den och satte in dess dörrar, lås och bommar.

15Shallun, Kol-Hoses son, ledare för Mispadistriktet, reparerade Källporten. Han byggde upp den, lade tak på den och satte in dess dörrar med lås och bommar. Sedan reparerade han muren vid vattenledningsdammen intill den kungliga trädgården ända fram till de trappor som leder ner från Davids stad. 16Närmast honom arbetade Asbuks son Nehemja, ledare för ena hälften av Bet-Surdistriktet. Han byggde upp muren fram till Davids gravar, vattenreservoaren och Hjältehuset.

17Intill honom arbetade leviter: Banis son Rechum, bredvid honom Hashavja, ledare för den ena hälften av Keiladistriktet, som reparerade sitt distrikts del. 18Intill dem arbetade deras bröder under Bavvaj3:18 Enligt en del handskrifter Binnuj., Henadads son, ledare för den andra hälften av Keiladistriktet.

19Bredvid dem arbetade Eser, Jeshuas son, ledare i Mispa, på mursektionen mitt emot uppgången till vapenförrådet, vid murvinkeln3:19 Grundtextens exakta innebörd är osäker.. 20Närmast honom reparerade Baruk, Sabbajs3:20 Eller Sackajs. son, ivrigt mursträckan från murvinkeln fram till översteprästen Eljashivs hus. 21Intill honom reparerade Urias son Meremot en mursträcka från ingången till Eljashivs hus till husets slut.

22Därnäst arbetade prästerna från stadens omgivningar. 23Intill dem arbetade Benjamin och Hashuv utanför sina egna hus, och sedan Asarja, Maasejas son och Ananjas sonson, invid sitt hus. 24Sedan kom Binnuj, Henadads son, som reparerade en mursträcka från Asarjas hus fram till murvinkeln och hörnet. 25Usajs son Palal fortsatte mitt emot vinkeln och tornet som skjuter ut från det övre kungapalatset, nära fängelsegården. Intill honom arbetade Paroshs son Pedaja 26och tempeltjänarna som bodde på Ofel, fram till östra Vattenporten och det framskjutande tornet. 27Tekoaiterna arbetade därnäst med sektionen mitt emot det stora utskjutande tornet och bort till Ofelmuren. 28Prästerna reparerade muren ovanför Hästporten, var och en framför sitt eget hus.

29Immers son Sadok arbetade intill dem vid muren framför sitt eget hus, och intill honom Shemaja, Shekanjas son, som var vakt vid Östra porten. 30Därnäst arbetade Hananja, Shelemjas son, och Hanun, Salafs sjätte son på nästa sträcka. Meshullam, Berekjas son, reparerade muren mitt emot sin tempelkammare. 31Intill honom arbetade Malkia, en av guldsmederna, ända bort till tempeltjänarnas och köpmännens hus mitt emot Mönstringsporten och vidare fram till övre Hörnsalen. 32Guldsmederna och köpmännen reparerade muren mellan övre Hörnsalen och Fårporten.