Nehemia 13 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nehemia 13:1-31

Nehemia Afanya Matengenezo Ya Mwisho

113:1 Amo 2:1-3; Kum 23:3Siku hiyo, Kitabu cha Mose kilisomwa kwa sauti kuu, na watu wote wakasikia. Humo ilionekana imeandikwa kwamba hakuna Mwamoni wala Mmoabu atakayeruhusiwa katika kusanyiko la watu wa Mungu, 213:2 Hes 22:3-11; 23:7; 23:8-11; Kum 23:3-5kwa sababu hawakuwalaki Waisraeli kwa chakula na maji. Badala yake walimwajiri Balaamu kuwalaani (lakini hata hivyo Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka). 313:3 Neh 9:2; Yak 1:27Watu waliposikia sheria hii, waliwatenga watu wote wasio Waisraeli waliokuwa wa uzao wa kigeni.

413:4 Neh 12:44; 2:10Kabla ya hili, kuhani Eliashibu alikuwa amewekwa kuwa msimamizi wa vyumba vya ghala ya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano wa karibu na Tobia, 513:5 Law 27:30; Hes 18:21naye alikuwa amempa Tobia chumba kikubwa ambacho mwanzo kilikuwa kikitumika kuweka sadaka za nafaka, uvumba na vyombo vya Hekalu, pamoja na zaka za nafaka, divai mpya na mafuta waliyoagizwa Waisraeli kwa ajili ya Walawi, waimbaji na mabawabu wa lango, pamoja na matoleo kwa makuhani.

613:6 Neh 5:14; 2:6Lakini wakati haya yote yalipokuwa yakitendeka, sikuwa Yerusalemu, kwa kuwa katika mwaka wa thelathini na mbili wa utawala wa Artashasta mfalme wa Babeli nilikuwa nimerudi kwa mfalme. Baadaye nilimwomba ruhusa, 713:7 Ezr 10:24nikarudi Yerusalemu. Hapo niligundua jambo la uovu alilofanya Eliashibu kwa kumpa Tobia chumba katika nyua za nyumba ya Mungu. 813:8 Mk 11:15-17; Yn 2:13; Lk 19:45-46Nilikasirika sana na nikavitupa nje vyombo vyote vya Tobia. 913:9 1Nya 23:28; 2Nya 29:5Nilitoa amri kutakasa vyumba, kisha nikavirudisha vifaa vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka za nafaka na uvumba.

1013:10 Kum 12:19; Hes 35:2Pia niligundua kuwa mafungu yaliyopangwa kupewa Walawi hawakuwa wamepewa, nao Walawi wote na waimbaji waliowajibika kwa huduma walikuwa wamerudi katika mashamba yao. 1113:11 Hag 1:9; 1Sam 2:17; Mal 3:8-9Basi niliwakemea maafisa na kuwauliza, “Kwa nini nyumba ya Mungu imepuuzwa?” Kisha niliwaita pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.

1213:12 Kum 18:8; 2Nya 31:5-6Yuda wote walileta zaka za nafaka, divai mpya na mafuta kwenye ghala. 1313:13 Neh 12:44; Mdo 6:1-5Nikamweka kuhani Shelemia, mwandishi Sadoki, na Mlawi aliyeitwa Pedaya kuwa wasimamizi wa ghala, na kumfanya Hanani mwana wa Zakuri, mwana wa Matania kuwa msaidizi wao, kwa sababu watu hawa walionekana kuwa waaminifu. Walipewa wajibu wa kugawa mahitaji kwa ndugu zao.

1413:14 Neh 5:19; Mwa 8:1; 2Fal 20:3Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa hili, wala usifute kile nilichokifanya kwa uaminifu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na kwa ajili ya huduma yake.

1513:15 Kut 34:21; Kum 5:12-15Siku hizo nikaona watu katika Yuda wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya Sabato na kuleta nafaka wakiwapakiza punda, pamoja na divai, zabibu, tini na aina nyingine za mizigo. Nao walikuwa wakileta haya yote Yerusalemu siku ya Sabato. Kwa hiyo niliwaonya dhidi ya kuuza vyakula siku hiyo. 1613:16 Neh 10:31Watu kutoka Tiro waliokuwa wakiishi Yerusalemu walileta samaki na aina nyingi za bidhaa na kuziuza Yerusalemu siku ya Sabato kwa watu wa Yuda. 1713:17 Neh 13:11Niliwakemea wakuu wa Yuda na kuwaambia, “Ni uovu gani huu mnaofanya wa kuinajisi siku ya Sabato? 1813:18 Neh 10:31; Yer 17:21-23Je, baba zenu hawakufanya mambo kama haya, hata wakamsababisha Mungu wetu kuleta maafa haya yote juu yetu na juu ya mji huu? Sasa bado mnazidi kuchochea ghadhabu yake dhidi ya Israeli kwa kuinajisi Sabato.”

1913:19 Law 23:32; Kut 31:14-17Wakati vivuli vya jioni vilipoangukia juu ya malango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe, wala isifunguliwe mpaka Sabato iishe. Nikawaweka baadhi ya watu wangu mwenyewe kwenye malango ili pasiwepo mzigo utakaoingizwa ndani siku ya Sabato. 20Mara moja au mbili wachuuzi na wauzaji wa bidhaa za aina zote walilala usiku nje ya mji wa Yerusalemu. 21Lakini niliwaonya na kuwaambia, “Kwa nini mnalala karibu na ukuta? Kama mkifanya hivi tena, nitawaadhibu.” Kuanzia wakati ule hawakuja tena siku ya Sabato. 2213:22 Mwa 8:1; Neh 1:8Kisha nikawaamuru Walawi kujitakasa na kwenda kulinda malango ili kutunza Sabato iwe takatifu.

Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya hili pia, nawe unionyeshe wema wako sawasawa na upendo wako mkuu.

2313:23 Neh 12:30; Ezr 9:1-2; Mal 2:11; Kut 34:16; Rut 1:4Zaidi ya hayo, niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake kutoka Ashdodi, Amoni na Moabu. 2413:24 Es 1:22; 3:12; 8:9Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Kiashidodi au lugha ya watu wengine, bali hawakuweza kuzungumza Kiyahudi. 2513:25 Ezr 10:5; Mit 28:4; Neh 10:29-30Niliwakemea na kuwalaani. Niliwapiga baadhi ya watu na kungʼoa nywele zao. Niliwaapisha kwa jina la Mungu na kusema: “Msiwaoze binti zenu kwa wana wao, wala binti zao wasiolewe na wana wenu wala ninyi wenyewe. 2613:26 1Fal 3:13; 2Nya 1:12Je, Solomoni hakutenda dhambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwepo mfalme kama yeye. Alipendwa na Mungu wake. Naye Mungu alimweka kuwa mfalme juu ya Israeli yote, lakini hata yeye, wanawake wa mataifa mengine walimfanya atende dhambi. 2713:27 Ezr 9:14; 10:2Je, tulazimike sasa kusikia kwamba ninyi pia mmefanya uovu huu mkubwa na kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”

2813:28 Ezr 10:24; Neh 10:30Mmoja wa wana wa Yoyada mwana wa Eliashibu kuhani mkuu alikuwa mkwewe Sanbalati Mhoroni. Nami nilimfukuza mbele yangu.

2913:29 Neh 10:34; Mwa 8:1; Neh 1:8Ee Mungu wangu, uwakumbuke, kwa sababu wamenajisi ukuhani, na agano la kikuhani na la Walawi.

3013:30 Neh 9:2Kwa hiyo niliwatakasa makuhani na Walawi kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni, na kuwapa wajibu, kila mmoja katika kazi yake. 3113:31 Neh 10:34; 10:35-36; Mwa 8:1; Neh 1:8Pia nilihakikisha kwamba matoleo ya kuni yaliletwa kwa wakati unaopaswa, na malimbuko kwa wakati wake.

Ee Mungu wangu, unikumbuke, unitendee mema.

La Bible du Semeur

Néhémie 13:1-31

La séparation d’avec les étrangers

1A cette époque, au cours d’une lecture du livre de Moïse en présence du peuple, on y trouva écrit que ni l’Ammonite, ni le Moabite ne seraient jamais admis dans la communauté de Dieu13.1 Voir Dt 23.4-6., 2parce qu’ils n’étaient pas venus à la rencontre des Israélites pour leur donner du pain et de l’eau. Au contraire, ils avaient soudoyé Balaam pour qu’il les maudisse ; mais notre Dieu avait changé la malédiction en bénédiction13.2 Voir Nb 22.1-6 ; Dt 23.3-5.. 3Dès que l’on eut entendu le texte de cette loi, on exclut tous les étrangers de la communauté d’Israël.

4Avant cette décision, le prêtre Eliashib, chargé de la responsabilité des salles du Temple et proche parent de Tobiya13.4 Qui était ammonite., 5avait mis à la disposition de ce dernier une grande salle où étaient précédemment entreposés les offrandes végétales, l’encens, les ustensiles, la dîme du blé, du vin nouveau et de l’huile, c’est-à-dire les redevances ordonnées par la Loi pour les lévites, les musiciens et les portiers, ainsi que les contributions revenant aux prêtres.

6J’étais absent de Jérusalem quand cela eut lieu, car j’étais retourné auprès d’Artaxerxès, le roi de Babylone, la trente-deuxième année de son règne13.6 En 433 av. J.-C. (voir 5.14). Près d’un an après sa conquête de Babylone, Cyrus avait pris le titre de « roi de Babylone » (Esd 5.13), et ses successeurs l’ont conservé à sa suite.. Au bout d’un certain temps, je sollicitai de l’empereur un nouveau congé 7et je retournai à Jérusalem. Là, je me rendis compte du mal qu’avait fait Eliashib en mettant une salle donnant sur le parvis du Temple à la disposition de Tobiya. 8J’en fus très irrité, et je jetai hors de la pièce tous les objets qui appartenaient à Tobiya. 9Puis je donnai ordre de procéder aux rites de purification pour les salles, et j’y fis remettre les objets du Temple, les offrandes et l’encens.

Les dîmes

10J’appris aussi que les parts des lévites ne leur avaient pas été remises13.10 Voir Dt 12.19. et que les lévites et les musiciens chargés des offices s’étaient retirés chacun sur ses terres. 11Aussi, je fis des reproches aux chefs du peuple et je leur dis : Pourquoi le temple de Dieu est-il laissé à l’abandon ?

Je rassemblai les lévites et les musiciens et je leur fis reprendre leurs fonctions. 12Alors tout le peuple de Juda apporta dans les magasins la dîme du blé, du vin nouveau et de l’huile13.12 Cf. Ml 3.10.. 13Je confiai l’intendance des magasins au prêtre Shélémia, à Tsadoq, spécialiste de la Loi, et à Pedaya, l’un des lévites. Je leur donnai pour les assister Hanân, fils de Zakkour, petit-fils de Mattania, car c’étaient tous des hommes que l’on considérait comme dignes de confiance. Ils furent chargés de faire les distributions à leurs collègues.

14Souviens-toi de moi, ô mon Dieu, pour tout cela, et n’oublie pas tout ce que j’ai fidèlement accompli pour ton temple et pour son culte.

Le jour du repos

15A la même époque, je remarquai en Juda des gens qui, un jour de sabbat, foulaient du raisin au pressoir, d’autres qui rentraient des gerbes, les chargeaient sur des ânes et transportaient du vin, des raisins, des figues et toutes sortes d’autres fardeaux pour les amener à Jérusalem en plein jour du repos. Je leur fis des reproches le jour où ils vendaient leurs marchandises13.15 Voir Ex 20.8-10 ; Dt 5.12-14 ; Jr 17.21-22.. 16Il y avait aussi des gens de Tyr qui s’étaient installés à Jérusalem. Ils y faisaient venir du poisson et toutes sortes d’autres marchandises pour les vendre aux Judéens et à Jérusalem le jour du sabbat. 17Je fis des reproches aux notables de Juda et je leur dis : Comment pouvez-vous laisser faire un si grand mal et profaner ainsi le jour du sabbat ! 18C’est exactement ainsi que vos ancêtres ont agi, et c’est bien à cause de cela que notre Dieu a fait venir tous ces malheurs sur nous et sur cette ville. Et vous, par votre manque de respect du jour du sabbat, vous allez encore aggraver sa colère contre Israël !

19Puis je donnai ordre de fermer les portes de Jérusalem dès la tombée de la nuit, avant le début du jour du sabbat et j’interdis de les rouvrir avant que ce jour soit passé. Je postai quelques-uns de mes serviteurs à proximité des portes pour veiller à ce qu’aucun fardeau ne soit introduit le jour du sabbat. 20Alors les commerçants et les marchands de toutes sortes de produits passèrent plusieurs fois la nuit à l’extérieur de Jérusalem. 21Je les avertis en ces termes : Pourquoi établissez-vous votre campement devant la muraille ? Si vous recommencez, je vous ferai arrêter.

Depuis ce jour-là, ils cessèrent de venir pendant le jour du sabbat. 22Puis j’ordonnai aux lévites d’accomplir les rites de purification et de venir surveiller les portes pour que le caractère sacré du jour du sabbat soit respecté.

De cela aussi, souviens-toi en ma faveur, ô mon Dieu, et fais-moi grâce dans ton immense bonté.

Les mariages mixtes

23A cette même époque, je constatai également que des Judéens avaient épousé des femmes ashdodiennes, ammonites et moabites13.23 Venant de pays environnants situés respectivement à l’ouest, à l’est et au sud-est de Juda. Voir la situation à laquelle Esdras avait dû faire face 25 ans plus tôt (Esd 9 et 10).. 24La moitié de leurs fils parlaient l’ashdodien et aucun ne savait la langue des Juifs ; ils ne connaissaient que celle de tel ou tel peuple. 25Je pris ces compatriotes à partie et j’appelai la malédiction sur eux ; je battis même quelques-uns d’entre eux et je leur arrachai les cheveux, puis je leur fis prêter serment au nom de Dieu en disant : Vous ne donnerez pas vos filles à des fils d’étrangers et vous ne prendrez leurs filles ni pour vos fils, ni pour vous-mêmes13.25 Voir Ex 34.11-16 ; Dt 7.1-5.. 26N’est-ce pas précisément ce genre d’unions qui a entraîné Salomon, roi d’Israël, dans le péché, lui qui n’avait pas son pareil parmi les rois des grandes nations étrangères, qui était aimé de son Dieu13.26 Voir 2 S 12.24-25. et que Dieu avait établi roi sur tout Israël ? Et pourtant, même lui fut entraîné dans le péché par les femmes étrangères13.26 Voir 1 R 11.1-8..

27Faut-il donc entendre dire de vous que vous commettez ce grand mal et que vous êtes infidèles à notre Dieu en épousant des femmes étrangères ?

28Un des fils de Yoyada et petit-fils d’Eliashib, le grand-prêtre, était devenu le gendre de Sanballat, le Horonite. C’est pourquoi je le chassai loin de moi.

29Souviens-toi de ces gens, ô mon Dieu, qui ont déshonoré la fonction sacerdotale et ton alliance avec les prêtres et les lévites.

Conclusion

30Je les purifiai donc de tout élément étranger et je remis en vigueur les règlements que devaient observer les prêtres et les lévites, chacun dans son service. 31Je rétablis aussi les offrandes de bois à fournir aux dates prescrites et celles des premiers produits de la terre.

Souviens-toi favorablement de moi, ô mon Dieu !