Nahumu 1 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nahumu 1:1-15

11:1 Isa 13:1; 19:1; Yer 23:33-34; 50:18; Mwa 10:11; Nah 2:8; 3:7Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.

Hasira Ya Mungu Dhidi Ya Ninawi

21:2 Kut 20:5; Mwa 4:24; Kum 32:41; 7:10; Za 94:1Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi;

Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu.

Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake,

naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.

31:3 Neh 9:17; Kut 34:7; 19:16; Za 103:8; Mik 7:18; 2Sam 22:10; Za 50:3; 104:3Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu,

Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia.

Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani,

na mawingu ni vumbi la miguu yake.

41:4 2Sam 22:16; Kut 14:22; Isa 33:9; Yos 3:15, 16Anakemea bahari na kuikausha,

anafanya mito yote kukauka.

Bashani na Karmeli zinanyauka

na maua ya Lebanoni hukauka.

51:5 Kut 19:18; Ay 9:6; 2Sam 22:8; Yoe 2:10; Eze 38:20; Mik 1:4Milima hutikisika mbele yake

na vilima huyeyuka.

Nchi hutetemeka mbele yake,

dunia na wote waishio ndani yake.

61:6 Za 130:3; Eze 22:14; Isa 5:24-25; 42:25; Yer 10:10; 1Fal 19:11Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu?

Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali?

Ghadhabu yake imemiminwa kama moto,

na miamba inapasuka mbele zake.

71:7 Yer 33:11; 17:17; Za 22:9; 1:6; 2Tim 2:19Bwana ni Mwema,

kimbilio wakati wa taabu.

Huwatunza wale wanaomtegemea,

81:8 Isa 8:7; Amo 8:8; Dan 9:26lakini kwa mafuriko makubwa,

ataangamiza Ninawi;

atafuatilia adui zake hadi gizani.

91:9 Hos 7:15Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana

yeye atalikomesha;

taabu haitatokea mara ya pili.

101:10 2Sam 23:6; Isa 49:26; 5:24; Mal 4:1Watasongwa katikati ya miiba

na kulewa kwa mvinyo wao.

Watateketezwa kama mabua makavu.

11Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja,

ambaye anapanga shauri baya

dhidi ya Bwana

na kushauri uovu.

121:12 Isa 10:34; 54:6-8; Mao 3:31-32Hili ndilo asemalo Bwana:

“Ingawa wana muungano nao ni wengi sana,

watakatiliwa mbali na kuangamia.

Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda,

sitakutesa tena.

131:13 Isa 9:4; Ay 12:18; Za 107:14Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako,

nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”

141:14 Isa 14:22; Mik 5:13; Yer 28:8; Eze 32:22-23Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi:

“Hutakuwa na wazao

watakaoendeleza jina lako.

Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha

ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu.

Nitaandaa kaburi lako,

kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”

151:15 Isa 40:9; Rum 10:15; Isa 52:7; Mdo 10:36; Law 23:2-4Tazama, huko juu milimani,

miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema,

ambaye anatangaza amani!

Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako,

nawe utimize nadhiri zako.

Waovu hawatakuvamia tena;

wataangamizwa kabisa.

New International Version – UK

Nahum 1:1-15

1A prophecy concerning Nineveh. The book of the vision of Nahum the Elkoshite.

The Lord’s anger against Nineveh

2The Lord is a jealous and avenging God;

the Lord takes vengeance and is filled with wrath.

The Lord takes vengeance on his foes

and vents his wrath against his enemies.

3The Lord is slow to anger but great in power;

the Lord will not leave the guilty unpunished.

His way is in the whirlwind and the storm,

and clouds are the dust of his feet.

4He rebukes the sea and dries it up;

he makes all the rivers run dry.

Bashan and Carmel wither

and the blossoms of Lebanon fade.

5The mountains quake before him

and the hills melt away.

The earth trembles at his presence,

the world and all who live in it.

6Who can withstand his indignation?

Who can endure his fierce anger?

His wrath is poured out like fire;

the rocks are shattered before him.

7The Lord is good,

a refuge in times of trouble.

He cares for those who trust in him,

8but with an overwhelming flood

he will make an end of Nineveh;

he will pursue his foes into the realm of darkness.

9Whatever they plot against the Lord

he will bring1:9 Or What do you foes plot against the Lord? / He will bring it to an end;

trouble will not come a second time.

10They will be entangled among thorns

and drunk from their wine;

they will be consumed like dry stubble.1:10 The meaning of the Hebrew for this verse is uncertain.

11From you, Nineveh, has one come forth

who plots evil against the Lord

and devises wicked plans.

12This is what the Lord says:

‘Although they have allies and are numerous,

they will be destroyed and pass away.

Although I have afflicted you, Judah,

I will afflict you no more.

13Now I will break their yoke from your neck

and tear your shackles away.’

14The Lord has given a command concerning you, Nineveh:

‘You will have no descendants to bear your name.

I will destroy the images and idols

that are in the temple of your gods.

I will prepare your grave,

for you are vile.’

15Look, there on the mountains,

the feet of one who brings good news,

who proclaims peace!

Celebrate your festivals, Judah,

and fulfil your vows.

No more will the wicked invade you;

they will be completely destroyed.1:15 In Hebrew texts this verse (1:15) is numbered 2:1.