Nahumu 1 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nahumu 1:1-15

11:1 Isa 13:1; 19:1; Yer 23:33-34; 50:18; Mwa 10:11; Nah 2:8; 3:7Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.

Hasira Ya Mungu Dhidi Ya Ninawi

21:2 Kut 20:5; Mwa 4:24; Kum 32:41; 7:10; Za 94:1Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi;

Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu.

Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake,

naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.

31:3 Neh 9:17; Kut 34:7; 19:16; Za 103:8; Mik 7:18; 2Sam 22:10; Za 50:3; 104:3Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu,

Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia.

Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani,

na mawingu ni vumbi la miguu yake.

41:4 2Sam 22:16; Kut 14:22; Isa 33:9; Yos 3:15, 16Anakemea bahari na kuikausha,

anafanya mito yote kukauka.

Bashani na Karmeli zinanyauka

na maua ya Lebanoni hukauka.

51:5 Kut 19:18; Ay 9:6; 2Sam 22:8; Yoe 2:10; Eze 38:20; Mik 1:4Milima hutikisika mbele yake

na vilima huyeyuka.

Nchi hutetemeka mbele yake,

dunia na wote waishio ndani yake.

61:6 Za 130:3; Eze 22:14; Isa 5:24-25; 42:25; Yer 10:10; 1Fal 19:11Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu?

Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali?

Ghadhabu yake imemiminwa kama moto,

na miamba inapasuka mbele zake.

71:7 Yer 33:11; 17:17; Za 22:9; 1:6; 2Tim 2:19Bwana ni Mwema,

kimbilio wakati wa taabu.

Huwatunza wale wanaomtegemea,

81:8 Isa 8:7; Amo 8:8; Dan 9:26lakini kwa mafuriko makubwa,

ataangamiza Ninawi;

atafuatilia adui zake hadi gizani.

91:9 Hos 7:15Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana

yeye atalikomesha;

taabu haitatokea mara ya pili.

101:10 2Sam 23:6; Isa 49:26; 5:24; Mal 4:1Watasongwa katikati ya miiba

na kulewa kwa mvinyo wao.

Watateketezwa kama mabua makavu.

11Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja,

ambaye anapanga shauri baya

dhidi ya Bwana

na kushauri uovu.

121:12 Isa 10:34; 54:6-8; Mao 3:31-32Hili ndilo asemalo Bwana:

“Ingawa wana muungano nao ni wengi sana,

watakatiliwa mbali na kuangamia.

Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda,

sitakutesa tena.

131:13 Isa 9:4; Ay 12:18; Za 107:14Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako,

nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”

141:14 Isa 14:22; Mik 5:13; Yer 28:8; Eze 32:22-23Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi:

“Hutakuwa na wazao

watakaoendeleza jina lako.

Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha

ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu.

Nitaandaa kaburi lako,

kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”

151:15 Isa 40:9; Rum 10:15; Isa 52:7; Mdo 10:36; Law 23:2-4Tazama, huko juu milimani,

miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema,

ambaye anatangaza amani!

Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako,

nawe utimize nadhiri zako.

Waovu hawatakuvamia tena;

wataangamizwa kabisa.

New International Reader’s Version

Nahum 1:1-15

1Here is a prophecy the Lord gave Nahum, who was from the town of Elkosh. The prophecy came in a vision and is written in a book. The prophecy is about Nineveh.

The Lord Is Angry With Nineveh

2The Lord is a jealous God who punishes people.

He pays them back for the evil things they do.

He directs his anger against them.

The Lord punishes his enemies.

He holds his anger back

until the right time to use it.

3The Lord is slow to get angry.

But he is very powerful.

The Lord will not let guilty people go

without punishing them.

When he marches out, he stirs up winds and storms.

Clouds are the dust kicked up by his feet.

4He controls the seas. He dries them up.

He makes all the rivers run dry.

Bashan and Mount Carmel dry up.

The flowers in Lebanon fade.

5He causes the mountains to shake.

The hills melt away.

The earth trembles because he is there.

The world and all those who live in it also tremble.

6Who can stand firm when his anger burns?

Who can live when he is angry?

His anger blazes out like fire.

He smashes the rocks to pieces.

7The Lord is good.

When people are in trouble,

they can go to him for safety.

He takes good care of those

who trust in him.

8But he will destroy Nineveh

with a powerful flood.

He will chase his enemies

into the place of darkness.

9The Lord will put an end

to anything they plan against him.

He won’t allow Assyria to win the battle

over his people a second time.

10His enemies will be tangled up among thorns.

Their wine will make them drunk.

They’ll be burned up like dry straw.

11Nineveh, a king has marched out from you.

He makes evil plans against the Lord.

He thinks about how he can do what is wrong.

12The Lord says,

“His army has many soldiers.

Other nations are helping them.

But they will be destroyed and pass away.

Judah, I punished you.

But I will not do it anymore.

13Now I will break Assyria’s yoke off your neck.

I will tear off the ropes that hold you.”

14Nineveh, the Lord has given an order concerning you.

He has said, “You will not have any children

to carry on your name.

I will destroy the wooden and metal statues

that are in the temple of your gods.

I will get your grave ready for you.

You are worthless.”

15Look at the mountains of Judah!

I see a messenger running to bring good news!

He’s telling us that peace has come!

People of Judah, celebrate your feasts.

Carry out your promises.

The evil Assyrians won’t attack you again.

They’ll be completely destroyed.