Nahumu 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nahumu 1:1-15

11:1 Isa 13:1; 19:1; Yer 23:33-34; 50:18; Mwa 10:11; Nah 2:8; 3:7Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.

Hasira Ya Mungu Dhidi Ya Ninawi

21:2 Kut 20:5; Mwa 4:24; Kum 32:41; 7:10; Za 94:1Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi;

Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu.

Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake,

naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.

31:3 Neh 9:17; Kut 34:7; 19:16; Za 103:8; Mik 7:18; 2Sam 22:10; Za 50:3; 104:3Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu,

Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia.

Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani,

na mawingu ni vumbi la miguu yake.

41:4 2Sam 22:16; Kut 14:22; Isa 33:9; Yos 3:15, 16Anakemea bahari na kuikausha,

anafanya mito yote kukauka.

Bashani na Karmeli zinanyauka

na maua ya Lebanoni hukauka.

51:5 Kut 19:18; Ay 9:6; 2Sam 22:8; Yoe 2:10; Eze 38:20; Mik 1:4Milima hutikisika mbele yake

na vilima huyeyuka.

Nchi hutetemeka mbele yake,

dunia na wote waishio ndani yake.

61:6 Za 130:3; Eze 22:14; Isa 5:24-25; 42:25; Yer 10:10; 1Fal 19:11Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu?

Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali?

Ghadhabu yake imemiminwa kama moto,

na miamba inapasuka mbele zake.

71:7 Yer 33:11; 17:17; Za 22:9; 1:6; 2Tim 2:19Bwana ni Mwema,

kimbilio wakati wa taabu.

Huwatunza wale wanaomtegemea,

81:8 Isa 8:7; Amo 8:8; Dan 9:26lakini kwa mafuriko makubwa,

ataangamiza Ninawi;

atafuatilia adui zake hadi gizani.

91:9 Hos 7:15Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana

yeye atalikomesha;

taabu haitatokea mara ya pili.

101:10 2Sam 23:6; Isa 49:26; 5:24; Mal 4:1Watasongwa katikati ya miiba

na kulewa kwa mvinyo wao.

Watateketezwa kama mabua makavu.

11Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja,

ambaye anapanga shauri baya

dhidi ya Bwana

na kushauri uovu.

121:12 Isa 10:34; 54:6-8; Mao 3:31-32Hili ndilo asemalo Bwana:

“Ingawa wana muungano nao ni wengi sana,

watakatiliwa mbali na kuangamia.

Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda,

sitakutesa tena.

131:13 Isa 9:4; Ay 12:18; Za 107:14Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako,

nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”

141:14 Isa 14:22; Mik 5:13; Yer 28:8; Eze 32:22-23Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi:

“Hutakuwa na wazao

watakaoendeleza jina lako.

Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha

ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu.

Nitaandaa kaburi lako,

kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”

151:15 Isa 40:9; Rum 10:15; Isa 52:7; Mdo 10:36; Law 23:2-4Tazama, huko juu milimani,

miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema,

ambaye anatangaza amani!

Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako,

nawe utimize nadhiri zako.

Waovu hawatakuvamia tena;

wataangamizwa kabisa.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

那鴻書 1:1-15

1以下是關於尼尼微的預言,是伊勒歌斯那鴻的啟示書。

耶和華向尼尼微發怒

2耶和華是痛恨不貞、施行報應的上帝。

耶和華施行報應,充滿烈怒。

耶和華報應祂的仇敵,向他們發烈怒。

3耶和華不輕易發怒,有偉大的能力。

耶和華斷不以有罪的為無罪。

祂行走在旋風和暴風中,

雲彩是祂腳下的塵土。

4祂斥責大海,使大海乾涸;

祂使一切河流枯竭。

巴珊迦密的草木凋零,

黎巴嫩的鮮花衰殘。

5在祂面前,群山震動,丘陵消融。

在祂面前,大地隆起,

世界和世上的一切都戰慄。

6祂發怒,誰能站立?

祂發烈怒,誰能承受?

祂的憤怒如火焰噴湧而出,

磐石在祂面前崩裂。

7耶和華是良善的,

是人患難時的避難所;

祂看顧那些信靠祂的人。

8祂必用滔滔洪水滅絕祂的敵人,

把他們驅逐到黑暗中。

9尼尼微人啊,

你們為何圖謀抵擋耶和華?

祂要徹底毀滅你們,

無需擊打兩次。

10你們像糾結的荊棘,

又像酩酊大醉的人,

要如乾稭被火燒盡。

11你們當中有一個人,

一個邪惡的陰謀者,

圖謀抵擋耶和華。

12耶和華說:

「儘管尼尼微勢力強大、人口眾多,

但必被剷除,化為烏有。

我的子民啊,我使你們受了苦,

但必不再使你們受苦。

13現在我要打碎他們套在你們頸項上的軛,

鬆開你們身上的鎖鏈。」

14尼尼微啊,

耶和華已發出有關你的命令:

「你的名不會傳於後世。

我要摧毀你神廟中雕刻和鑄造的偶像。

我要為你掘好墳墓,

因為你毫無用處。」

15看啊,

傳喜訊、報平安的人穿山越嶺而來。

猶大啊,

慶祝你的節期,

還你許的願吧!

邪惡之人將不再侵擾你,

他們都將被徹底毀滅。