Mwanzo 9 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 9:1-29

Mungu Aweka Agano Na Noa

19:1 Mwa 1:22Ndipo Mungu akambariki Noa na wanawe, akiwaambia, “Zaeni mkaongezeke kwa idadi na mkaijaze tena dunia. 29:2 Mwa 1:26Wanyama wote wa duniani, ndege wote wa angani, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi, na samaki wote wa baharini wamekabidhiwa mikononi mwenu, nao watawaogopa na kuwahofu. 39:3 Mwa 1:29; Kol 2:16; Mdo 10:15Kila kitu chenye uhai kiendacho kitakuwa chakula chenu. Kama vile nilivyowapa mimea mbalimbali, sasa nawapa kila kitu.

49:4 Law 3:17; 7:26; 17:10-14; 19:26; Kum 12:16, 23-25; 15:23; 1Sam 14:33; Eze 33:25; Mdo 15:20, 29“Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu ya uhai wake, kwa maana damu ni uhai. 59:5 Mwa 4:10; 42:22; 50:15; 1Fal 2:32; 2Nya 24:22; Za 9:12; Kut 21:28-32Hakika damu ya uhai wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila mnyama. Kutoka kwa kila mwanadamu pia nitaidai kwa ajili ya uhai wa mtu mwenzake.

69:6 Mwa 1:26; 4:14; Amu 9:24; Mt 26:52“Yeyote amwagaye damu ya mwanadamu,

damu yake itamwagwa na mwanadamu,

kwa kuwa katika mfano wa Mungu,

Mungu alimuumba mwanadamu.

79:7 Mwa 1:22; 9:19Kuhusu ninyi, zaeni mwongezeke kwa wingi, mzidi katika dunia na kuijaza.”

8Ndipo Mungu akamwambia Noa na wanawe pamoja naye: 99:9 Mwa 6:18“Sasa mimi ninaweka Agano langu nanyi, pamoja na uzao wenu baada yenu, 10pia na kila kiumbe hai kilichokuwa pamoja nanyi: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wote wa porini, wale wote waliotoka katika safina pamoja nanyi, kila kiumbe hai duniani. 119:11 Isa 24:5; 33:8; 54:9; Hos 6:7; Mwa 8:21Ninaweka Agano nanyi: Kamwe uhai hautafutwa tena kwa gharika, kamwe haitakuwepo tena gharika ya kuangamiza dunia.”

129:12 Mwa 17:11-12; Kut 12:14; Law 3:17; 6:18; 17:7; Hes 10:8Mungu akasema, “Hii ni ishara ya Agano ninalofanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, Agano kwa vizazi vyote vijavyo: 139:13 Eze 1:28; Ufu 4:3; 10:1Nimeweka upinde wangu wa mvua mawinguni, nao utakuwa ishara ya Agano nifanyalo kati yangu na dunia. 14Wakati wowote ninapotanda mawingu juu ya dunia na upinde wa mvua ukijitokeza mawinguni, 159:15 Mwa 8:1, 21; Kut 2:24; 6:5; 34:10; Law 26:42-45; Kum 7:9; Za 89:34; 103:18; 105:8; 106:45; Eze 16:60nitakumbuka Agano langu kati yangu na ninyi na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina. Kamwe maji hayatakuwa tena gharika ya kuangamiza uhai wote. 169:16 Mwa 17:7-13, 19; 2Sam 7:13; 23:5; Za 105:9-10; Isa 9:7; 54:10; 55:3; 59:21; 61:8; Yer 31:34; 32:40; 33:21; Eze 16:60; 37:26; Ebr 13:20Wakati wowote upinde wa mvua unapotokea mawinguni, nitauona na kukumbuka Agano la milele kati ya Mungu na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina duniani.”

17Hivyo Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya Agano ambalo nimelifanya kati yangu na viumbe vyote vilivyo hai duniani.”

Wana Wa Noa

189:18 Mwa 5:32; 10:6, 15; Lk 3:36Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.) 199:19 Mwa 5:32; 1:22; 10:32; 11:4-9Hawa ndio waliokuwa wana watatu wa Noa, kutokana nao watu walienea katika dunia.

20Noa akawa mkulima, akawa mtu wa kwanza kupanda mizabibu. 219:21 Mwa 19:35Alipokunywa huo mvinyo wake akalewa na akalala uchi kwenye hema lake. 229:22 Hab 2:15Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake na kuwaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. 23Lakini Shemu na Yafethi wakachukua nguo wakaitanda mabegani mwao wote wawili, kisha wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zilielekea upande mwingine ili wasiuone uchi wa baba yao.

24Noa alipolevuka kutoka kwenye mvinyo wake na kujua lile ambalo mwanawe mdogo kuliko wote alilokuwa amemtendea, 259:25 Mwa 27:12, 29-40; 25:23; 37:10; 49:8; Kut 20:5; Za 79:8; Isa 14:21; Yer 31:29; 32:18; Hes 24:18; Yos 9:23akasema,

“Alaaniwe Kanaani!

Atakuwa mtumwa wa chini sana

kuliko watumwa wote kwa ndugu zake.”

269:26 Mwa 14:20; Kut 18:10; Za 7:17; 1Fal 9:21Pia akasema,

“Abarikiwe Bwana, Mungu wa Shemu!

Kanaani na awe mtumwa wa Shemu.

279:27 Mwa 10:2-5; Efe 2:13-14; 3:6Mungu na apanue mipaka ya Yafethi;

Yafethi na aishi katika mahema ya Shemu,

na Kanaani na awe mtumwa wake.”

28Baada ya gharika Noa aliishi miaka 350. 299:29 Mwa 2:17Noa alikuwa na jumla ya miaka 950, ndipo akafa.

New International Version – UK

Genesis 9:1-29

God’s covenant with Noah

1Then God blessed Noah and his sons, saying to them, ‘Be fruitful and increase in number and fill the earth. 2The fear and dread of you will fall on all the beasts of the earth, and on all the birds in the sky, on every creature that moves along the ground, and on all the fish in the sea; they are given into your hands. 3Everything that lives and moves about will be food for you. Just as I gave you the green plants, I now give you everything.

4‘But you must not eat meat that has its lifeblood still in it. 5And for your lifeblood I will surely demand an accounting. I will demand an accounting from every animal. And from each human being, too, I will demand an accounting for the life of another human being.

6‘Whoever sheds human blood,

by humans shall their blood be shed;

for in the image of God

has God made mankind.

7As for you, be fruitful and increase in number; multiply on the earth and increase upon it.’

8Then God said to Noah and to his sons with him: 9‘I now establish my covenant with you and with your descendants after you 10and with every living creature that was with you – the birds, the livestock and all the wild animals, all those that came out of the ark with you – every living creature on earth. 11I establish my covenant with you: never again will all life be destroyed by the waters of a flood; never again will there be a flood to destroy the earth.’

12And God said, ‘This is the sign of the covenant I am making between me and you and every living creature with you, a covenant for all generations to come: 13I have set my rainbow in the clouds, and it will be the sign of the covenant between me and the earth. 14Whenever I bring clouds over the earth and the rainbow appears in the clouds, 15I will remember my covenant between me and you and all living creatures of every kind. Never again will the waters become a flood to destroy all life. 16Whenever the rainbow appears in the clouds, I will see it and remember the everlasting covenant between God and all living creatures of every kind on the earth.’

17So God said to Noah, ‘This is the sign of the covenant I have established between me and all life on the earth.’

The sons of Noah

18The sons of Noah who came out of the ark were Shem, Ham and Japheth. (Ham was the father of Canaan.) 19These were the three sons of Noah, and from them came the people who were scattered over the whole earth.

20Noah, a man of the soil, proceeded9:20 Or soil, was the first to plant a vineyard. 21When he drank some of its wine, he became drunk and lay uncovered inside his tent. 22Ham, the father of Canaan, saw his father naked and told his two brothers outside. 23But Shem and Japheth took a garment and laid it across their shoulders; then they walked in backwards and covered their father’s naked body. Their faces were turned the other way so that they would not see their father naked.

24When Noah awoke from his wine and found out what his youngest son had done to him, 25he said,

‘Cursed be Canaan!

The lowest of slaves

will he be to his brothers.’

26He also said,

‘Praise be to the Lord, the God of Shem!

May Canaan be the slave of Shem.

27May God extend Japheth’s9:27 Japheth sounds like the Hebrew for extend. territory;

may Japheth live in the tents of Shem,

and may Canaan be the slave of Japheth.’

28After the flood Noah lived 350 years. 29Noah lived a total of 950 years, and then he died.