Mwanzo 49 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 49:1-33

Yakobo Abariki Wanawe

149:1 Hes 24:14; Kum 31:29Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.

249:2 Yos 24:1; Za 34:11“Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo,

msikilizeni baba yenu Israeli.

349:3 Mwa 29:32; Kum 21:17; Za 78:51“Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza,

nguvu zangu, tunda la kwanza la nguvu zangu,

umepita kwa heshima, umepita kwa uwezo.

4Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena,

kwa kuwa ulipanda kwenye kitanda cha baba yako,

kwenye kitanda changu na kukinajisi.

549:5 Mwa 29:33; Mit 4:17“Simeoni na Lawi ni wana ndugu:

panga zao ni silaha za jeuri.

649:6 Mit 1:15; Efe 5:11Mimi na nisiingie katika baraza lao,

nami nisiunganike katika kusanyiko lao,

kwa kuwa wamewaua watu katika hasira yao,

walikata mishipa ya miguu ya mafahali

kama walivyopenda.

749:7 Yos 19:1, 9; Mwa 29:35Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno,

nayo ghadhabu yao ni ya ukatili!

Nitawatawanya katika Yakobo

Na kuwasambaza katika Israeli.

849:8 1Nya 5:2; Kum 28:48“Yuda, ndugu zako watakusifu;

mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako;

wana wa baba yako watakusujudia.

949:9 Hes 24:9; Ay 38:39Ee Yuda, wewe ni mwana simba;

unarudi toka mawindoni, mwanangu.

Kama simba hunyemelea na kulala chini,

kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?

1049:10 Eze 21:27; Isa 42:1Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda,

wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake,

hadi aje yeye ambaye milki ni yake,

ambaye utii wa mataifa ni wake.

11Atamfunga punda wake katika mzabibu,

naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi;

atafua mavazi yake katika divai,

majoho yake katika damu ya mizabibu.

12Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai,

meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.

1349:13 Mwa 30:20; 10:19“Zabuloni ataishi pwani ya bahari

na kuwa bandari za kuegesha meli;

mpaka wake utapanuka kuelekea Sidoni.

14“Isakari ni punda mwenye nguvu

ambaye amelala kati ya mizigo yake.

1549:15 Yos 19:17-23; Eze 29:18Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika

na jinsi nchi yake inavyopendeza,

atainamisha bega lake kwenye mzigo

na kujitolea kwa ajili ya kazi ngumu.

16“Dani atahukumu watu wake kwa haki

kama mmoja wa makabila ya Israeli.

1749:17 Amu 18:27; Yer 8:17Dani atakuwa nyoka kando ya barabara,

nyoka mwenye sumu kando ya njia,

yule aumaye visigino vya farasi

ili yule ampandaye aanguke chali.

18“Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.

19“Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji,

lakini yeye atawageukia na kuwashinda kabisa.

2049:20 Mwa 30:13; Isa 25:6; Ay 29:6“Chakula cha Asheri kitakuwa kinono,

naye atatoa chakula kitamu kimfaacho mfalme.

21“Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru

azaaye watoto wazuri.

2249:22 Mwa 30:24; Eze 19:10“Yosefu ni mzabibu uzaao,

mzabibu uzaao ulio kando ya chemchemi,

ambao matawi yake hutanda ukutani.

23Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia,

wakampiga mshale kwa ukatili.

2449:24 Za 18:34; Isa 1:24Lakini upinde wake ulibaki imara,

mikono yake ikatiwa nguvu,

na mkono wa Mwenye Nguvu wa Yakobo,

kwa sababu ya Mchungaji, Mwamba wa Israeli,

2549:25 Kut 18:4; Mwa 27:28kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia,

kwa sababu ya Mwenyezi,49:25 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania. yeye anayekubariki

kwa baraka za mbinguni juu,

baraka za kilindi kilichoko chini,

baraka za matitini na za tumbo la uzazi.

26Baraka za baba yako ni kubwa

kuliko baraka za milima ya kale,

nyingi kuliko vilima vya kale.

Baraka hizo zote na zikae juu ya kichwa cha Yosefu,

juu ya paji la yule mkuu miongoni mwa ndugu zake.

2749:27 Amu 20:12-13; Ebr 1:8; Hes 31:11“Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu;

asubuhi hurarua mawindo yake,

jioni hugawa nyara.”

28Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.

Kifo Cha Yakobo

2949:29 Mwa 25:8; 2Sam 2:32Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti, 30pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba. 3149:31 Mwa 25:9; 23:19Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea. 32Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”

3349:33 Mwa 25:8; Mdo 7:15Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.

Persian Contemporary Bible

پيدايش 49:1-33

آخرين سخنان يعقوب

1آنگاه يعقوب همهٔ پسرانش را نزد خود فرا خواند و به ايشان گفت: «دور من جمع شويد تا به شما بگويم كه در آينده بر شما چه خواهد گذشت. 2ای پسران يعقوب به سخنان پدر خود اسرائيل گوش دهيد.

3«رئوبين، تو پسر ارشد من و فرزند اوايل جوانی من هستی. تو از لحاظ مقام و قدرت از همه برتر می‌باشی، 4ولی چون امواج سركش دريا، خروشانی. پس از اين ديگر برتر از همه نخواهی بود، زيرا با يكی از زنان من نزديكی نموده، مرا بی‌حرمت كردی.

5«شمعون و لاوی، شما مثل هم هستيد، مردانی بی‌رحم و بی‌انصاف. 6من هرگز در نقشه‌های پليد شما شريک نخواهم شد، زيرا از روی خشم خود انسانها را كُشتيد و خودسرانه رگ پاهای گاوان را قطع كرديد. 7لعنت بر خشم شما كه اينچنين شديد و بی‌رحم بود. من نسل شما را در سراسر سرزمين اسرائيل پراكنده خواهم ساخت.

8«ای يهودا، برادرانت تو را ستايش خواهند كرد. تو دشمنانت را منهدم خواهی نمود. 9يهودا مانند شير بچه‌ای است كه از شكار برگشته و خوابيده است. كيست كه جرأت كند او را بيدار سازد؟ 10عصای سلطنت از يهودا دور نخواهد شد تا شيلو كه همهٔ قومها او را اطاعت می‌كنند، بيايد. 11الاغ خود را به بهترين درخت انگور خواهد بست و جامهٔ خود را در شراب خواهد شست. 12چشمان او تيره‌تر از شراب و دندانهايش سفيدتر از شير خواهد بود.

13«زبولون در سواحل دريا ساكن خواهد شد و بندری برای كشتيها خواهد بود و مرزهايش تا صيدون گسترش خواهد يافت.

14«يساكار حيوان باركش نيرومندی است كه زير بار خود خوابيده است. 15وقتی ببيند جايی كه خوابيده دلپسند است، تن به كار خواهد داد و چون برده‌ای به بيگاری كشيده خواهد شد.

16«دان قبيلهٔ خود را چون يكی از قبايل اسرائيل داوری خواهد كرد. 17او مثل مار بر سر راه قرار گرفته، پاشنه اسبان را نيش خواهد زد تا سوارانشان سرنگون شوند. 18خداوندا، منتظر نجات تو می‌باشم.

19«جاد مورد حملهٔ غارتگران واقع خواهد شد، اما او بر آنها هجوم خواهد آورد.

20«اشير سرزمينی حاصلخيز خواهد داشت و از محصول آن برای پادشاهان خوراک تهيه خواهد كرد.

21«نفتالی غزالی است آزاد كه بچه‌های زيبا به وجود می‌آورد.

22«يوسف درخت پرثمريست در كنار چشمهٔ آب كه شاخه‌هايش به اطراف سايه افكنده است. 23دشمنان بر او هجوم آوردند و با تيرهای خود به او صدمه زدند. 24ولی خدای قادر يعقوب يعنی شبان و پناهگاه اسرائيل بازو و كمان آنها را شكسته است. 25باشد كه خدای قادر مطلق، خدای پدرت، تو را ياری كند و از بركات آسمانی و زمينی بهره‌مند گرداند و فرزندان تو را زياد سازد. 26بركت پدر تو عظيم‌تر از وفور محصولات کوههای قديمی است. تمام اين بركات بر يوسف كه از ميان برادرانش برگزيده شد، قرار گيرد.

27«بنيامين گرگ درنده‌ای است كه صبحگاهان دشمنانش را می‌بلعد و شامگاهان آنچه را كه به غنيمت گرفته است، تقسيم می‌نمايد.»

28اين بود بركات يعقوب به پسران خود كه دوازده قبيلهٔ اسرائيل را به وجود آوردند.

مرگ يعقوب

29‏-30سپس يعقوب چنين وصيت كرد: «من بزودی می‌ميرم و به اجداد خود می‌پيوندم. شما جسد مرا به كنعان برده، در كنار پدرانم در غار مكفيله كه مقابل ممری است دفن كنيد. ابراهيم آن را با مزرعه‌اش از عفرون حيتّی خريداری نمود تا مقبره خانوادگی‌اش باشد. 31در آنجا ابراهيم و همسرش ساره، اسحاق و همسر وی ربكا دفن شده‌اند. ليه را هم در آنجا به خاک سپردم. 32پدربزرگم ابراهيم آن غار و مزرعه‌اش را برای همين منظور از حيتّی‌ها خريد.»

33پس از آنکه يعقوب اين وصيت را با پسرانش به پايان رساند، بر بستر خود دراز كشيده، جان سپرد و به اجداد خود پيوست.