Mwanzo 49 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 49:1-33

Yakobo Abariki Wanawe

149:1 Hes 24:14; Kum 31:29Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.

249:2 Yos 24:1; Za 34:11“Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo,

msikilizeni baba yenu Israeli.

349:3 Mwa 29:32; Kum 21:17; Za 78:51“Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza,

nguvu zangu, tunda la kwanza la nguvu zangu,

umepita kwa heshima, umepita kwa uwezo.

4Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena,

kwa kuwa ulipanda kwenye kitanda cha baba yako,

kwenye kitanda changu na kukinajisi.

549:5 Mwa 29:33; Mit 4:17“Simeoni na Lawi ni wana ndugu:

panga zao ni silaha za jeuri.

649:6 Mit 1:15; Efe 5:11Mimi na nisiingie katika baraza lao,

nami nisiunganike katika kusanyiko lao,

kwa kuwa wamewaua watu katika hasira yao,

walikata mishipa ya miguu ya mafahali

kama walivyopenda.

749:7 Yos 19:1, 9; Mwa 29:35Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno,

nayo ghadhabu yao ni ya ukatili!

Nitawatawanya katika Yakobo

Na kuwasambaza katika Israeli.

849:8 1Nya 5:2; Kum 28:48“Yuda, ndugu zako watakusifu;

mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako;

wana wa baba yako watakusujudia.

949:9 Hes 24:9; Ay 38:39Ee Yuda, wewe ni mwana simba;

unarudi toka mawindoni, mwanangu.

Kama simba hunyemelea na kulala chini,

kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?

1049:10 Eze 21:27; Isa 42:1Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda,

wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake,

hadi aje yeye ambaye milki ni yake,

ambaye utii wa mataifa ni wake.

11Atamfunga punda wake katika mzabibu,

naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi;

atafua mavazi yake katika divai,

majoho yake katika damu ya mizabibu.

12Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai,

meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.

1349:13 Mwa 30:20; 10:19“Zabuloni ataishi pwani ya bahari

na kuwa bandari za kuegesha meli;

mpaka wake utapanuka kuelekea Sidoni.

14“Isakari ni punda mwenye nguvu

ambaye amelala kati ya mizigo yake.

1549:15 Yos 19:17-23; Eze 29:18Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika

na jinsi nchi yake inavyopendeza,

atainamisha bega lake kwenye mzigo

na kujitolea kwa ajili ya kazi ngumu.

16“Dani atahukumu watu wake kwa haki

kama mmoja wa makabila ya Israeli.

1749:17 Amu 18:27; Yer 8:17Dani atakuwa nyoka kando ya barabara,

nyoka mwenye sumu kando ya njia,

yule aumaye visigino vya farasi

ili yule ampandaye aanguke chali.

18“Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.

19“Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji,

lakini yeye atawageukia na kuwashinda kabisa.

2049:20 Mwa 30:13; Isa 25:6; Ay 29:6“Chakula cha Asheri kitakuwa kinono,

naye atatoa chakula kitamu kimfaacho mfalme.

21“Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru

azaaye watoto wazuri.

2249:22 Mwa 30:24; Eze 19:10“Yosefu ni mzabibu uzaao,

mzabibu uzaao ulio kando ya chemchemi,

ambao matawi yake hutanda ukutani.

23Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia,

wakampiga mshale kwa ukatili.

2449:24 Za 18:34; Isa 1:24Lakini upinde wake ulibaki imara,

mikono yake ikatiwa nguvu,

na mkono wa Mwenye Nguvu wa Yakobo,

kwa sababu ya Mchungaji, Mwamba wa Israeli,

2549:25 Kut 18:4; Mwa 27:28kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia,

kwa sababu ya Mwenyezi,49:25 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania. yeye anayekubariki

kwa baraka za mbinguni juu,

baraka za kilindi kilichoko chini,

baraka za matitini na za tumbo la uzazi.

26Baraka za baba yako ni kubwa

kuliko baraka za milima ya kale,

nyingi kuliko vilima vya kale.

Baraka hizo zote na zikae juu ya kichwa cha Yosefu,

juu ya paji la yule mkuu miongoni mwa ndugu zake.

2749:27 Amu 20:12-13; Ebr 1:8; Hes 31:11“Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu;

asubuhi hurarua mawindo yake,

jioni hugawa nyara.”

28Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.

Kifo Cha Yakobo

2949:29 Mwa 25:8; 2Sam 2:32Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti, 30pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba. 3149:31 Mwa 25:9; 23:19Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea. 32Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”

3349:33 Mwa 25:8; Mdo 7:15Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Génesis 49:1-33

Jacob bendice a sus hijos

1Jacob llamó a sus hijos y les dijo: «Reuníos, que voy a declararos lo que os va a suceder en el futuro:

2»Hijos de Jacob: acercaos y escuchad;

prestad atención a vuestro padre Israel.

3»Tú, Rubén, eres mi primogénito,

primer fruto de mi fuerza y virilidad,

primero en honor y en poder.

4Impetuoso como un torrente,

ya no serás el primero:

te acostaste en mi cama;

profanaste la cama de tu propio padre.

5»Simeón y Leví son chacales;49:5 chacales (lectura probable); hermanos (TM).

sus espadas49:5 espadas. Palabra de difícil traducción. son instrumentos de violencia.

6¡No quiero participar de sus reuniones,

ni arriesgar mi honor en sus asambleas!

En su furor mataron hombres,

y por capricho mutilaron toros.

7¡Malditas sean la violencia de su enojo

y la crueldad de su furor!

Los dispersaré en el país de Jacob,

los desparramaré en la tierra de Israel.

8»Tú, Judá, serás alabado49:8 En hebreo, Judá suena como el verbo que significa alabar. por tus hermanos;

dominarás a tus enemigos,

y tus propios hermanos se inclinarán ante ti.

9Mi hijo Judá es como un cachorro de león

que se ha nutrido de la presa.

Se tiende al acecho como león,

como leona que nadie se atreve a molestar.

10El cetro no se apartará de Judá,

ni de entre sus pies el bastón de mando,

hasta que llegue el verdadero rey,49:10 el verdadero rey. Alt. Siló. Texto de difícil traducción.

quien merece la obediencia de los pueblos.

11Judá amarra su asno a la vid,

y la cría de su asno a la mejor cepa;

lava su ropa en vino;

su manto, en la sangre de las uvas.

12Sus ojos son más oscuros que el vino;

sus dientes, más blancos que la leche.49:12 Sus ojos … la leche. Alt. Sus ojos están oscurecidos por el vino; sus dientes, blanqueados por la leche.

13»Zabulón vivirá a la orilla del mar;

será puerto seguro para las naves,

y sus fronteras llegarán hasta Sidón.

14»Isacar es un asno fuerte

echado entre dos alforjas.

15Al ver que el establo era bueno

y que la tierra era agradable,

agachó el hombro para llevar la carga

y se sometió a la esclavitud.

16»Dan hará justicia en su pueblo,

como una de las tribus de Israel.

17Dan es una serpiente junto al camino,

una víbora junto al sendero,

que muerde los talones del caballo

y hace caer de espaldas al jinete.

18»¡Señor, espero tu salvación!

19»Las hordas atacan a Gad,

pero él las atacará por la espalda.

20»Aser disfrutará de comidas deliciosas;

ofrecerá manjares de reyes.

21»Neftalí es una gacela libre,

que tiene hermosos cervatillos.49:21 que … cervatillos. Alt. que pronuncia hermosas palabras.

22»José es un retoño fértil,

fértil retoño junto al agua,

cuyas ramas trepan por el muro.

23Los arqueros lo atacaron sin piedad;

le tiraron flechas, lo hostigaron.

24Pero su arco se mantuvo firme,

porque sus brazos son fuertes.

¡Gracias al Dios fuerte de Jacob,

al Pastor y Roca de Israel!

25¡Gracias al Dios de tu padre, que te ayuda!

¡Gracias al Todopoderoso, que te bendice!

¡Con bendiciones de lo alto!

¡Con bendiciones del abismo!

¡Con bendiciones de los pechos y del seno materno!

26Son mejores las bendiciones de tu padre

que las de los montes de antaño,

que la abundancia de las colinas eternas.

¡Que descansen estas bendiciones

sobre la cabeza de José,

sobre la frente del escogido entre sus hermanos!

27»Benjamín es un lobo rapaz

que en la mañana devora la presa

y en la tarde reparte los despojos».

28Estas son las doce tribus de Israel, y esto es lo que su padre les dijo cuando impartió a cada una de ellas su bendición.

Muerte de Jacob

29Además, Jacob les dio estas instrucciones: «Ya estoy a punto de reunirme con los míos. Enterradme junto a mis antepasados, en la cueva que está en el campo de Efrón el hitita. 30Se trata de la cueva de Macpela, frente a Mamré, en la tierra de Canaán. Está en el campo que Abraham le compró a Efrón el hitita, para que fuera el sepulcro de la familia. 31Allí fueron sepultados Abraham y su esposa Sara, Isaac y su esposa Rebeca, y allí también enterré a Lea. 32Ese campo y su cueva se les compró a los hititas».

33Cuando Jacob terminó de dar estas instrucciones a sus hijos, volvió a acostarse, exhaló el último suspiro, y fue a reunirse con sus antepasados.