Mwanzo 49 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 49:1-33

Yakobo Abariki Wanawe

149:1 Hes 24:14; Kum 31:29Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.

249:2 Yos 24:1; Za 34:11“Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo,

msikilizeni baba yenu Israeli.

349:3 Mwa 29:32; Kum 21:17; Za 78:51“Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza,

nguvu zangu, tunda la kwanza la nguvu zangu,

umepita kwa heshima, umepita kwa uwezo.

4Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena,

kwa kuwa ulipanda kwenye kitanda cha baba yako,

kwenye kitanda changu na kukinajisi.

549:5 Mwa 29:33; Mit 4:17“Simeoni na Lawi ni wana ndugu:

panga zao ni silaha za jeuri.

649:6 Mit 1:15; Efe 5:11Mimi na nisiingie katika baraza lao,

nami nisiunganike katika kusanyiko lao,

kwa kuwa wamewaua watu katika hasira yao,

walikata mishipa ya miguu ya mafahali

kama walivyopenda.

749:7 Yos 19:1, 9; Mwa 29:35Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno,

nayo ghadhabu yao ni ya ukatili!

Nitawatawanya katika Yakobo

Na kuwasambaza katika Israeli.

849:8 1Nya 5:2; Kum 28:48“Yuda, ndugu zako watakusifu;

mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako;

wana wa baba yako watakusujudia.

949:9 Hes 24:9; Ay 38:39Ee Yuda, wewe ni mwana simba;

unarudi toka mawindoni, mwanangu.

Kama simba hunyemelea na kulala chini,

kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?

1049:10 Eze 21:27; Isa 42:1Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda,

wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake,

hadi aje yeye ambaye milki ni yake,

ambaye utii wa mataifa ni wake.

11Atamfunga punda wake katika mzabibu,

naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi;

atafua mavazi yake katika divai,

majoho yake katika damu ya mizabibu.

12Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai,

meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.

1349:13 Mwa 30:20; 10:19“Zabuloni ataishi pwani ya bahari

na kuwa bandari za kuegesha meli;

mpaka wake utapanuka kuelekea Sidoni.

14“Isakari ni punda mwenye nguvu

ambaye amelala kati ya mizigo yake.

1549:15 Yos 19:17-23; Eze 29:18Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika

na jinsi nchi yake inavyopendeza,

atainamisha bega lake kwenye mzigo

na kujitolea kwa ajili ya kazi ngumu.

16“Dani atahukumu watu wake kwa haki

kama mmoja wa makabila ya Israeli.

1749:17 Amu 18:27; Yer 8:17Dani atakuwa nyoka kando ya barabara,

nyoka mwenye sumu kando ya njia,

yule aumaye visigino vya farasi

ili yule ampandaye aanguke chali.

18“Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.

19“Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji,

lakini yeye atawageukia na kuwashinda kabisa.

2049:20 Mwa 30:13; Isa 25:6; Ay 29:6“Chakula cha Asheri kitakuwa kinono,

naye atatoa chakula kitamu kimfaacho mfalme.

21“Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru

azaaye watoto wazuri.

2249:22 Mwa 30:24; Eze 19:10“Yosefu ni mzabibu uzaao,

mzabibu uzaao ulio kando ya chemchemi,

ambao matawi yake hutanda ukutani.

23Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia,

wakampiga mshale kwa ukatili.

2449:24 Za 18:34; Isa 1:24Lakini upinde wake ulibaki imara,

mikono yake ikatiwa nguvu,

na mkono wa Mwenye Nguvu wa Yakobo,

kwa sababu ya Mchungaji, Mwamba wa Israeli,

2549:25 Kut 18:4; Mwa 27:28kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia,

kwa sababu ya Mwenyezi,49:25 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania. yeye anayekubariki

kwa baraka za mbinguni juu,

baraka za kilindi kilichoko chini,

baraka za matitini na za tumbo la uzazi.

26Baraka za baba yako ni kubwa

kuliko baraka za milima ya kale,

nyingi kuliko vilima vya kale.

Baraka hizo zote na zikae juu ya kichwa cha Yosefu,

juu ya paji la yule mkuu miongoni mwa ndugu zake.

2749:27 Amu 20:12-13; Ebr 1:8; Hes 31:11“Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu;

asubuhi hurarua mawindo yake,

jioni hugawa nyara.”

28Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.

Kifo Cha Yakobo

2949:29 Mwa 25:8; 2Sam 2:32Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti, 30pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba. 3149:31 Mwa 25:9; 23:19Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea. 32Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”

3349:33 Mwa 25:8; Mdo 7:15Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.

Bibelen på hverdagsdansk

1. Mosebog 49:1-33

Jakobs sidste ord til sine 12 sønner

1Derefter tilkaldte Jakob alle sine sønner, og de samlede sig omkring ham: „Nu skal jeg fortælle jer, hvordan det vil gå jer fremover.

2Kom og hør, I Jakobs sønner,

lyt til Israel, jeres far!

3Ruben, du min ældste søn,

det første skud på stammen,

ypperlig i rang og styrke,

4men uregerlig som havets bølger.

Du mistede din forret som førstefødt,

for du gik i seng med din fars kone.

Hvilken skændig handling

at vanære sin far sådan.

5Simeon og Levi, to alen af ét stykke,

mænd af vold og vrede ord.

6Jeres planer og motiver kan jeg ikke acceptere,

i galskab myrdede I mennesker og lemlæstede okser for sjov.

7Forbandet være jeres hidsighed,

forbandet jeres vrede og vold.

I bliver adskilt i Israel,

spredt ud over landet.

8Juda, dine brødre vil juble,

når du tilintetgør dine fjender.

Ja, dine brødre skal bøje sig for dig.

9Juda er en løve, der vogter over sit bytte.

Når han hviler sig, hvem tør da vække ham?

10Scepteret skal tilhøre Juda,

og han skal herske,

indtil den rette hersker kommer,49,10 Betydningen af det hebraiske shilo er omstridt, men det henviser nok til den Messiaskonge, der skulle komme fra Judas slægt.

han, som alle folkeslag skal lyde.

11Han binder sit æsel til en vinstok

og vasker sit tøj i druesaft.

12Hans øjne er mørkere end rødvin,

hans tænder hvidere end mælk.

13Zebulon vil havne ved havet,

hans land bliver hjemsted for skibe,

det strækker sig helt til Sidon.

14Issakar er stærk som et æsel,

han hviler sig mellem kvægfoldene.

15Når han opdager, hvor godt et sted, han har fundet

og hvor frugtbart landet er,

tager han villigt åget på skuldrene

og arbejder hårdt for føden.

16Dan skaffer sit folk deres ret

så godt som nogen af Israels stammer.

17Han er som en slange på stien,

hugger i hestens hæl, så rytteren styrter.

18Åh Gud, du er vores redning!

19Gad bliver angrebet af omstrejfende bander,

men han forfølger og udplyndrer dem.

20Asher får en overflod af afgrøder

og kan levere til kongens hof.

21Naftali løber frit omkring,

kommer gerne med smukke ord.49,21 Eller: „smukt afkom”. Oversættelsen er usikker i flere af disse korte, poetiske vers.

22Josef er som en vinstok, plantet ved kilden,

hvis ranker spreder sig over muren.

23Han blev beskudt med bitterheds pile,

hans modstandere behandlede ham hårdt,

24men han holdt sin bue med fasthed,

hans stærke arme rystede ikke.

Han blev hjulpet af Jakobs mægtige Gud,

og igennem det blev han en hyrde,

en frelser for Israels folk.

25Din fars Gud er din hjælper,

og den Almægtige velsigner dig

med himlens velsignelser ovenfra

og jordens velsignelser nedenfra,

med ægteskabelige glæder

og med mange børn.

26Den velsignelse, du får fra din far,

overgår de ældgamle bjerges velsignelser

og det, de evige høje kan tilbyde.

Må disse velsignelser hvile på Josefs hoved,

på issen af fyrsten blandt brødre.

27Benjamin er som en ulv på rov.

Han æder af sit bytte om morgenen

og deler ud af sit overskud om aftenen.”

28Det var, hvad Jakob sagde til Israels 12 stammeoverhoveder. Hver især fik de deres særlige ord med på vejen.

Jakobs død og begravelse

29Til sidst sagde Jakob til sine sønner: „Nu skal jeg dø. Begrav mig hos mine forfædre i Kana’ans land i hulen på Makpela-marken øst for Mamre, den mark, som Abraham købte af hittitten Efron. 30-32I den gravhule ligger Abraham og Sara begravet. Der ligger også Isak og Rebekka, og der har jeg selv begravet Lea.” 33Med disse ord til sine sønner udtrykte Jakob sin sidste vilje. Så lagde han sig til rette i sengen og drog sit sidste åndedrag.