Mwanzo 47 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 47:1-31

Yakobo Ambariki Farao

147:1 Mwa 46:31Yosefu akaenda na kumwambia Farao, “Baba yangu na ndugu zangu wamekuja kutoka nchi ya Kanaani wakiwa na makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na kila kitu walicho nacho, nao sasa wapo huko Gosheni.” 2Akachagua ndugu zake watano na kuwaonyesha kwa Farao.

347:3 Mwa 46:33Farao akawauliza hao ndugu zake, “Kazi yenu ni nini?”

Wakamjibu, “Watumishi wako ni wachunga mifugo, kama vile baba zetu walivyokuwa.” 447:4 Mwa 46:34Pia wakamwambia Farao, “Tumekuja kukaa huku kwa muda mfupi, kwa sababu njaa ni kali huko Kanaani, na mifugo ya watumishi wako haina malisho. Kwa hiyo sasa, tafadhali uruhusu watumishi wako wakae huko Gosheni.”

5Farao akamwambia Yosefu, “Baba yako na ndugu zako wamekuja kwako, 647:6 Kut 18:21nayo nchi ya Misri ipo mbele yako, uwakalishe baba yako na ndugu zako katika sehemu iliyo bora kupita zote katika nchi. Na waishi Gosheni. Kama unamfahamu yeyote miongoni mwao mwenye uwezo maalum, waweke wawe wasimamizi wa mifugo yangu.”

747:7 2Sam 14:22Ndipo Yosefu akamleta Yakobo baba yake na kumtambulisha mbele ya Farao. Baada ya Yakobo kumbariki Farao, 8Farao akamuuliza, “Je una umri gani?”

947:9 Mwa 25:7Naye Yakobo akamwambia Farao, “Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni miaka 130. Miaka yangu imekuwa michache na ya taabu, wala haikufikia miaka ya kusafiri ya baba zangu.” 1047:10 Mwa 47:7Kisha Yakobo akambariki Farao, naye akaondoka mbele ya uso wake.

1147:11 Hes 33:3, 5Ndipo Yosefu akawakalisha baba yake na ndugu zake katika nchi ya Misri na kuwapa milki katika sehemu bora sana ya nchi, wilaya ya Ramesesi, kama Farao alivyoelekeza. 1247:12 Mwa 45:11Pia Yosefu akampa baba yake, na ndugu zake na wote wa nyumbani mwa baba yake vyakula, kwa kulingana na hesabu ya watoto wao.

Uongozi Wa Yosefu Wakati Wa Njaa

1347:13 Mwa 12:10Hata hivyo, hapakuwepo chakula katika sehemu yote kwa kuwa njaa ilikuwa kali sana; Misri na Kanaani zote zikaharibiwa kwa sababu ya njaa. 1447:14 Kut 7:23Yosefu akakusanya fedha zote zilizopatikana kutoka mauzo ya nafaka huko Misri na Kanaani, akazileta kwenye jumba la kifalme la Farao. 1547:15 Kut 16:3Fedha za watu wa Misri na Kanaani zilipokwisha, Wamisri wote wakamjia Yosefu na kumwambia, “Tupatie chakula. Kwa nini tufe mbele ya macho yako? Fedha zetu zimekwisha.”

1647:16 Mwa 47:18, 19Yosefu akawaambia, “Basi leteni mifugo yenu, nitawauzia chakula kwa kubadilisha na mifugo yenu, kwa kuwa fedha zenu zimekwisha.” 1747:17 Kut 14:9Kwa hiyo wakaleta mifugo yao kwa Yosefu, naye akawapa chakula kwa kubadilishana na farasi zao, kondoo na mbuzi zao, ngʼombe na punda zao. Katika mwaka huo wote Yosefu akawapa chakula kwa kubadilishana na mifugo yao yote.

18Mwaka ule ulipokwisha, wakamjia mwaka uliofuata na kumwambia, “Hatuwezi kuficha ukweli mbele za bwana wetu kwamba, kwa kuwa fedha zetu zimekwisha na wanyama wetu ni mali yako, sasa hakuna chochote kilichosalia kwa ajili ya bwana wetu isipokuwa miili yetu na ardhi yetu. 19Kwa nini tuangamie mbele ya macho yako, sisi pamoja na nchi yetu? Utununue sisi pamoja na ardhi yetu ili kubadilishana kwa chakula. Nasi pamoja na nchi yetu tutakuwa watumwa wa Farao. Tupe sisi mbegu ili tuweze kuishi wala tusife, nchi yetu isije ikawa ukiwa.”

2047:20 Mwa 12:10Kwa hiyo Yosefu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri. Wamisri, mmoja baada ya mwingine, waliuza mashamba yao, kwa sababu njaa ilikuwa kali sana kwao. Nchi ikawa mali ya Farao, 21naye Yosefu akawafanya watu watumike kama watumwa, kuanzia upande mmoja wa Misri hadi upande mwingine. 2247:22 Kum 14:28-29Hata hivyo, hakununua nchi ya makuhani, kwa sababu walikuwa wanapata mgawo wao wa kawaida kutoka kwa Farao, nao walikuwa na chakula cha kuwatosha kutokana na mgawo waliopewa na Farao. Hii ndiyo sababu hawakuuza ardhi yao.

2347:23 Neh 5:3Yosefu akawaambia watu, “Kwa vile nimewanunua ninyi pamoja na nchi yenu leo kuwa mali ya Farao, hapa kuna mbegu kwa ajili yenu ili mweze kuziotesha. 2447:24 Mwa 41:34Lakini wakati mazao yatakapokuwa tayari, mpeni Farao sehemu ya tano. Sehemu hizo nne zitakazobaki mtaziweka kama mbegu kwa ajili ya mashamba na kwa ajili ya chakula chenu wenyewe na cha watu wa nyumbani mwenu na watoto wenu.”

2547:25 Mwa 32:5Wakamwambia, “Umeokoa maisha yetu. Basi na tupate kibali mbele ya macho ya bwana wetu; tutakuwa watumwa wa Farao.”

2647:26 Mwa 41:34Basi Yosefu akaiweka iwe sheria kuhusu nchi ya Misri, ambayo inatumika mpaka leo, kwamba, sehemu ya tano ya mazao ni mali ya Farao. Ni nchi ya makuhani tu ambayo haikuwa ya Farao.

2747:27 Mwa 1:22Basi Waisraeli wakaishi Misri katika nchi ya Gosheni. Wakapata mali huko wakastawi na kuongezeka kwa wingi sana.

2847:28 Za 105:23Yakobo akaishi Misri miaka kumi na saba, nayo miaka ya maisha yake ilikuwa 147. 2947:29 Mwa 24:32Wakati ulipokaribia wa Israeli kufa, akamwita mwanawe Yosefu na kumwambia, “Kama nimepata kibali machoni pake, weka mkono wako chini ya paja langu na uniahidi kuwa utanifanyia fadhili na uaminifu. Usinizike Misri, 3047:30 Yos 24:32lakini nitakapopumzika na baba zangu, unichukue kutoka Misri, ukanizike walipozikwa.”

Yosefu akamwambia, “Nitafanya kama unavyosema.”

3147:31 Amu 15:12Akamwambia, “Niapie.” Ndipo Yosefu akamwapia, naye Israeli akaabudu, akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Начало 47:1-31

Встреча фараона с семьёй Юсуфа

1Юсуф пошёл к фараону и сказал ему:

– Мой отец и братья со своими стадами крупного и мелкого скота и всем имуществом пришли из земли Ханона и сейчас находятся в Гошене.

2Он выбрал пятерых из своих братьев и представил их фараону.

3Фараон спросил братьев:

– Чем вы занимаетесь?

Они ответили фараону:

– Твои рабы – пастухи, как и наши отцы, – 4ещё они сказали: – Мы пришли сюда жить, потому что в земле Ханона жестокий голод и твоим рабам негде пасти свои отары. Поэтому позволь твоим рабам поселиться в Гошене.

5Фараон сказал Юсуфу:

– Твой отец и братья пришли к тебе. 6Земля Египта – перед тобой; посели отца и братьев в лучшей части этой земли. Пусть живут в Гошене. А если ты знаешь среди них способных к тому людей, поставь их смотреть за моим собственным скотом.

7Юсуф привёл своего отца Якуба и представил его фараону, и Якуб благословил47:7 Или: «приветствовал». фараона. 8Фараон спросил его:

– Сколько тебе лет?

9Якуб ответил фараону:

– Я прожил на свете сто тридцать лет. Жизнь моя была короткой и трудной, и я не достиг возраста моих отцов.

10Якуб благословил фараона47:10 Или: «простился с фараоном». и покинул его дворец.

11Юсуф поселил отца и братьев в Египте и дал им в собственность лучшую часть земли в округе Раамсес, как повелел фараон. 12Юсуф обеспечил едой отца, и братьев, и весь свой род, дав каждому по числу членов его семьи.

Юсуф управляет Египтом во время голода

13Потом нигде не стало еды, потому что был жестокий голод; и Египет, и Ханон были истощены от голода. 14Юсуф собрал все деньги, какие только были в Египте и Ханоне, в уплату за зерно, которое у него покупали; он хранил их во дворце фараона. 15Когда кончились деньги и в Египте, и в Ханоне, все египтяне пришли к Юсуфу и сказали:

– Дай нам хлеба; зачем нам умирать у тебя на глазах? Наши деньги кончились.

16Юсуф сказал:

– Приведите свой скот, а я дам вам хлеба в обмен на него, раз у вас кончились деньги.

17Они привели к Юсуфу скот, и он дал им хлеба в обмен на лошадей, овец и коз, быков, коров и ослов. Он кормил их хлебом в тот год, в обмен на весь их скот.

18Когда год прошёл, они пришли к нему и сказали:

– Мы не станем таить от нашего господина, что наши деньги кончились и наш скот принадлежит тебе, так что у нас ничего не осталось для нашего господина, кроме наших тел и нашей земли. 19Зачем нам гибнуть у тебя на глазах, и нам самим, и нашей земле? Купи нас и нашу землю в обмен на хлеб, а мы с нашей землёй будем в рабстве у фараона; и дай нам семян, чтобы нам остаться в живых, и чтобы эта земля не опустела.

20Так Юсуф купил всю землю в Египте для фараона. Египтяне продали каждый своё поле, потому что голод одолел их, и земля стала собственностью фараона, 21а народ Юсуф сделал рабами, от одного конца Египта до другого. 22Он не купил только землю жрецов, потому что они получали постоянную долю от фараона, и этой доли, которую дал им фараон, им хватало на пропитание; вот почему они не продали свою землю.

23Юсуф сказал народу:

– Теперь, когда я купил вас и вашу землю для фараона, вот вам семена, чтобы засеять землю. 24Когда поспеет урожай, отдайте одну пятую от него фараону, а остальные четыре пятых будут вам на семена для полей и на пропитание для вас самих, для ваших домашних и для детей.

25Они сказали:

– Ты спас нам жизнь. Да найдём мы расположение в глазах нашего господина: мы будем рабами фараона.

26Так Юсуф установил в Египте закон о земле, который и сегодня в силе: одна пятая всего урожая принадлежит фараону, кроме урожая с земель жрецов, которая не стала собственностью фараона.

Последнее желание Якуба

27Исроильтяне жили в Египте в области Гошен; они приобрели там собственность и были плодовиты; число их возрастало.

28Якуб прожил в Египте семнадцать лет, так что всего он жил сто сорок семь лет. 29Когда пришло ему время умирать, он позвал своего сына Юсуфа и сказал ему:

– Если я нашёл расположение в твоих глазах, положи руку мне под бедро47:29 Таков был обычай принесения торжественной клятвы (см. 24:2). и обещай, что явишь мне милость и верность. Не хорони меня в Египте, 30но когда я сойду к моим отцам, вынеси меня из Египта и похорони там, где похоронены они.

Юсуф ответил:

– Я сделаю так, как ты говоришь.

31– Поклянись, – сказал он.

Юсуф поклялся ему, и Исроил поклонился, оперевшись на свой посох47:31 Или: «Исроил склонился на изголовье своей постели»..