Mwanzo 43 – NEN & CARSA

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 43:1-34

Safari Ya Pili Ya Kwenda Misri

143:1 Mwa 12:10Wakati huu njaa ilikuwa bado ni kali mno katika nchi. 2Hivyo wakati walikuwa wamemaliza kula nafaka yote waliyoileta kutoka Misri, Yakobo baba yao akawaambia, “Rudini Misri mkatununulie chakula kingine zaidi.”

343:3 Mwa 42:15Lakini Yuda akamwambia, “Mtu yule alituonya kwa msisitizo, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje na ndugu yenu.’ 4Kama utakubali ndugu yetu aende pamoja nasi, tutakwenda kuwanunulia chakula. 543:5 2Sam 3:13Lakini ikiwa hutamruhusu aende, hatutakwenda, kwa sababu mtu yule alituambia, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje pamoja na ndugu yenu.’ ”

643:6 Mwa 34:30Israeli akauliza, “Kwa nini mkaniletea taabu hii kwa kumwambia yule mtu mlikuwa na ndugu mwingine?”

743:7 Mwa 42:13Wakamjibu, “Yule mtu alituhoji kwa undani sana habari zetu na za jamaa yetu. Alituuliza, ‘Je, baba yenu bado yungali hai? Je mnaye ndugu mwingine?’ Sisi tulimjibu maswali yake tu. Tungewezaje kujua kwamba angesema, ‘Mleteni mdogo wenu hapa’?”

8Ndipo Yuda akamwambia baba yake Israeli, “Mtume kijana pamoja nami, nasi tutaondoka mara, ili sisi na wewe pamoja na watoto wetu tuweze kuishi, wala tusife. 943:9 Mwa 42:37; Flm 18-19Mimi mwenyewe nitakuhakikishia usalama wake, mimi mwenyewe nitawajibika kumrudisha. Ikiwa sitamrudisha kwako na kumweka mbele yako, nitakuwa mwenye lawama mbele yako maisha yangu yote. 1043:10 Mwa 45:9Hakika, kama hatukuchelewa kuondoka, tungekuwa tumekwenda na kurudi mara mbili.”

1143:11 Mwa 37:25Basi baba yao Israeli akawaambia, “Kama ni lazima iwe hivyo, basi fanyeni hivi: Wekeni baadhi ya mazao bora ya nchi katika mifuko yenu na mpelekeeni yule mtu kama zawadi, zeri kidogo, asali kidogo, vikolezo, manemane, kungu na lozi. 1243:12 Mwa 42:25Chukueni fedha mara mbili, kwa kuwa mtazirudisha zile fedha zilizowekwa midomoni mwa magunia yenu. Labda ziliwekwa kwa makosa. 13Mchukueni ndugu yenu pia mrudi kwa huyo mtu mara moja. 1443:14 Kum 13:17Naye Mungu Mwenyezi43:14 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). awajalieni rehema mbele ya huyo mtu ili apate kumwachia yule ndugu yenu na Benyamini mweze kurudi pamoja. Kwangu mimi kama nikufiwa nimefiwa.”

15Basi hao watu wakazichukua zile zawadi na zile fedha mara mbili pamoja na Benyamini. Wakafanya haraka kwenda Misri na walipofika wakajionyesha kwa Yosefu. 1643:16 Mwa 44:1, 4, 12Yosefu alipomwona Benyamini pamoja nao, akamwambia msimamizi wa nyumba yake, “Wachukue watu hawa nyumbani kwangu, mchinje mnyama na kuandalia chakula kwa kuwa watakula chakula cha mchana pamoja nami.”

1743:17 Mwa 43:16Yule Msimamizi akafanya kama Yosefu alivyomwambia na akawachukua wale watu nyumbani kwa Yosefu. 1843:18 Mwa 44:14Basi watu hao wakaogopa walipopelekwa nyumbani kwa Yosefu. Wakafikiri, “Tumeletwa hapa kwa ajili ya zile fedha zilizorudishwa katika magunia yetu mara ile ya kwanza. Anataka kutushambulia na kutushinda, atuchukue sisi kama watumwa, na atwae hawa punda zetu.”

19Hivyo wakamwendea msimamizi wa nyumba wa Yosefu na kuzungumza naye kwenye ingilio la nyumbani. 2043:20 Mwa 42:3Wakasema, “Tafadhali bwana, tulikuja hapa mara ya kwanza kununua chakula. 2143:21 Mwa 43:15Lakini mahali pale tulipotua wakati wa jioni tulifungua magunia yetu, na kila mmoja wetu akakuta fedha zake, kwenye mdomo wa gunia lake kiasi kile kile tulicholeta. Kwa hiyo tumezirudisha. 22Pia tumeleta fedha nyingine kwa ajili ya kununulia chakula. Hatujui ni nani aliziweka fedha hizo katika magunia yetu.”

23Akawaambia, “Vema, msiogope. Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, amewapa ninyi hazina katika magunia yenu; mimi nilipokea fedha yenu.” Ndipo akawaletea Simeoni.

2443:24 Mwa 43:16; 18:4Msimamizi akawapeleka wale watu katika nyumba ya Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu na kuwapa punda wao majani. 2543:25 Mwa 32:13Wakaandaa zawadi zao ili wampe Yosefu wakati atakapofika adhuhuri, kwa kuwa walikuwa wamesikia kwamba watakula chakula huko.

2643:26 Mt 2:11Yosefu alipokuja nyumbani, walimkabidhi zile zawadi walizokuwa nazo, ambazo walikuwa wamezileta mle nyumbani, nao wakamsujudia hadi nchi. 2743:27 Mwa 37:3Akawauliza kuhusu hali yao, kisha akawaambia, “Yule baba yenu mzee mliyeniambia habari zake, yu hali gani? Je, bado yu hai?”

2843:28 Mwa 37:7Wakamjibu, “Mtumishi wako baba yetu bado anaishi na ni mzima.” Kisha wakainama chini kumpa heshima.

2943:29 Mwa 42:13Alipotazama na kumwona Benyamini ndugu yake, mwana wa mama yake hasa, akauliza, “Je, huyu ndiye ndugu yenu wa mwisho, ambaye mlinieleza habari zake?” Ndipo akasema, “Mungu na akufadhili, mwanangu.” 30Akiwa ameguswa sana kwa kumwona ndugu yake, Yosefu akatoka nje kwa haraka na kutafuta mahali pa kulilia. Akaingia kwenye chumba chake cha pekee na kulilia humo.

31Baada ya kunawa uso wake, akatoka nje na huku akijizuia akasema, “Pakueni chakula.”

3243:32 Mwa 46:34Wakampakulia Yosefu peke yake, ndugu zake peke yao na Wamisri waliokula pamoja naye peke yao, kwa sababu Wamisri wasingeweza kula pamoja na Waebrania, kwa maana ilikuwa ni chukizo kwa Wamisri. 33Watu hao walikuwa wameketi mbele yake kwa mfuatano wa umri wao, kuanzia mzaliwa wa kwanza hadi mzaliwa wa mwisho, wakatazamana wao kwa wao kwa mshangao. 3443:34 Mwa 37:3Wakati walipelekewa sehemu ya chakula kutoka mezani mwa Yosefu, sehemu ya Benyamini ilikuwa mara tano zaidi ya sehemu ya wale wengine. Kwa hiyo wakanywa na kufurahi pamoja naye.

Священное Писание (Восточный перевод), версия с «Аллахом»

Начало 43:1-34

Якуб отпускает Вениамина в Египет

1В той земле по-прежнему свирепствовал голод. 2Когда они съели всё зерно, привезённое из Египта, отец сказал им:

– Вернитесь и купите нам ещё немного еды.

3Но Иуда сказал ему:

– Тот человек нас строго предупредил: «Не показывайтесь мне на глаза, если с вами не будет вашего брата». 4Если ты отпустишь с нами брата, то мы пойдём и купим для тебя еды. 5Но если ты не отпустишь его, мы не пойдём, потому что тот человек сказал нам: «Не показывайтесь мне на глаза, если с вами не будет вашего брата».

6– Зачем вы навели на меня эту беду, зачем сказали тому человеку, что у вас есть ещё один брат? – спросил Исраил.

7Они ответили:

– Тот человек подробно расспрашивал нас о нас самих и о нашей семье: «Жив ли ещё ваш отец? Нет ли у вас ещё одного брата?» Мы просто отвечали на его вопросы. Откуда нам было знать, что он скажет: «Приведите сюда вашего брата»?

8Иуда сказал Исраилу, своему отцу:

– Отпусти мальчика со мной, и мы тотчас же отправимся, чтобы все мы выжили и не погибли: и мы, и ты, и наши дети. 9Я лично буду за него порукой; с меня лично ты спросишь за него. Если я не приведу его к тебе и не поставлю здесь перед тобой, я буду виноват перед тобой до самой смерти. 10Если бы мы не медлили, то могли бы пойти и вернуться уже дважды.

11Тогда их отец Исраил сказал им:

– Если этого не избежать, то сделайте вот что: положите в ваши сумки лучшие плоды этой земли и отнесите в дар тому человеку – бальзам и мёд, специи и мирру, фисташки и миндаль. 12Возьмите вдвое больше серебра, чтобы вам принести с собой и то, что было положено обратно в ваши мешки: возможно, это была ошибка. 13Возьмите и вашего брата и, не медля, идите снова к тому человеку. 14Пусть Бог Всемогущий дарует вам милость перед ним, чтобы он позволил и другому вашему брату, и Вениамину вернуться с вами. Что же до меня, то если мне суждено лишиться детей, пусть я лишусь.

Второе прибытие братьев Юсуфа в Египет

15Они взяли подарки и вдвое больше серебра, затем взяли Вениамина, немедля отправились в Египет и предстали перед Юсуфом. 16Когда Юсуф увидел, что Вениамин с ними, он сказал своему управляющему:

– Отведи этих людей ко мне в дом, заколи что-нибудь из скота и приготовь обед; они будут есть со мной в полдень.

17Человек сделал, как ему было велено, и привёл их в дом Юсуфа. 18Они испугались, когда их привели к нему в дом, потому что подумали: «Нас привели сюда из-за серебра, которое вернулось в наши мешки в первый раз. Он хочет напасть на нас, и одолеть, и взять в рабство, и забрать наших ослов».

19Они подошли к управляющему Юсуфа и заговорили с ним у входа в дом:

20– Послушай, господин, – сказали они, – мы уже приходили сюда один раз купить еды, 21но когда мы остановились на ночь и развязали мешки, каждый из нас нашёл там своё серебро полным весом; поэтому мы принесли его обратно. 22Мы принесли с собой и ещё серебра, чтобы купить еды, и мы не знаем, кто в прошлый раз положил наше серебро к нам в мешки.

23Он ответил:

– Всё в порядке, не бойтесь. Ваш Бог – Бог вашего отца – положил это сокровище в ваши мешки, а я получил ваше серебро.

Затем он вывел к ним Шимона.

24Управляющий привёл братьев в дом Юсуфа, дал им воды вымыть ноги и дал корма их ослам. 25Они приготовили подарки к прибытию Юсуфа в полдень, потому что им сказали, что они будут там обедать.

26Когда Юсуф пришёл домой, они преподнесли ему подарки и склонились перед ним до земли. 27Он спросил их о здоровье, потом сказал:

– А как ваш престарелый отец, о котором вы говорили мне? Жив ли он ещё?

28Они ответили:

– Раб твой, наш отец, ещё жив и здоров.

И почтительно поклонились ему. 29Он оглянулся и увидел своего брата Вениамина, сына своей матери.

Он спросил:

– Это ваш младший брат, тот, о котором вы говорили мне? Аллах да будет милостив к тебе, мой сын.

30Глубоко тронутый видом брата, он поспешно ушёл и искал укромного места. Он вошёл к себе в комнату и там разрыдался. 31Затем, умыв лицо, он вновь вышел к гостям и, взяв себя в руки, сказал:

– Подавайте еду.

32Ему подали отдельно, братьям отдельно и египтянам, которые ели с ним, отдельно, потому что египтяне не могли есть с евреями, это было мерзко для египтян. 33Братьев усадили перед ним по возрасту, от первенца до младшего; и они глядели друг на друга в изумлении. 34Им подавали кушанья со стола Юсуфа, и доля Вениамина была впятеро больше, чем у других. Они пировали и пили с ним вволю.