Mwanzo 43 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 43:1-34

Safari Ya Pili Ya Kwenda Misri

143:1 Mwa 12:10Wakati huu njaa ilikuwa bado ni kali mno katika nchi. 2Hivyo wakati walikuwa wamemaliza kula nafaka yote waliyoileta kutoka Misri, Yakobo baba yao akawaambia, “Rudini Misri mkatununulie chakula kingine zaidi.”

343:3 Mwa 42:15Lakini Yuda akamwambia, “Mtu yule alituonya kwa msisitizo, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje na ndugu yenu.’ 4Kama utakubali ndugu yetu aende pamoja nasi, tutakwenda kuwanunulia chakula. 543:5 2Sam 3:13Lakini ikiwa hutamruhusu aende, hatutakwenda, kwa sababu mtu yule alituambia, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje pamoja na ndugu yenu.’ ”

643:6 Mwa 34:30Israeli akauliza, “Kwa nini mkaniletea taabu hii kwa kumwambia yule mtu mlikuwa na ndugu mwingine?”

743:7 Mwa 42:13Wakamjibu, “Yule mtu alituhoji kwa undani sana habari zetu na za jamaa yetu. Alituuliza, ‘Je, baba yenu bado yungali hai? Je mnaye ndugu mwingine?’ Sisi tulimjibu maswali yake tu. Tungewezaje kujua kwamba angesema, ‘Mleteni mdogo wenu hapa’?”

8Ndipo Yuda akamwambia baba yake Israeli, “Mtume kijana pamoja nami, nasi tutaondoka mara, ili sisi na wewe pamoja na watoto wetu tuweze kuishi, wala tusife. 943:9 Mwa 42:37; Flm 18-19Mimi mwenyewe nitakuhakikishia usalama wake, mimi mwenyewe nitawajibika kumrudisha. Ikiwa sitamrudisha kwako na kumweka mbele yako, nitakuwa mwenye lawama mbele yako maisha yangu yote. 1043:10 Mwa 45:9Hakika, kama hatukuchelewa kuondoka, tungekuwa tumekwenda na kurudi mara mbili.”

1143:11 Mwa 37:25Basi baba yao Israeli akawaambia, “Kama ni lazima iwe hivyo, basi fanyeni hivi: Wekeni baadhi ya mazao bora ya nchi katika mifuko yenu na mpelekeeni yule mtu kama zawadi, zeri kidogo, asali kidogo, vikolezo, manemane, kungu na lozi. 1243:12 Mwa 42:25Chukueni fedha mara mbili, kwa kuwa mtazirudisha zile fedha zilizowekwa midomoni mwa magunia yenu. Labda ziliwekwa kwa makosa. 13Mchukueni ndugu yenu pia mrudi kwa huyo mtu mara moja. 1443:14 Kum 13:17Naye Mungu Mwenyezi43:14 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). awajalieni rehema mbele ya huyo mtu ili apate kumwachia yule ndugu yenu na Benyamini mweze kurudi pamoja. Kwangu mimi kama nikufiwa nimefiwa.”

15Basi hao watu wakazichukua zile zawadi na zile fedha mara mbili pamoja na Benyamini. Wakafanya haraka kwenda Misri na walipofika wakajionyesha kwa Yosefu. 1643:16 Mwa 44:1, 4, 12Yosefu alipomwona Benyamini pamoja nao, akamwambia msimamizi wa nyumba yake, “Wachukue watu hawa nyumbani kwangu, mchinje mnyama na kuandalia chakula kwa kuwa watakula chakula cha mchana pamoja nami.”

1743:17 Mwa 43:16Yule Msimamizi akafanya kama Yosefu alivyomwambia na akawachukua wale watu nyumbani kwa Yosefu. 1843:18 Mwa 44:14Basi watu hao wakaogopa walipopelekwa nyumbani kwa Yosefu. Wakafikiri, “Tumeletwa hapa kwa ajili ya zile fedha zilizorudishwa katika magunia yetu mara ile ya kwanza. Anataka kutushambulia na kutushinda, atuchukue sisi kama watumwa, na atwae hawa punda zetu.”

19Hivyo wakamwendea msimamizi wa nyumba wa Yosefu na kuzungumza naye kwenye ingilio la nyumbani. 2043:20 Mwa 42:3Wakasema, “Tafadhali bwana, tulikuja hapa mara ya kwanza kununua chakula. 2143:21 Mwa 43:15Lakini mahali pale tulipotua wakati wa jioni tulifungua magunia yetu, na kila mmoja wetu akakuta fedha zake, kwenye mdomo wa gunia lake kiasi kile kile tulicholeta. Kwa hiyo tumezirudisha. 22Pia tumeleta fedha nyingine kwa ajili ya kununulia chakula. Hatujui ni nani aliziweka fedha hizo katika magunia yetu.”

23Akawaambia, “Vema, msiogope. Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, amewapa ninyi hazina katika magunia yenu; mimi nilipokea fedha yenu.” Ndipo akawaletea Simeoni.

2443:24 Mwa 43:16; 18:4Msimamizi akawapeleka wale watu katika nyumba ya Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu na kuwapa punda wao majani. 2543:25 Mwa 32:13Wakaandaa zawadi zao ili wampe Yosefu wakati atakapofika adhuhuri, kwa kuwa walikuwa wamesikia kwamba watakula chakula huko.

2643:26 Mt 2:11Yosefu alipokuja nyumbani, walimkabidhi zile zawadi walizokuwa nazo, ambazo walikuwa wamezileta mle nyumbani, nao wakamsujudia hadi nchi. 2743:27 Mwa 37:3Akawauliza kuhusu hali yao, kisha akawaambia, “Yule baba yenu mzee mliyeniambia habari zake, yu hali gani? Je, bado yu hai?”

2843:28 Mwa 37:7Wakamjibu, “Mtumishi wako baba yetu bado anaishi na ni mzima.” Kisha wakainama chini kumpa heshima.

2943:29 Mwa 42:13Alipotazama na kumwona Benyamini ndugu yake, mwana wa mama yake hasa, akauliza, “Je, huyu ndiye ndugu yenu wa mwisho, ambaye mlinieleza habari zake?” Ndipo akasema, “Mungu na akufadhili, mwanangu.” 30Akiwa ameguswa sana kwa kumwona ndugu yake, Yosefu akatoka nje kwa haraka na kutafuta mahali pa kulilia. Akaingia kwenye chumba chake cha pekee na kulilia humo.

31Baada ya kunawa uso wake, akatoka nje na huku akijizuia akasema, “Pakueni chakula.”

3243:32 Mwa 46:34Wakampakulia Yosefu peke yake, ndugu zake peke yao na Wamisri waliokula pamoja naye peke yao, kwa sababu Wamisri wasingeweza kula pamoja na Waebrania, kwa maana ilikuwa ni chukizo kwa Wamisri. 33Watu hao walikuwa wameketi mbele yake kwa mfuatano wa umri wao, kuanzia mzaliwa wa kwanza hadi mzaliwa wa mwisho, wakatazamana wao kwa wao kwa mshangao. 3443:34 Mwa 37:3Wakati walipelekewa sehemu ya chakula kutoka mezani mwa Yosefu, sehemu ya Benyamini ilikuwa mara tano zaidi ya sehemu ya wale wengine. Kwa hiyo wakanywa na kufurahi pamoja naye.

Bibelen på hverdagsdansk

1. Mosebog 43:1-34

Benjamin kommer med til Egypten

1Imidlertid fortsatte hungersnøden i Kana’ans land, 2så da kornet, som Josefs brødre havde hentet i Egypten, var ved at slippe op, sagde Jakob til sine sønner: „Tag af sted igen og køb os noget mere korn.”

3„Manden mente det alvorligt, da han advarede os imod at komme tilbage uden Benjamin!” indvendte Juda. 4„Hvis du vil lade drengen komme med os, rejser vi gerne derned og køber korn, 5men hvis du ikke vil det, er der ikke noget at gøre. Manden sagde udtrykkeligt, at vi ikke måtte komme uden Benjamin!”

6„Hvorfor i alverden fortalte I ham, at I havde en bror til?” jamrede Jakob. „Hvordan kunne I være så onde imod mig?”

7„Manden forhørte os jo indgående om vores familie!” svarede de. „Han ville vide, om vores far stadig levede, og om vi havde flere brødre. Vi var da nødt til at svare ham! Hvordan kunne vi vide, at han ville sige: ‚Hent jeres bror herned?’ ”

8Juda var ved at miste tålmodigheden: „Far, giv os nu lov til at tage drengen med, så vi kan komme af sted, inden vi alle sammen dør af sult—både vi, du og vores børn! 9Jeg garanterer dig for, at han vil være i sikre hænder! Jeg vil personligt tage den fulde skyld, hvis han ikke vender tilbage i god behold. 10Hvis vi ikke havde spildt tiden med snak frem og tilbage, kunne vi have været i Egypten og tilbage igen to gange allerede!”

11Endelig gav Jakob sig. „Hvis der ikke er nogen anden udvej, så lov mig i hvert fald at fylde jeres sække op med de bedste varer, vores land kan tilbyde, og aflever dem som gave til denne mand. Tag balsam, honning, krydderier, myrra, pistacienødder og mandler. 12Tag dobbelt så mange penge med, som kornet koster, så I kan betale det tilbage, som lå oven i jeres sække. Det var nok en fejltagelse, at I fik dem med hjem. 13Tag så jeres bror og rejs tilbage til manden. 14Må Gud den almægtige være jer nådig, når I står over for ham, så han løslader Simeon og lader Benjamin vende tilbage i god behold. Hvis jeg skal opleve den smerte at miste mine børn, så lad mig da gøre det!”

15Brødrene tog så Benjamin og gaverne og dobbelt så mange penge med og skyndte sig af sted til Egypten, hvor deres ankomst blev meldt til Josef. 16Da Josef så, at Benjamin var med, sagde han til sin husholder: „Før de der mænd hen til mit hus og lav et festmåltid. De skal spise hos mig i dag ved middagstid.” 17Husholderen gjorde, som han havde fået besked på, og førte brødrene til Josefs hus, 18men de blev bange, da de så, hvor de blev ført hen.

„Han vil nok anholde os og gøre os til slaver og tage vores æsler på grund af det med pengene oven i sækkene!” sagde de til hinanden. „Han tror sikkert, vi stjal dem!”

19Derfor gik de hen til husholderen, som stod ved indgangen 20og sagde: „Undskyld, men der er noget, vi må fortælle dig: Da vi var på vej hjem fra Egypten sidste gang, 21standsede vi undervejs for at overnatte, og da vi åbnede vores sække, lå de penge, som vi havde betalt for kornet, oven i sækkene! Se, her er de! Vi har taget dem med tilbage! 22Og vi har taget ekstra med, så vi kan købe mere korn! Men vi aner ikke, hvem der lagde pengene i vores sække.”

23„Det skal I ikke være bekymrede over,” svarede husholderen. „Det må være jeres fædres Gud, som har lagt dem oven i jeres sække. Vi har i alt fald fået betaling for det korn, I købte.” Så hentede han Simeon, 24hvorefter de alle blev lukket ind i Josefs hus og fik vand, så de kunne vaske støvet af deres fødder, mens æslerne blev fodret udenfor. 25Da de fik at vide, at de skulle spise der i huset, fik de travlt med at gøre deres gaver til Josef parat. 26Da Josef kom ind, gav de ham deres gaver og bøjede sig dybt med ansigtet til jorden.

27Josef spurgte dem, hvordan de havde haft det. „Og hvordan går det med jeres far—ham, I fortalte mig om? Han må være gammel! Lever han endnu?”

28„Ja,” svarede de, „han lever og har det godt.” Så bøjede de sig endnu en gang for Josef.

29Josef så på sin bror Benjamin og spurgte: „Er det så jeres yngste bror, som I fortalte mig om? Må Gud være med dig, min dreng.” 30Mere fik han ikke sagt, før han måtte skynde sig ud og ind i sit soveværelse for at give tårerne frit løb. Følelserne over for hans egen lillebror overvældede ham. 31Så beherskede han sig, vaskede sit ansigt og gik tilbage til brødrene. „Bring maden ind!” beordrede han.

32Josef spiste for sig selv, mens brødrene blev opvartet ved et andet bord, og de tilstedeværende egyptere sad ved et tredje bord. Egypterne bryder sig nemlig ikke om at spise sammen med hebræere. 33Josef havde placeret brødrene umiddelbart foran sig, efter alder, så den ældste sad først og den yngste sidst, hvilket fik dem til at sende hinanden undrende blikke. 34Maden blev bragt dem fra Josefs eget bord, og Benjamin fik den største portion—fem gange så meget som de andre! Der var rigeligt med mad og drikke, og snakken gik lystigt imellem dem.