Mwanzo 41 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 41:1-57

Ndoto Za Farao

141:1 Kut 2:5Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili, 241:2 Ay 40:21wakati ngʼombe saba, wazuri na wanono, walitokea mtoni wakajilisha kwenye matete. 3Baada yao ngʼombe wengine saba, wabaya na waliokonda, wakatokea mtoni Naili wakasimama kando ya wale wanono ukingoni mwa mto. 441:4 Mwa 41:7Wale ngʼombe wabaya na waliokonda wakawala wale saba wazuri na wanono. Kisha Farao akaamka.

5Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja. 641:6 Za 11:6Baadaye, masuke mengine saba yakachipua, yakiwa membamba yaliyonyaushwa na upepo wa mashariki. 741:7 Mwa 41:4Masuke yale membamba yakameza yale masuke saba yenye afya na yaliyojaa. Basi Farao akaamka kutoka usingizini, kumbe ilikuwa ndoto.

841:8 Kut 7:11, 22; Dan 4:18Asubuhi yake, alifadhaika akilini, hivyo akawaita waaguzi wote pamoja na watu wenye busara wa Misri. Walipokuja, Farao akawaeleza ndoto zake, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kumfasiria.

9Ndipo mnyweshaji mkuu alipomwambia Farao, “Leo nimekumbushwa kuhusu kosa langu. 1041:10 Mwa 40:2Wakati fulani Farao aliwakasirikia watumishi wake, akanifunga mimi na mwokaji mkuu katika nyumba ya mkuu wa ulinzi. 1141:11 Mwa 40:5Kila mmoja wetu aliota ndoto katika usiku mmoja na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti. 1241:12 Mwa 40:12Basi kijana wa Kiebrania aliyekuwa pamoja nasi huko, alikuwa mtumishi wa mkuu wa kikosi cha ulinzi. Tulimweleza ndoto zetu, naye akatufasiria, akitupa kila mtu tafsiri ya ndoto yake. 1341:13 Mwa 40:22Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.”

1441:14 Za 105:20; Rut 3:3Basi, Farao akatuma Yosefu aitwe, naye akatolewa kifungoni haraka. Baada ya kunyoa na kubadilisha nguo zake akaenda mbele ya Farao.

1541:15 Dan 5:16Farao akamwambia Yosefu, “Nimeota ndoto, wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuifasiri. Lakini nimesikia ikisemwa kwa habari yako kwamba unapoelezwa ndoto waweza kuifasiri.”

1641:16 Mwa 40:8Yosefu akamjibu Farao, “Siwezi kuifasiri, lakini Mungu atampa Farao jibu analolihitaji.”

17Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Katika ndoto yangu nilikuwa nimesimama ukingoni mwa Mto Naili, 18nikawaona ngʼombe saba, wazuri na wanono, wakijitokeza kutoka mtoni wakaja kujilisha kwenye matete. 19Baada ya hao, ngʼombe wengine saba wadhaifu wakatokea, wabaya sana na waliokonda. Kamwe sikuwahi kuona ngʼombe wabaya jinsi hiyo katika nchi yote ya Misri. 20Hao ngʼombe waliokonda na wabaya sana wakawala wale ngʼombe saba walionona waliojitokeza kwanza. 21Lakini hata baada ya kuwala, hakuna mtu ambaye angeweza kusema kwamba wamekula, bado walionekana wabaya kama mwanzoni. Kisha nikaamka kutoka usingizini.

22“Pia katika ndoto zangu niliona masuke saba ya nafaka, yamejaa na mazuri, yanakua katika bua moja. 23Baada ya hayo masuke mengine saba yakachipua, yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki. 24Yale masuke membamba ya nafaka yakayameza yale masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka. Nimewaeleza waaguzi, wala hakuna yeyote aliyeweza kunifasiria.”

2541:25 Dan 2:45Ndipo Yosefu akamwambia Farao, “Ndoto za Farao ni ndoto iyo hiyo moja. Mungu amemfunulia Farao jambo analokusudia kufanya karibuni. 26Ngʼombe saba wazuri ni miaka saba, nayo masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka ni miaka saba, ni ndoto iyo hiyo moja. 27Ngʼombe saba waliokonda na wabaya wale waliojitokeza baadaye ni miaka saba, vivyo hivyo masuke saba ya ngano yaliyodhoofika na kukaushwa na upepo wa mashariki, ni miaka saba ya njaa.

28“Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni. 2941:29 Mwa 41:47Miaka saba ya neema inakuja katika nchi yote ya Misri, 3041:30 Mwa 41:54; 47:13lakini itafuata miaka saba ya njaa. Ndipo neema yote ya Misri itasahaulika na njaa itaikumba nchi.

31“Neema iliyokuwa katika nchi haitakumbukwa, kwa sababu njaa itakayofuata itakuwa kali mno. 32Sababu ya ndoto kumjia Farao kwa namna mbili ni kwamba jambo hilo Mungu ameshaamua kwa hakika, naye Mungu atalifanya karibuni.

3341:33 Mwa 41:39“Basi sasa Farao na atafute mtu mwenye akili na hekima ili amweke kuwa msimamizi wa nchi ya Misri. 3441:34 Es 2:3Farao na aweke wenye amri nchini kote wakusanye sehemu ya tano ya mavuno ya Misri katika miaka hii saba ya neema. 3541:35 Mwa 41:48Wakusanye chakula chote katika miaka hii saba ya neema inayokuja na kuhifadhi nafaka chini ya mamlaka ya Farao, iwe akiba ya chakula katika miji. 36Chakula hiki kitakuwa akiba ya tahadhari kwa ajili ya nchi, ili kitumike katika ile miaka saba ya njaa itakayokuja Misri, ili nchi isiharibiwe na njaa.”

37Mpango huu ulionekana mzuri kwa Farao na kwa maafisa wake wote. 3841:38 Hes 27:18; Dan 4:8-9, 18; 5:11, 14Hivyo Farao akawauliza, “Je tunaweza kumpata yeyote kama mtu huyu, ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”

39Ndipo Farao akamwambia Yosefu, “Maadamu Mungu amekufunulia yote haya, hakuna mwingine yeyote mwenye akili na hekima kama wewe. 4041:40 Za 105:21-22; Mdo 7:10Wewe utakuwa msimamizi wa jumba langu la kifalme, na watu wangu wote watatii amri zako. Ni kuhusu kiti cha ufalme tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.”

Yosefu Msimamizi Wa Misri

4141:41 Mwa 42:6Kwa hiyo Farao akamwambia Yosefu, “Sasa nakuweka uwe msimamizi wa nchi yote ya Misri.” 4241:42 Es 3:10; Dan 5:29Ndipo Farao akaivua pete yake ya muhuri kutoka kidoleni mwake na kuivalisha katika kidole cha Yosefu. Akamvika majoho mazuri ya kitani safi na mkufu wa dhahabu shingoni mwake. 4341:43 Isa 2:7Akampandisha katika gari lake la farasi kama msaidizi wake, watu wakatangulia wakishangilia, wakisema, “Fungueni njia!” Ndivyo Farao alivyomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nchi yote ya Misri.

44Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Mimi ni Farao, lakini pasipo neno lako, hakuna mtu mwenye ruhusa kuinua mkono au mguu katika nchi yote ya Misri.” 4541:45 Es 2:7Farao akamwita Yosefu Safenath-Panea, pia akampa Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni,41:45 Yaani Heliopoli (Mji wa Jua). kuwa mke wake. Ndipo Yosefu akaitembelea nchi yote ya Misri.

4641:46 Mit 22:29Yosefu alikuwa na miaka thelathini alipoingia katika utumishi wa Farao mfalme wa Misri. Naye Yosefu akatoka mbele ya Farao akasafiri katika nchi yote ya Misri. 4741:47 Mwa 41:29Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana. 4841:48 Mwa 41:34Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo. 4941:49 Mwa 12:2Yosefu alihifadhi nafaka nyingi, mfano wa mchanga wa bahari, ilikuwa nyingi mno kiasi kwamba walishindwa kuweka kumbukumbu kwa sababu akiba ilizidi sana kupita kipimo.

50Kabla ya miaka ya njaa kuanza, Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, alikuwa amemzalia Yosefu wana wawili wa kiume. 5141:51 Hes 1:34Yosefu akamwita mzaliwa wake wa kwanza Manase, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote pamoja na jamaa yote ya nyumba ya baba yangu.” 5241:52 Mwa 17:6Mwana wa pili akamwita Efraimu, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenistawisha katika nchi ya mateso yangu.”

53Ile miaka saba ya neema huko Misri ikaisha, 5441:54 Mdo 7:11nayo miaka ile saba ya njaa ikaanza, sawasawa na alivyosema Yosefu. Kulikuwa na njaa katika nchi nyingine zote, bali katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula. 55Wakati nchi yote ya Misri ilipopatwa na njaa, watu wakamlilia Farao ili awape chakula. Ndipo Farao alipowaagiza Wamisri wote, akisema, “Nendeni kwa Yosefu, nanyi mfanye anachowaambia.”

56Wakati njaa ilipokuwa imeenea katika nchi yote, Yosefu akafungua ghala za vyakula na kuwauzia Wamisri nafaka, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno katika nchi yote ya Misri. 57Pia nchi nyingine zote zilikuja Misri kununua nafaka kutoka kwa Yosefu, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno duniani kote.

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Начало 41:1-57

Юсуф толкует сны фараона

1Прошло два года, и фараону приснился сон: он стоял на берегу Нила, 2и вот из реки поднялись семь коров – гладких и жирных – и стали пастись в тростниках. 3Вслед за ними вышли из Нила другие семь коров – безобразных и тощих – и встали рядом с теми на берегу реки. 4И безобразные, тощие коровы пожрали семь гладких, жирных коров. Тут фараон проснулся.

5Он заснул вновь, и ему приснился другой сон: семь колосьев – здоровых и полных – росли на одном стебле. 6Вслед за ними выросли ещё семь колосьев – тощих и опалённых восточным ветром. 7Тощие колосья проглотили семь здоровых, полных колосьев. Тут фараон проснулся, это был сон.

8Утром его не оставляла тревога. Он созвал всех чародеев и мудрецов Египта и рассказал им свои сны, но никто не смог их истолковать.

9Тогда главный виночерпий сказал фараону:

– Теперь я вспоминаю, что провинился. 10Однажды фараон разгневался на своих слуг и заключил меня и главного пекаря в доме начальника стражи. 11И мне, и ему в одну и ту же ночь приснился сон, и каждый сон имел своё значение. 12Там с нами был молодой еврей, слуга начальника стражи. Мы рассказали ему наши сны, и он истолковал их нам; каждому он дал своё толкование. 13И как он истолковал, так всё и вышло: меня возвратили на прежнюю службу, а того посадили на кол.

14Фараон послал за Юсуфом, и его спешно привели из темницы. Он подстригся, сменил одежду и предстал перед фараоном. 15Фараон сказал Юсуфу:

– Мне приснился сон, и никто не может его истолковать. Но я слышал о тебе, что ты понимаешь сны и умеешь толковать их.

16Юсуф ответил:

– Не я, но Всевышний даст фараону ответ во благо.

17Фараон сказал Юсуфу:

– Мне снилось, что я стою на берегу Нила, 18и вдруг из реки поднялись семь коров, жирных и гладких, и стали пастись в тростниках. 19Вслед за ними поднялись семь других коров – костлявых, худых и таких безобразных, каких я никогда прежде не видел во всей земле египетской. 20Тощие, безобразные коровы пожрали семь жирных коров, которые вышли первыми. 21Но это не пошло им впрок: они остались такими же безобразными, как и прежде. Тут я проснулся.

22Потом я видел во сне семь колосьев на одном стебле, полных доброго зерна. 23Вслед за ними выросли другие семь колосьев – сухие, тощие и опалённые восточным ветром. 24Тощие колосья проглотили семь полных колосьев. Я рассказал чародеям, но никто не смог дать мне объяснение.

25Юсуф сказал фараону:

– Смысл обоих снов фараона один. Всевышний открыл фараону, что Он собирается сделать. 26Семь хороших коров – это семь лет, и семь хороших колосьев – это семь лет; смысл тот же. 27Семь худых, безобразных коров, которые пришли следом, – это семь лет, и так же – семь тощих колосьев, опалённых восточным ветром, – это семь лет голода.

28Вот что я имел в виду, когда сказал фараону, что Всевышний открыл ему Свои замыслы. 29В земле египетской наступают семь лет великого изобилия, 30а за ними последуют семь лет голода, когда всё изобилие в Египте будет забыто, и голод опустошит землю. 31Прежнее изобилие забудется в этой земле из-за голода, который последует за ним, потому что голод будет жестокий. 32А то, что сон повторился фараону дважды, означает, что Всевышний твёрдо определил это и вскоре исполнит Свой замысел.

33Пусть же фараон найдёт проницательного и мудрого человека и поставит его над землёй Египта. 34Пусть фараон назначит чиновников по всей стране, чтобы они собирали пятую часть урожая в Египте в те семь лет изобилия. 35Пусть в те добрые годы они собирают всё продовольствие, что поступает к ним, и пусть властью фараона запасают зерно и хранят его в городах. 36Это продовольствие будет для страны про запас, чтобы страна не погибла в те семь лет голода, которые потом будут в Египте.

Юсуф назначается главным правителем Египта

37Фараон и все его приближённые одобрили этот план. 38Фараон спросил своих приближённых:

– Найдём ли мы ещё такого, как этот человек, в котором Дух Всевышнего?

39И фараон сказал Юсуфу:

– Раз Всевышний открыл тебе всё это, значит, нет никого мудрее и проницательнее тебя. 40Я ставлю тебя над моим домом, и весь мой народ будет слушаться твоих приказов. Только троном я буду выше тебя.

41Фараон сказал Юсуфу:

– Смотри, я ставлю тебя над всей землёй Египта.

42Он снял с пальца свой перстень и надел на палец Юсуфу, он одел его в одежды из тонкого полотна и повесил ему на шею золотую цепь. 43Он велел возить его в колеснице как второго после себя41:43 Или: «в колеснице второго после себя»; или: «в своей второй колеснице». и кричать перед ним: «Дорогу!»41:43 Или: «Кланяйтесь!» Так он поставил его над всей землёй Египта.

44Фараон сказал Юсуфу:

– Я фараон, но без твоего слова никто во всём Египте не посмеет и пальцем шевельнуть.

45Он дал Юсуфу имя Цафнат-Панеах и отдал ему в жёны Асенефу, дочь Потифера, жреца города Она41:45 То есть Гелиополь; также в ст. 50 и 46:20.. И Юсуф отправился в путь по всей египетской земле41:45 Или: «получил власть над всей землёй египетской»; или: «путешествовал по всей земле египетской»; так же в ст. 46..

46Юсуфу было тридцать лет, когда он поступил на службу к фараону, царю Египта. Юсуф вышел от фараона и отправился в путь по всему Египту. 47В семь лет изобилия земля приносила богатый урожай. 48Юсуф собирал весь урожай тех семи лет изобилия в Египте и складывал его в городах; в каждом городе он складывал урожай с окрестных полей. 49Собранного Юсуфом зерна было так много, как песка в море, и он перестал вести ему счёт, потому что сосчитать его было невозможно.

50Прежде чем пришли годы голода, у Юсуфа родились два сына от Асенефы, дочери Потифера, жреца города Она. 51Юсуф назвал своего первенца Манасса («дать забыть») и сказал: «Это потому, что Всевышний дал мне забыть все мои страдания и дом моего отца». 52Второго сына он назвал Ефраим («быть плодовитым»), сказав: «Это потому, что Всевышний сделал меня плодовитым в земле моего страдания».

53Семь лет изобилия в Египте подошли к концу, 54и начались семь лет голода, как Юсуф и предсказал. Голод был во всех других землях, только в земле Египта была пища.

55Когда весь Египет начал голодать, люди взмолились к фараону о пище, и фараон сказал египтянам:

– Идите к Юсуфу и делайте, как он скажет.

56Когда голод распространился по всей стране, Юсуф открыл склады и стал продавать зерно египтянам, потому что голод в Египте был жестокий.

57И из всех стран приходили в Египет, чтобы купить у Юсуфа зерна, потому что по всему миру был жестокий голод.