Mwanzo 41 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 41:1-57

Ndoto Za Farao

141:1 Kut 2:5Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili, 241:2 Ay 40:21wakati ngʼombe saba, wazuri na wanono, walitokea mtoni wakajilisha kwenye matete. 3Baada yao ngʼombe wengine saba, wabaya na waliokonda, wakatokea mtoni Naili wakasimama kando ya wale wanono ukingoni mwa mto. 441:4 Mwa 41:7Wale ngʼombe wabaya na waliokonda wakawala wale saba wazuri na wanono. Kisha Farao akaamka.

5Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja. 641:6 Za 11:6Baadaye, masuke mengine saba yakachipua, yakiwa membamba yaliyonyaushwa na upepo wa mashariki. 741:7 Mwa 41:4Masuke yale membamba yakameza yale masuke saba yenye afya na yaliyojaa. Basi Farao akaamka kutoka usingizini, kumbe ilikuwa ndoto.

841:8 Kut 7:11, 22; Dan 4:18Asubuhi yake, alifadhaika akilini, hivyo akawaita waaguzi wote pamoja na watu wenye busara wa Misri. Walipokuja, Farao akawaeleza ndoto zake, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kumfasiria.

9Ndipo mnyweshaji mkuu alipomwambia Farao, “Leo nimekumbushwa kuhusu kosa langu. 1041:10 Mwa 40:2Wakati fulani Farao aliwakasirikia watumishi wake, akanifunga mimi na mwokaji mkuu katika nyumba ya mkuu wa ulinzi. 1141:11 Mwa 40:5Kila mmoja wetu aliota ndoto katika usiku mmoja na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti. 1241:12 Mwa 40:12Basi kijana wa Kiebrania aliyekuwa pamoja nasi huko, alikuwa mtumishi wa mkuu wa kikosi cha ulinzi. Tulimweleza ndoto zetu, naye akatufasiria, akitupa kila mtu tafsiri ya ndoto yake. 1341:13 Mwa 40:22Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.”

1441:14 Za 105:20; Rut 3:3Basi, Farao akatuma Yosefu aitwe, naye akatolewa kifungoni haraka. Baada ya kunyoa na kubadilisha nguo zake akaenda mbele ya Farao.

1541:15 Dan 5:16Farao akamwambia Yosefu, “Nimeota ndoto, wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuifasiri. Lakini nimesikia ikisemwa kwa habari yako kwamba unapoelezwa ndoto waweza kuifasiri.”

1641:16 Mwa 40:8Yosefu akamjibu Farao, “Siwezi kuifasiri, lakini Mungu atampa Farao jibu analolihitaji.”

17Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Katika ndoto yangu nilikuwa nimesimama ukingoni mwa Mto Naili, 18nikawaona ngʼombe saba, wazuri na wanono, wakijitokeza kutoka mtoni wakaja kujilisha kwenye matete. 19Baada ya hao, ngʼombe wengine saba wadhaifu wakatokea, wabaya sana na waliokonda. Kamwe sikuwahi kuona ngʼombe wabaya jinsi hiyo katika nchi yote ya Misri. 20Hao ngʼombe waliokonda na wabaya sana wakawala wale ngʼombe saba walionona waliojitokeza kwanza. 21Lakini hata baada ya kuwala, hakuna mtu ambaye angeweza kusema kwamba wamekula, bado walionekana wabaya kama mwanzoni. Kisha nikaamka kutoka usingizini.

22“Pia katika ndoto zangu niliona masuke saba ya nafaka, yamejaa na mazuri, yanakua katika bua moja. 23Baada ya hayo masuke mengine saba yakachipua, yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki. 24Yale masuke membamba ya nafaka yakayameza yale masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka. Nimewaeleza waaguzi, wala hakuna yeyote aliyeweza kunifasiria.”

2541:25 Dan 2:45Ndipo Yosefu akamwambia Farao, “Ndoto za Farao ni ndoto iyo hiyo moja. Mungu amemfunulia Farao jambo analokusudia kufanya karibuni. 26Ngʼombe saba wazuri ni miaka saba, nayo masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka ni miaka saba, ni ndoto iyo hiyo moja. 27Ngʼombe saba waliokonda na wabaya wale waliojitokeza baadaye ni miaka saba, vivyo hivyo masuke saba ya ngano yaliyodhoofika na kukaushwa na upepo wa mashariki, ni miaka saba ya njaa.

28“Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni. 2941:29 Mwa 41:47Miaka saba ya neema inakuja katika nchi yote ya Misri, 3041:30 Mwa 41:54; 47:13lakini itafuata miaka saba ya njaa. Ndipo neema yote ya Misri itasahaulika na njaa itaikumba nchi.

31“Neema iliyokuwa katika nchi haitakumbukwa, kwa sababu njaa itakayofuata itakuwa kali mno. 32Sababu ya ndoto kumjia Farao kwa namna mbili ni kwamba jambo hilo Mungu ameshaamua kwa hakika, naye Mungu atalifanya karibuni.

3341:33 Mwa 41:39“Basi sasa Farao na atafute mtu mwenye akili na hekima ili amweke kuwa msimamizi wa nchi ya Misri. 3441:34 Es 2:3Farao na aweke wenye amri nchini kote wakusanye sehemu ya tano ya mavuno ya Misri katika miaka hii saba ya neema. 3541:35 Mwa 41:48Wakusanye chakula chote katika miaka hii saba ya neema inayokuja na kuhifadhi nafaka chini ya mamlaka ya Farao, iwe akiba ya chakula katika miji. 36Chakula hiki kitakuwa akiba ya tahadhari kwa ajili ya nchi, ili kitumike katika ile miaka saba ya njaa itakayokuja Misri, ili nchi isiharibiwe na njaa.”

37Mpango huu ulionekana mzuri kwa Farao na kwa maafisa wake wote. 3841:38 Hes 27:18; Dan 4:8-9, 18; 5:11, 14Hivyo Farao akawauliza, “Je tunaweza kumpata yeyote kama mtu huyu, ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”

39Ndipo Farao akamwambia Yosefu, “Maadamu Mungu amekufunulia yote haya, hakuna mwingine yeyote mwenye akili na hekima kama wewe. 4041:40 Za 105:21-22; Mdo 7:10Wewe utakuwa msimamizi wa jumba langu la kifalme, na watu wangu wote watatii amri zako. Ni kuhusu kiti cha ufalme tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.”

Yosefu Msimamizi Wa Misri

4141:41 Mwa 42:6Kwa hiyo Farao akamwambia Yosefu, “Sasa nakuweka uwe msimamizi wa nchi yote ya Misri.” 4241:42 Es 3:10; Dan 5:29Ndipo Farao akaivua pete yake ya muhuri kutoka kidoleni mwake na kuivalisha katika kidole cha Yosefu. Akamvika majoho mazuri ya kitani safi na mkufu wa dhahabu shingoni mwake. 4341:43 Isa 2:7Akampandisha katika gari lake la farasi kama msaidizi wake, watu wakatangulia wakishangilia, wakisema, “Fungueni njia!” Ndivyo Farao alivyomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nchi yote ya Misri.

44Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Mimi ni Farao, lakini pasipo neno lako, hakuna mtu mwenye ruhusa kuinua mkono au mguu katika nchi yote ya Misri.” 4541:45 Es 2:7Farao akamwita Yosefu Safenath-Panea, pia akampa Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni,41:45 Yaani Heliopoli (Mji wa Jua). kuwa mke wake. Ndipo Yosefu akaitembelea nchi yote ya Misri.

4641:46 Mit 22:29Yosefu alikuwa na miaka thelathini alipoingia katika utumishi wa Farao mfalme wa Misri. Naye Yosefu akatoka mbele ya Farao akasafiri katika nchi yote ya Misri. 4741:47 Mwa 41:29Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana. 4841:48 Mwa 41:34Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo. 4941:49 Mwa 12:2Yosefu alihifadhi nafaka nyingi, mfano wa mchanga wa bahari, ilikuwa nyingi mno kiasi kwamba walishindwa kuweka kumbukumbu kwa sababu akiba ilizidi sana kupita kipimo.

50Kabla ya miaka ya njaa kuanza, Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, alikuwa amemzalia Yosefu wana wawili wa kiume. 5141:51 Hes 1:34Yosefu akamwita mzaliwa wake wa kwanza Manase, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote pamoja na jamaa yote ya nyumba ya baba yangu.” 5241:52 Mwa 17:6Mwana wa pili akamwita Efraimu, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenistawisha katika nchi ya mateso yangu.”

53Ile miaka saba ya neema huko Misri ikaisha, 5441:54 Mdo 7:11nayo miaka ile saba ya njaa ikaanza, sawasawa na alivyosema Yosefu. Kulikuwa na njaa katika nchi nyingine zote, bali katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula. 55Wakati nchi yote ya Misri ilipopatwa na njaa, watu wakamlilia Farao ili awape chakula. Ndipo Farao alipowaagiza Wamisri wote, akisema, “Nendeni kwa Yosefu, nanyi mfanye anachowaambia.”

56Wakati njaa ilipokuwa imeenea katika nchi yote, Yosefu akafungua ghala za vyakula na kuwauzia Wamisri nafaka, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno katika nchi yote ya Misri. 57Pia nchi nyingine zote zilikuja Misri kununua nafaka kutoka kwa Yosefu, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno duniani kote.

Bibelen på hverdagsdansk

1. Mosebog 41:1-57

Josef tyder Faraos drømme

1To år senere drømte Farao en nat, at han stod på Nilens bred. 2Pludselig kom der syv smukke og fede køer op af floden og gav sig til at græsse på flodbredden. 3Derefter kom der endnu syv køer op af floden, men de var grimme og magre. De stillede sig ved siden af de syv første køer på flodbredden, 4og de syv grimme og magre køer åd de syv smukke og fede køer. I samme øjeblik vågnede Farao.

5Lidt efter faldt han igen i søvn og havde en anden drøm. Denne gang så han syv fulde og modne aks vokse frem på et og samme strå. 6Pludselig voksede der syv aks mere frem på strået, men de var tynde og helt indtørrede af østenvinden. 7De visne aks opslugte de fulde aks. Da vågnede Farao og blev klar over, at han havde drømt noget betydningsfuldt.

8Drømmene bekymrede ham, så om morgenen sendte han bud efter alle Egyptens vise mænd og drømmetydere og fortalte dem, hvad han havde drømt. Men ingen af dem kunne tyde drømmene for ham. 9Da tog mundskænken ordet: „Jeg er kommet i tanker om noget, der skete for længe siden,” sagde han til Farao. 10„Dengang du var vred på hofbageren og mig og kastede os i fængsel, 11da skete det en nat, at både bageren og jeg havde en drøm, og begge drømme havde en betydning. 12I fængslet var der en ung hebræisk slave, som arbejdede for livvagtens øverstbefalende. Ham fortalte vi vores drømme, og han tydede dem for os. 13Og det gik nøjagtig, som han sagde: Jeg fik mit gamle job tilbage, og hofbageren blev henrettet.”

14Farao sendte straks bud efter Josef. Han blev hurtigt taget ud af fængslet, blev barberet og fik pænt tøj på. Så blev han ført frem for Farao. 15„I nat havde jeg en drøm,” begyndte Farao. „Ingen af de her mænd kan tyde den, men jeg har hørt, at du kun behøver at høre en drøm, så kan du tyde den.”

16„Jeg kan ikke tyde drømme,” svarede Josef, „men Gud vil åbenbare for Farao, hvad drømmen betyder.”

17Så fortalte Farao ham sin drøm. „Jeg stod ved Nilens bred,” sagde han. 18„Pludselig så jeg syv fede og velplejede køer stige op af floden, og de begyndte straks at græsse på bredden. 19Bagefter steg der syv magre og forsømte køer op af floden, de var så radmagre, at jeg aldrig har set noget lignende i hele Egypten. 20Og de magre og grimme køer åd de syv fede køer, 21men da de havde ædt dem, var de stadig lige magre. Så vågnede jeg.”

22„Lidt senere havde jeg endnu en drøm,” fortsatte Farao. „Denne gang så jeg syv fulde og modne aks på et og samme strå. 23Men lidt efter skød der syv tynde og visne aks frem på strået, helt udtørrede af østenvinden. 24Og de visne aks opslugte de fulde aks. Jeg har fortalt de to drømme til drømmetyderne, men ingen af dem kunne tyde dem for mig.”

25„Begge drømme betyder det samme,” sagde Josef. „Gennem dem har Gud ladet Farao vide, hvad der vil ske i den nærmeste fremtid. 26De syv fede køer og de syv fulde aks svarer til hinanden. De betyder syv gode år. 27De syv magre køer og de syv visne aks svarer ligeledes til hinanden. De betyder syv år med hungersnød. 28Som jeg sagde før, har Gud med disse drømme afsløret for Farao, hvad han vil gøre i den nærmeste fremtid: 29I de næste syv år vil hele Egypten opleve stor overflod, 30men bagefter kommer der en syvårig periode med hungersnød, og man vil glemme, at der var overflod i Egypten. Hungersnøden vil hærge hele jorden. 31Man vil glemme overfloden, fordi hungersnøden bliver så hård. 32At Farao drømte to gange, betyder, at Guds beslutning står fast og at det, han har vist Farao, snart vil ske. 33Derfor vil jeg foreslå, at Farao finder en klog og dygtig mand og lader ham administrere et landsomfattende projekt. 34Udnævn derefter embedsmænd i alle distrikter med ansvar for at indsamle en femtedel af alt høstudbyttet i de syv gode år. 35Lad dem indsamle høstudbyttet og oplagre det i de aflåste kongelige kornmagasiner i byerne. 36På den måde vil der være nok at spise, når de syv års hungersnød kommer over Egypten, og en sultkatastrofe kan afværges.”

Josef bliver guvernør i Egypten

37Farao og hans embedsmænd syntes godt om Josefs forslag, 38og Farao udbrød: „Hvem er vel bedre egnet til opgaven end Josef? Han er jo fyldt med Guds Ånd!” 39Så vendte Farao sig mod Josef og sagde: „Siden Gud har åbenbaret drømmenes betydning for dig, må du være den klogeste mand i landet. 40Derfor giver jeg dig ansvar for mit palads og udnævner dig til at lede det store projekt. Dit ord skal være lov i Egypten. Kun jeg selv skal stå over dig. 41Jeg gør dig hermed til guvernør og øverste leder for hele Egypten.” 42Så tog Farao sin signetring af og satte den på Josefs finger som et tegn på hans autoritet. Han gav ham også smukke klæder og hængte den kongelige guldkæde om hans hals. 43Farao gav ham tilmed sin næstbedste vogn at køre i. Hvor som helst Josef kom frem, blev der råbt: „Giv plads!”41,43 Der bruges et egyptisk ord, hvis mening ikke kendes med sikkerhed. Det betyder muligvis: „bøj jer”, „giv plads” eller „vær velsignet”. I alle tilfælde angiver det Josefs høje position.

Således gjorde Farao Josef til øverste leder i Egypten, 44og han sagde til ham: „Jeg, Farao, konge af Egypten, sværger herved, at ingen i hele Egypten må foretage sig noget som helst uden din tilladelse.” 45Farao gav ham også et egyptisk navn: Safenat-Panea, og han gav ham Asenat til kone. Hun var en datter af Potifera, der var præst for solguden Ra i Heliopolis. Josef fik således ansvar for hele Egypten. 46Han var 30 år gammel, da han kom i kong Faraos tjeneste, og han rejste omkring i hele Egypten for at inspicere landet.

47De følgende syv år var der ganske rigtigt rekordhøst over alt i Egypten. 48I løbet af de syv år tog Josef en del af alt, hvad der blev høstet i Egypten, og oplagrede det i de kongelige kornmagasiner i byerne. 49Som årene gik, fyldtes kornmagasinerne til overflod. Der var så meget korn, som der er sand på stranden, så til sidst opgav man helt at holde regnskab med, hvor meget der var.

50I den periode—altså inden hungersnøden kom—fik Josef og Asenat, præsten Potiferas datter, to sønner. 51Josef kaldte sin ældste søn Manasse,41,51 På hebraisk ordspil med „at få til at glemme”. for han sagde: „Gud har ladet mig glemme min familie og al min ulykke.” 52Sin anden søn kaldte han Efraim,41,52 På hebraisk ordspil med „gøre rig”. for han sagde: „Gud har gjort mig rig her i det land, hvor jeg har lidt så meget.”

53Så endte de syv overflodsår, 54og hungersnødens syv år begyndte, nøjagtig som Josef havde forudsagt. Hungersnøden ramte alle lande, men i Egypten var der masser af korn i reservelagrene. 55Da nu egypterne begyndte at sulte, bad de Farao om mad. Men Farao sagde: „Henvend jer til Josef, og gør som han siger.”

56Så da hungersnøden blev rigtig alvorlig, åbnede Josef for kornmagasinerne og solgte korn til egypterne. 57Også folk fra de omliggende lande kom til Egypten for at købe korn af Josef, for der var streng hungersnød i hele verden.