Mwanzo 37 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 37:1-36

Ndoto Za Yosefu

137:1 Mwa 17:8; 10:19Yakobo akaishi Kanaani katika nchi ambayo baba yake alikuwa ameishi.

237:2 Za 78:71; 1Sam 2:24Zifuatazo ni habari za Yakobo.

Yosefu, kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga makundi ya kondoo na mbuzi pamoja na ndugu zake wa mama wengine, yaani wana wa Bilha na wana wa Zilpa wake za baba yake, naye akawa akimletea baba yake taarifa mbaya kuhusu hao ndugu zake.

337:3 Mwa 44:20; 2Sam 13:18-19Basi, Israeli akampenda Yosefu kuliko yeyote miongoni mwa kaka zake, kwani ni mwanawe wa uzeeni, akamshonea joho lililorembwa vizuri sana. 437:4 Mwa 27:41; Mdo 7:9Ndugu zake walipoona kwamba baba yao anampenda Yosefu kuliko yeyote mwingine miongoni mwao, walimchukia na hawakusema naye neno lolote jema.

5Yosefu akaota ndoto, naye alipowaeleza ndugu zake, wakamchukia zaidi. 6Akawaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota: 737:7 Mwa 42:6, 9; 43:26, 28Tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani, ghafula mganda wangu ukasimama wima, wakati miganda yenu ikiuzunguka na kuuinamia.”

837:8 Mwa 49:26; Kum 33:16Ndugu zake wakamwambia, “Wewe unakusudia kututawala? Hivi kweli wewe utatutawala sisi?” Wakaongeza kumchukia zaidi kwa sababu ya ndoto yake pamoja na yale aliyowaambia.

9Kisha akaota ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake akisema, “Sikilizeni, nimeota ndoto nyingine, wakati huu jua, mwezi na nyota kumi na moja zilikuwa zinanisujudia.”

1037:10 Rut 2:16Alipomwambia baba yake pamoja na ndugu zake, baba yake akamkemea akisema, “Ni ndoto gani hii uliyoota? Hivi kweli mama yako na mimi na ndugu zako tutakuja kukusujudia wewe hadi nchi?” 1137:11 Mdo 7:9; Lk 2:19, 51Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliweka jambo hilo moyoni.

Yosefu Auzwa Na Ndugu Zake

1237:12 Mwa 12:6Basi, ndugu zake walikuwa wamekwenda kuchunga makundi ya baba yao karibu na Shekemu, 1337:13 Mwa 17:5naye Israeli akamwambia Yosefu, “Kama ujuavyo, ndugu zako wanachunga makundi huko karibu na Shekemu. Njoo, nitakutuma kwao.”

Yosefu akajibu, “Vema sana, niko tayari.”

1437:14 1Sam 17:18Kwa hiyo akamwambia, “Nenda uone kama mambo yote ni salama kwa ndugu zako na makundi, kisha uniletee habari.” Ndipo akamtuma Yosefu kutoka Bonde la Hebroni.

Yosefu alipofika Shekemu, 15mtu mmoja akamkuta akizungukazunguka mashambani na akamuuliza, “Unatafuta nini?”

16Akajibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Unaweza kuniambia wanachunga wapi makundi yao?”

1737:17 2Fal 6:13Yule mtu akajibu, “Wamehama hapa. Nilisikia wakisema, ‘Twende Dothani.’ ”

Kwa hiyo Yosefu akawafuatilia ndugu zake na kuwakuta karibu na Dothani. 1837:18 Mk 14:1Ndugu zake walipomwona akiwa mbali, kabla hajawafikia, wakapanga shauri baya la kumuua.

1937:19 Mwa 28:12Wakaambiana, “Yule mwota ndoto anakuja! 2037:20 Mwa 50:20Njooni sasa, tumuue na kumtupa katika shimo mojawapo na tuseme kwamba mnyama mkali amemrarua. Kisha tutaona matokeo ya ndoto zake.”

2137:21 Mwa 42:22Reubeni aliposikia jambo hili, akajaribu kumwokoa kutoka mikononi mwao akasema, “Tusiutoe uhai wake. 2237:22 Mwa 37:20Tusimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.

2337:23 Mwa 37:3Kwa hiyo Yosefu alipowafikia ndugu zake, walimvua lile joho lake, lile joho lililorembwa vizuri alilokuwa amevaa. 2437:24 Mwa 37:4Kisha wakamchukua wakamtupa katika shimo. Wakati huo shimo lilikuwa tupu, halikuwa na maji ndani yake.

2537:25 Mwa 37:28Walipokaa ili wale chakula chao, wakainua macho wakaona msafara wa Waishmaeli ukija kutoka Gileadi. Ngamia wao walikuwa wamepakizwa mizigo ya vikolezo, uvumba na manemane, nao walikuwa njiani kuvipeleka Misri.

2637:26 Mwa 4:10Yuda akawaambia ndugu zake, “Tutafaidi nini ikiwa tutamuua ndugu yetu na kuificha damu yake? 2737:27 Mwa 42:21Njooni, tumuuze kwa hawa Waishmaeli. Tusimguse, kwa kuwa hata hivyo yeye ni ndugu yetu, nyama yetu na damu yetu wenyewe.” Ndugu zake wakakubali.

2837:28 Kut 21:16; Za 105:17Kwa hiyo wale wafanyabiashara Wamidiani walipofika pale, ndugu zake wakamtoa Yosefu kutoka kwenye lile shimo, na kumuuza kwa shekeli ishirini37:28 Shekeli 20 ni sawa na gramu 200. za fedha kwa wale Waishmaeli, ambao walimpeleka Misri.

2937:29 Ay 1:20; Yoe 2:13Reubeni aliporudi kutazama kwenye lile shimo na kuona kwamba Yosefu hayupo, alirarua nguo zake. 3037:30 Mwa 37:22Akawarudia ndugu zake na kusema, “Kijana hayuko mle! Nielekee wapi sasa?”

31Kisha wakalichukua lile joho la Yosefu, wakachinja mbuzi na kulichovya katika damu. 32Wakalichukua lile joho lililorembwa vizuri na kulipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeliokota hili joho. Uchunguze uone kama ni la mwanao.”

3337:33 Mwa 37:20Baba yao akalitambua akasema, “Hili ni joho la mwanangu! Mnyama mkali amemrarua. Hakika Yosefu ameraruliwa vipande vipande.”

3437:34 2Sam 3:31; 2Fal 6:30; Ay 16:15Kisha Yakobo akararua nguo zake, akavaa nguo ya gunia na kumwombolezea mwanawe kwa siku nyingi. 3537:35 Mwa 42:38; 2Sam 12:23Wanawe wote na binti zake wakaja kumfariji, lakini hakukubali kufarijiwa. Akasema, “Hapana, nitamwombolezea mwanangu mpaka nimfikie kaburini.” Kwa hiyo baba yake akaendelea kumlilia.

3637:36 Mwa 39:1; 1Sam 22:14Wakati ule ule, Wamidiani wakamuuza Yosefu huko Misri kwa Potifa, mmojawapo wa maafisa wa Farao, aliyekuwa mkuu wa ulinzi.

New International Reader’s Version

Genesis 37:1-36

Joseph Has Two Dreams

1Jacob lived in the land of Canaan. It’s the land where his father had stayed.

2Here is the story of the family line of Jacob.

Joseph was a young man. He was 17 years old. He was taking care of the flocks with some of his brothers. They were the sons of Bilhah and the sons of Zilpah, the wives of his father Jacob. Joseph brought their father a bad report about his brothers.

3Israel loved Joseph more than any of his other sons. That’s because Joseph had been born to him when he was old. Israel made him a beautiful robe. 4Joseph’s brothers saw that their father loved him more than any of them. So they hated Joseph. They couldn’t even speak one kind word to him.

5Joseph had a dream. When he told it to his brothers, they hated him even more. 6He said to them, “Listen to the dream I had. 7We were tying up bundles of grain out in the field. Suddenly my bundle stood up straight. Your bundles gathered around my bundle and bowed down to it.”

8His brothers said to him, “Do you plan to be king over us? Will you really rule over us?” So they hated him even more because of his dream. They didn’t like what he had said.

9Then Joseph had another dream. He told it to his brothers. “Listen,” he said. “I had another dream. This time the sun and moon and 11 stars were bowing down to me.”

10He told his father as well as his brothers. Then his father rebuked him. He said, “What about this dream you had? Will your mother and I and your brothers really do that? Will we really come and bow down to the ground in front of you?” 11His brothers were jealous of him. But his father kept the dreams in mind.

Joseph Is Sold by His Brothers

12Joseph’s brothers had gone to take care of their father’s flocks near Shechem. 13Israel said to Joseph, “As you know, your brothers are taking care of the flocks near Shechem. Come. I’m going to send you to them.”

“All right,” Joseph replied.

14So Israel said to him, “Go to your brothers. See how they are doing. Also see how the flocks are doing. Then come back and tell me.” So he sent him away from the Hebron Valley.

Joseph arrived at Shechem. 15A man found him wandering around in the fields. He asked Joseph, “What are you looking for?”

16He replied, “I’m looking for my brothers. Can you tell me where they are taking care of their flocks?”

17“They’ve moved on from here,” the man answered. “I heard them say, ‘Let’s go to Dothan.’ ”

So Joseph went to look for his brothers. He found them near Dothan. 18But they saw him a long way off. Before he reached them, they made plans to kill him.

19“Here comes that dreamer!” they said to one another. 20“Come. Let’s kill him. Let’s throw him into one of these empty wells. Let’s say that a wild animal ate him up. Then we’ll see whether his dreams will come true.”

21Reuben heard them talking. He tried to save Joseph from them. “Let’s not take his life,” he said. 22“Don’t spill any of his blood. Throw him into this empty well here in the desert. But don’t harm him yourselves.” Reuben said that to save Joseph from them. He was hoping he could take him back to his father.

23When Joseph came to his brothers, he was wearing his beautiful robe. They took it away from him. 24And they threw him into the well. The well was empty. There wasn’t any water in it.

25Then they sat down to eat their meal. As they did, they saw some Ishmaelite traders coming from Gilead. Their camels were loaded with spices, lotion and myrrh. They were on their way to take them down to Egypt.

26Judah said to his brothers, “What will we gain if we kill our brother and try to cover up what we’ve done? 27Come. Let’s sell him to these traders. Let’s not harm him ourselves. After all, he’s our brother. He’s our own flesh and blood.” Judah’s brothers agreed with him.

28The traders from Midian came by. Joseph’s brothers pulled him up out of the well. They sold him to the Ishmaelite traders for eight ounces of silver. Then the traders took him to Egypt.

29Later, Reuben came back to the empty well. He saw that Joseph wasn’t there. He was so upset that he tore his clothes. 30He went back to his brothers and said, “The boy isn’t there! Now what should I do?”

31Then they got Joseph’s beautiful robe. They killed a goat and dipped the robe in the blood. 32They took the robe back to their father. They said, “We found this. Take a look at it. See if it’s your son’s robe.”

33Jacob recognized it. He said, “It’s my son’s robe! A wild animal has eaten him up. Joseph must have been torn to pieces.”

34Jacob tore his clothes. He put on the rough clothing people wear when they’re sad. Then he mourned for his son many days. 35All Jacob’s other sons and daughters came to comfort him. But they weren’t able to. He said, “I will continue to mourn until I go down into the grave to be with my son.” So Joseph’s father mourned for him.

36But the traders from Midian sold Joseph to Potiphar in Egypt. Potiphar was one of Pharaoh’s officials. He was the captain of the palace guard.