Mwanzo 36 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 36:1-43

Wazao Wa Esau

(1 Nyakati 1:34-42)

136:1 Mwa 2:4; 25:30Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).

236:2 Mwa 26:34; 28:8-9Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi, 3pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.

436:4 1Nya 1:35Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli, 536:5 1Nya 1:35Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.

636:6 Mwa 12:5; 1Nya 1:35Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake. 736:7 Mwa 13:6; 27:39Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao. 836:8 Kum 2:4Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.

936:9 Mwa 2:4Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.

1036:10 Mwa 36:3Haya ndiyo majina ya wana wa Esau:

Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.

1136:11 1Nya 1:45Wana wa Elifazi ni:

Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.

1236:12 Kut 17:8, 16; 1Sam 15:2Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.

1336:13 Mwa 36:3Wana wa Reueli ni:

Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.

1436:14 Mwa 36:2Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni:

Yeushi, Yalamu na Kora.

1536:15 Mwa 36:19-40; Kut 15:15Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau:

Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni:

Temani, Omari, Sefo, Kenazi, 1636:16 Mwa 32:3Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.

1736:17 1Nya 1:37Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni:

Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.

1836:18 Mwa 36:2Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni:

Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.

1936:19 1Nya 1:35Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.

2036:20 Mwa 14:6Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile:

Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, 2136:21 Mwa 36:30Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.

22Wana wa Lotani walikuwa:

Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.

23Wana wa Shobali walikuwa:

Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.

2436:24 Mwa 36:2Wana wa Sibeoni walikuwa:

Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.

2536:25 Mwa 36:2Watoto wa Ana walikuwa:

Dishoni na Oholibama binti wa Ana.

26Wana wa Dishoni walikuwa:

Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.

27Wana wa Eseri walikuwa:

Bilhani, Zaavani na Akani.

28Wana wa Dishani walikuwa:

Usi na Arani.

2936:29 Mwa 36:20Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori:

Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, 3036:30 Mwa 36:21Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.

Watawala Wa Edomu

(1 Nyakati 1:43-54)

3136:31 Mwa 17:6Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:

32Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.

3336:33 Isa 34:6Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.

3436:34 Yer 49:7Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.

3536:35 Rut 1:1, 6; Mwa 19:37Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.

36Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.

3736:37 Mwa 26:22Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.

38Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.

39Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.

4036:40 Mwa 36:15Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao:

Timna, Alva, Yethethi, 41Oholibama, Ela, Pinoni, 42Kenazi, Temani, Mibsari, 4336:43 Mwa 36:9Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki.

Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.

Bibelen på hverdagsdansk

1. Mosebog 36:1-43

Esaus slægt

1Det følgende er Esaus historie, han som også blev kaldt Edom:

2Esau giftede sig med to kana’anæiske piger: Ada, en datter af hittitten Elon, og Oholibama, en datter af Ana og barnebarn af hivvitten Zibon. 3Han giftede sig også med sin kusine Basemat, en datter af Ishmael og søster til Nebajot. 4Esau og Ada fik en søn, der blev kaldt Elifaz. Esau og Basemat fik en søn, der blev kaldt Reuel. 5Esau og Oholibama fik tre sønner, der fik navnene Jeush, Jalam og Kora. Alle disse sønner blev født i Kana’ans land.

6Senere tog Esau sine koner, sine sønner, sine døtre, hele sin husstand og besætning og alt, hvad han havde samlet sig i Kana’ans land, og flyttede til et andet land af frygt for sin bror Jakob. 7Deres husdyr var jo også blevet alt for mange til, at de som fremmede kunne bo samme sted som de fastboende. Der var slet ikke græs nok. 8Esau slog sig derfor ned i Seirs bjergland.

9Her følger en liste over Esaus efterkommere, edomitterne, som bor i Seirs bjergland:

10-13Ada fødte som sagt Esau en søn, der fik navnet Elifaz, og han fik fem sønner: Teman, Omar, Zefo, Gatam og Kenaz. Elifaz havde også en kone, som hed Timna, og med hende fik han sønnen Amalek.

Esau og hans kone Basemat fik sønnen Reuel, og han fik fire sønner: Nahat, Zerach, Shamma og Mizza.

14Esaus kone Oholibama, en datter af Zibons søn Ana, fødte tre sønner: Jeush, Jalam og Kora.

15-16Esaus sønner og sønnesønner blev stamfædre for de forskellige stammer blandt Edoms folk. De stammer, der er kendt under navnene Teman, Omar, Zefo, Kenaz, Kora, Gatam og Amalek, nedstammer alle fra Elifaz, Esaus og Adas ældste søn.

17De stammer, der er kendt under navnene Nahat, Zerach, Shamma og Mizza, nedstammer alle fra Reuel, Esaus og Basemats søn.

18-19Desuden er der stammerne Jeush, Jalam og Kora, opkaldt efter de sønner, som Esau fik med sin kone Oholibama, Anas datter.

Edoms oprindelige indbyggere

20-21Her følger en liste med navnene på de stammer, som oprindeligt boede i Seirs land: Lotan, Shobal, Zibon, Ana, Dishon, Etzer og Dishan. De er efterkommere af og har navn efter horitten Seirs sønner.

22Lotan, Seirs søn, havde følgende sønner: Hori og Hemam. Lotan havde også en søster ved navn Timna.

23Shobals sønner hed Alvan, Manahat, Ebal, Shefo og Onam.

24Zibons sønner hed Ajja og Ana. Det var Ana, som opdagede en varm kilde i ørkenen, dengang han vogtede sin fars æsler. 25Anas børn var sønnen Dishon og datteren Oholibama. 26Dishons sønner hed Hemdan, Eshban, Jitran og Keran.

27Etzers sønner hed Bilhan, Za’avan og Akan.

28Dishans sønner hed Utz og Aran.

29-30Horitternes stammer i Seirs land hed altså: Lotan, Shobal, Zibon, Ana, Dishon, Etzer og Dishan.

De oprindelige konger i Seirs land

31-39Endnu før der var konger i Israel, herskede følgende konger i det, der nu hedder Edom: Først Bela, Beors søn, fra byen Dinhaba. Da han døde, efterfulgtes han af Jobab, Zerachs søn fra Botzra. Da Jobab døde, efterfulgtes han af Husham fra temanitternes område. Da Husham døde, blev Hadad konge. Han var søn af Bedad og kom fra byen Avit. Det var ham, der besejrede midjanitternes hær i Moabs land. Da Hadad døde, blev Samla fra Masreka konge. Da han døde, blev Shaul fra flodbyen Rehobot konge. Da han døde, blev Ba’al-Hanan, Ahbors søn, konge. Da han døde, blev Hadar fra Pau konge. Hans kone hed Mehetabel og var datter af Matred, som igen var datter af Mezahab.

40Slægtsoverhovederne i Esaus slægt hed Timna, Alva, Jetet, 41Oholibama, Ela, Pinon, 42Kenaz, Teman, Mibzar, 43Magdiel og Iram. Det område, som hver enkelt slægt boede i, overtog efterhånden slægtens navn.