Mwanzo 35 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 35:1-29

Yakobo Arudi Betheli

135:1 Mwa 12:8Kisha Mungu akamwambia Yakobo, “Panda uende Betheli ukakae huko na ukamjengee Mungu madhabahu huko, Yeye aliyekutokea ulipokuwa unamkimbia Esau ndugu yako.”

235:2 Yos 24:15; Kut 19:10, 14Hivyo Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake pamoja na wote waliokuwa naye, “Iondoeni miungu ya kigeni ile iliyoko katikati yenu, jitakaseni na mkabadilishe nguo zenu. 335:3 Mwa 32:7; Amu 2:15Kisha njooni, twende Betheli, mahali nitakapomjengea Mungu madhabahu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, ambaye amekuwa pamoja nami popote nilipokwenda.” 435:4 Mwa 24:22Kwa hiyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo, pamoja na pete zilizokuwa masikioni mwao. Yakobo akavizika chini ya mti wa mwaloni huko Shekemu. 535:5 Kut 15:16Kisha wakaondoka, na hofu ya Mungu ikawapata miji yote iliyowazunguka. Kwa hiyo hakuna aliyewafuatia wana wa Yakobo.

635:6 Mwa 28:19; 10:19Yakobo na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika Luzu (ndio Betheli), katika nchi ya Kanaani. 735:7 Mwa 8:20Huko akajenga madhabahu na akapaita mahali pale El-Betheli,35:7 El-Betheli maana yake Mungu wa Betheli. kwa sababu mahali pale ndipo Mungu alipojifunua kwake alipokuwa akimkimbia ndugu yake.

835:8 Mwa 24:59; 12:8Wakati huu Debora, mlezi wa Rebeka, akafa na akazikwa chini ya mti wa mwaloni ulioko chini ya Betheli. Kwa hiyo pakaitwa Alon-Bakuthi.35:8 Alon-Bakuthi maana yake Mwaloni wa Kilio.

935:9 Mwa 28:13; 32:29Baada ya Yakobo kurudi kutoka Padan-Aramu, Mungu alimtokea tena na kumbariki. 1035:10 Mwa 17:5Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini hutaitwa tena Yakobo, jina lako utakuwa Israeli.” Kwa hiyo akamwita Israeli.

1135:11 Mwa 17:1; 17:6Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi,35:11 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). ukazae na kuongezeka. Taifa na jamii ya mataifa itatoka kwako, nao wafalme watatoka viunoni mwako. 1235:12 Mwa 28:13; 12:7Nchi niliyowapa Abrahamu na Isaki nakupa wewe pia, nami nitawapa wazao wako baada yako.” 1335:13 Mwa 17:22Kisha Mungu akapanda juu kutoka kwake mahali pale alipozungumza naye.

1435:14 Mwa 28:18; Kut 29:40Yakobo akasimamisha nguzo ya jiwe mahali pale Mungu alipozungumza naye, akamimina sadaka ya kinywaji juu yake, pia akamimina mafuta juu yake. 1535:15 Mwa 12:8Yakobo akapaita mahali pale Mungu alipozungumza naye Betheli.35:15 Betheli maana yake Nyumba ya Mungu.

Vifo Vya Raheli Na Isaki

1635:16 Mwa 48:7Kisha wakaondoka Betheli. Walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kusikia uchungu na alipata shida kuu. 1735:17 Kut 1:15; Mwa 30:24Alipokuwa katika shida hii katika kujifungua, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwa sababu umempata mwana mwingine.” 1835:18 1Sam 4:21Hapo alipopumua pumzi yake ya mwisho, kwa maana alikuwa akifa, akamwita mwanawe Benoni.35:18 Benoni maana yake Mwana wa huzuni yangu. Lakini babaye akamwita Benyamini.35:18 Benyamini maana yake Mwana wa mkono wangu wa kuume.

1935:19 Mwa 48:7Kwa hiyo Raheli akafa, akazikwa kando ya njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu). 2035:20 1Sam 10:2; 6:18Juu ya kaburi lake, Yakobo akasimamisha nguzo, ambayo mpaka leo inatambulisha kaburi la Raheli.

21Israeli akaendelea tena na safari yake na kupiga hema mbele mnara wa Ederi. 22Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili.

Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili:

23Wana wa Lea walikuwa:

Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo,

Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni.

2435:24 Mwa 30:24; 35:18Wana wa Raheli walikuwa:

Yosefu na Benyamini.

2535:25 Mwa 30:24Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa:

Dani na Naftali.

2635:26 Mwa 37:2Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa:

Gadi na Asheri.

Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu.

2735:27 Mwa 13:18; Amu 1:10Yakobo akarudi nyumbani kwa baba yake Isaki huko Mamre, karibu na Kiriath-Arba (yaani Hebroni), ambapo walikuwa wameishi Abrahamu na Isaki. 2835:28 Mwa 25:7Isaki aliishi miaka 180. 2935:29 Mwa 15:15; 25:8-9Kisha Isaki akapumua pumzi yake ya mwisho akafa, akakusanywa pamoja na watu wake akiwa mzee wa miaka mingi. Nao wanawe Esau na Yakobo wakamzika.

Nueva Versión Internacional

Génesis 35:1-29

Jacob vuelve a Betel

1Dios dijo a Jacob: «Sube a Betel y quédate a vivir ahí. Erige allí un altar al Dios que se te apareció cuando escapabas de tu hermano Esaú».

2Entonces Jacob dijo a su familia y a quienes lo acompañaban: «Desháganse de todos los dioses extraños que tengan con ustedes, purifíquense y cámbiense de ropa. 3Subamos a Betel. Allí construiré un altar al Dios que me socorrió cuando estaba yo en peligro y que me ha acompañado en mi camino».

4Así que entregaron a Jacob todos los dioses extraños que tenían, junto con los aretes que llevaban en las orejas, y Jacob los enterró a la sombra de la encina que estaba cerca de Siquén. 5Cuando partieron, nadie persiguió a la familia de Jacob, porque un terror divino se apoderó de las ciudades vecinas.

6Fue así como Jacob y quienes lo acompañaban llegaron a Luz, es decir, Betel, en la tierra de Canaán. 7Erigió un altar y llamó a ese lugar El Betel,35:7 En hebreo, El Betel significa Dios de Betel. porque allí se le había revelado Dios cuando escapaba de su hermano Esaú.

8Por esos días murió Débora, la nodriza de Rebeca, y la sepultaron a la sombra de un árbol de roble que se encuentra cerca de Betel. Por eso Jacob llamó a ese lugar Elón Bacut.35:8 En hebreo, Elón Bacut significa roble del llanto.

9Cuando Jacob regresó de Padán Aram,35:9 Padán Aram. Es decir, el noroeste de Mesopotamia; también en v. 26. Dios se le apareció otra vez y lo bendijo 10con estas palabras: «Tu nombre es Jacob,35:10 En hebreo, Jacob significa él agarra el talón (en sentido figurado: él suplanta o engaña). pero ya no te llamarás así. De aquí en adelante te llamarás Israel».35:10 En hebreo, Israel significa él lucha con Dios. Y en efecto, ese fue el nombre que le puso.

11Luego Dios añadió: «Yo soy el Dios Todopoderoso. Sé fecundo y multiplícate. De ti nacerá una nación y una comunidad de naciones, y habrá reyes entre tus descendientes. 12La tierra que di a Abraham y a Isaac te la doy a ti y a tus descendientes». 13Y Dios se retiró del lugar donde había hablado con Jacob.

14Jacob erigió una piedra como monumento en el lugar donde Dios le había hablado. Vertió sobre ella una ofrenda líquida, la ungió con aceite 15y al lugar donde Dios le había hablado lo llamó Betel.35:15 En hebreo, Betel significa casa de Dios.

La muerte de Raquel y el pecado de Rubén

16Después partieron de Betel. Cuando estaban a cierta distancia de Efrata, Raquel dio a luz, pero tuvo un parto muy difícil. 17En el momento más difícil del parto, la partera le dijo: «¡No temas; estás por tener otro varón!». 18No obstante, ella se estaba muriendo y en sus últimos suspiros alcanzó a llamar a su hijo Benoní,35:18 En hebreo, Benoní significa hijo de mi aflicción o hijo de mi tristeza. pero Jacob, su padre, le puso por nombre Benjamín.35:18 En hebreo, Benjamín significa hijo de mi mano derecha.

19Así murió Raquel y la sepultaron en el camino que va hacia Efrata, que es Belén. 20Sobre la tumba Jacob erigió un monumento, que hasta el día de hoy señala el lugar donde Raquel fue sepultada.

21Israel siguió su camino y acampó más allá de la Torre del Rebaño. 22Mientras vivía en esa región, Rubén fue y se acostó con Bilhá, la concubina35:22 Véase nota en Gn 22:24. de su padre. Cuando Israel se enteró de esto, se enojó muchísimo.35:22 Cuando … muchísimo (LXX); Israel se enteró (TM).

Los hijos de Jacob

35:23-261Cr 2:1-2

Jacob tuvo doce hijos:

23Los hijos de Lea fueron:

Rubén, que era el primogénito de Jacob,

Simeón, Leví, Judá, Isacar y Zabulón.

24Los hijos de Raquel fueron:

José y Benjamín.

25Los hijos de Bilhá, la esclava de Raquel:

Dan y Neftalí.

26Los hijos de Zilpá, la esclava de Lea:

Gad y Aser.

Estos fueron los hijos que tuvo Jacob en Padán Aram.

Muerte de Isaac

27Jacob volvió a la casa de su padre Isaac en Mamré, cerca de Quiriat Arbá, es decir, Hebrón, donde también habían vivido Abraham e Isaac. 28Isaac tenía ciento ochenta años 29cuando se reunió con sus antepasados. Era ya muy anciano cuando murió; lo sepultaron sus hijos Esaú y Jacob.