Mwanzo 34 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 34:1-31

Dina Na Washekemu

134:1 Mwa 30:21Basi Dina, binti wa Yakobo aliyezaliwa na Lea, akatoka nje kuwatembelea wanawake wa nchi ile. 234:2 Mwa 33:19Ikawa Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mtawala wa eneo lile alipomwona, akamchukua na kumnajisi. 3Moyo wake ukavutwa sana kwa Dina binti Yakobo, akampenda huyu msichana na akazungumza naye kwa kumbembeleza. 434:4 Mwa 21:21Shekemu akamwambia baba yake Hamori, “Nipatie msichana huyu awe mke wangu.”

534:5 Mwa 34:2-3Yakobo aliposikia kwamba binti yake Dina amenajisiwa, wanawe walikuwa mashambani wakichunga mifugo yake, kwa hiyo akalinyamazia jambo hilo mpaka waliporudi nyumbani.

634:6 Amu 14:2-5Kisha Hamori baba yake Shekemu akaenda kuzungumza na Yakobo. 734:7 Kum 22:21; Amu 20:6Basi wana wa Yakobo walikuwa wamerudi kutoka mashambani mara tu waliposikia kilichotokea. Walikuwa wamejawa na huzuni na ghadhabu, kwa sababu Shekemu alikuwa amefanya jambo la aibu katika Israeli kwa kukutana kimwili na binti wa Yakobo, kitu ambacho hakingepasa kufanyika.

834:8 Mwa 21:21Lakini Hamori akawaambia, “Moyo wa mwanangu Shekemu umeelekea kwa binti yenu. Tafadhali mpeni awe mke wake. 934:9 Kum 7:3Oaneni na sisi, tupeni binti zenu, nanyi mchukue binti zetu. 1034:10 Mwa 47:6, 27; 13:9Mwaweza kuishi katikati yetu, nchi ni wazi kwenu. Ishini ndani yake, fanyeni biashara humu na mjipatie mali.”

1134:11 Mwa 32:5Kisha Shekemu akamwambia baba yake Dina pamoja na ndugu zake, “Na nipate kibali machoni penu, nami nitawapa chochote mtakachosema. 1234:12 Kum 22:29; 1Sam 18:25Niambieni kiasi cha mahari na zawadi nitakayoileta, hata iwe kubwa kiasi gani, nami nitawalipa chochote mtakachodai. Nipeni tu huyu msichana awe mke wangu.”

1334:13 Mwa 27:36Kwa sababu ndugu yao Dina alikuwa amenajisiwa, wana wa Yakobo wakajibu kwa udanganyifu walipozungumza na Shekemu pamoja na baba yake Hamori. 1434:14 Mwa 17:14; Isa 31:4Wakawaambia, “Hatuwezi kufanya jambo kama hili, hatuwezi kumtoa dada yetu kwa mtu ambaye hakutahiriwa. Hiyo itakuwa aibu kwetu. 1534:15 1Sam 11:2; Kut 12:48Tutakuruhusu kwa sharti moja tu, kwamba mtakuwa kama sisi kwa kuwatahiri wanaume wenu wote. 1634:16 Mwa 33:19Kisha tutawapa binti zetu na sisi tutawachukua binti zenu. Tutaishi kwenu na tutakuwa watu wamoja nanyi. 17Lakini mkikataa kutahiriwa, tutamchukua ndugu yetu na kuondoka.”

18Pendekezo lao likawa jema kwa Hamori na Shekemu mwanawe. 19Kijana mdogo, ambaye alikuwa ameheshimiwa kati ya wote walioishi nyumbani mwa baba yake, hakupoteza muda kufanya waliyoyasema, kwa sababu alikuwa amependezwa sana na binti Yakobo. 2034:20 Mwa 18:1Kwa hiyo Hamori na Shekemu mwanawe walikwenda kwenye lango la mji kuzungumza na wenzao wa mjini. 2134:21 Mwa 33:19Wakasema, “Hawa watu ni marafiki kwetu, tuwaruhusu waishi katika nchi yetu na kufanya biashara ndani yake, nchi ina nafasi tele kwa ajili yao. Tunaweza kuoa binti zao. Nao wanaweza kuoa binti zetu. 2234:22 Mwa 34:15Lakini watu hao watakuwa tayari kukubali kuishi nasi kama watu wamoja nao kwa sharti kwamba wanaume wetu watahiriwe, kama wao. 2334:23 Mwa 34:28Je, si mifugo yao, mali zao na wanyama wao wengine wote watakuwa wetu? Basi na tuwape kibali, nao wataishi miongoni mwetu.”

2434:24 Mwa 18:1Wanaume wote waliotoka nje ya lango la mji walikubaliana na Hamori na Shekemu mwanawe na kila mwanaume katika mji ule akatahiriwa.

2534:25 Mwa 49:5; 49:7Baada ya siku tatu, wakati wote wakiwa wangali katika maumivu, wana wawili wa Yakobo, yaani Simeoni na Lawi, ndugu zake Dina, wakachukua panga zao na kuvamia mji ambao haukutazamia vita, wakaua kila mwanaume. 26Wakawaua Hamori na Shekemu mwanawe kwa upanga kisha wakamchukua Dina kutoka nyumba ya Shekemu na kuondoka. 27Wana wa Yakobo walipita juu ya maiti katika kuteka nyara mji ule ambamo dada yao alikuwa amenajisiwa. 28Wakachukua kondoo na mbuzi, ngʼombe, punda na kila kitu kilichokuwa chao ndani ya mji ule na mashambani. 29Walichukua utajiri wao wote pamoja na wanawake na watoto wao, wakachukua nyara kila kitu ndani ya nyumba zao.

30Kisha Yakobo akawaambia Simeoni na Lawi, “Mmeleta taabu kwangu kwa kunifanya ninuke kama uvundo kwa Wakanaani na Waperizi, watu waishio katika nchi hii. Sisi ni wachache, kama wakiunganisha nguvu zao dhidi yangu na kunishambulia, mimi na nyumba yangu tutaangamizwa.”

31Lakini wakamjibu, “Je, ilikuwa vyema kumtendea dada yetu kama kahaba?”

New International Version – UK

Genesis 34:1-31

Dinah and the Shechemites

1Now Dinah, the daughter Leah had borne to Jacob, went out to visit the women of the land. 2When Shechem son of Hamor the Hivite, the ruler of that area, saw her, he took her and raped her. 3His heart was drawn to Dinah daughter of Jacob; he loved the young woman and spoke tenderly to her. 4And Shechem said to his father Hamor, ‘Get me this girl as my wife.’

5When Jacob heard that his daughter Dinah had been defiled, his sons were in the fields with his livestock; so he did nothing about it until they came home.

6Then Shechem’s father Hamor went out to talk with Jacob. 7Meanwhile, Jacob’s sons had come in from the fields as soon as they heard what had happened. They were shocked and furious, because Shechem had done an outrageous thing in34:7 Or against Israel by sleeping with Jacob’s daughter – a thing that should not be done.

8But Hamor said to them, ‘My son Shechem has his heart set on your daughter. Please give her to him as his wife. 9Intermarry with us; give us your daughters and take our daughters for yourselves. 10You can settle among us; the land is open to you. Live in it, trade34:10 Or move about freely; also in verse 21 in it, and acquire property in it.’

11Then Shechem said to Dinah’s father and brothers, ‘Let me find favour in your eyes, and I will give you whatever you ask. 12Make the price for the bride and the gift I am to bring as great as you like, and I’ll pay whatever you ask me. Only give me the young woman as my wife.’

13Because their sister Dinah had been defiled, Jacob’s sons replied deceitfully as they spoke to Shechem and his father Hamor. 14They said to them, ‘We can’t do such a thing; we can’t give our sister to a man who is not circumcised. That would be a disgrace to us. 15We will enter into an agreement with you on one condition only: that you become like us by circumcising all your males. 16Then we will give you our daughters and take your daughters for ourselves. We’ll settle among you and become one people with you. 17But if you will not agree to be circumcised, we’ll take our sister and go.’

18Their proposal seemed good to Hamor and his son Shechem. 19The young man, who was the most honoured of all his father’s family, lost no time in doing what they said, because he was delighted with Jacob’s daughter. 20So Hamor and his son Shechem went to the gate of their city to speak to the men of their city. 21‘These men are friendly towards us,’ they said. ‘Let them live in our land and trade in it; the land has plenty of room for them. We can marry their daughters and they can marry ours. 22But the men will agree to live with us as one people only on the condition that our males be circumcised, as they themselves are. 23Won’t their livestock, their property and all their other animals become ours? So let us agree to their terms, and they will settle among us.’

24All the men who went out of the city gate agreed with Hamor and his son Shechem, and every male in the city was circumcised.

25Three days later, while all of them were still in pain, two of Jacob’s sons, Simeon and Levi, Dinah’s brothers, took their swords and attacked the unsuspecting city, killing every male. 26They put Hamor and his son Shechem to the sword and took Dinah from Shechem’s house and left. 27The sons of Jacob came upon the dead bodies and looted the city where34:27 Or because their sister had been defiled. 28They seized their flocks and herds and donkeys and everything else of theirs in the city and out in the fields. 29They carried off all their wealth and all their women and children, taking as plunder everything in the houses.

30Then Jacob said to Simeon and Levi, ‘You have brought trouble on me by making me obnoxious to the Canaanites and Perizzites, the people living in this land. We are few in number, and if they join forces against me and attack me, I and my household will be destroyed.’

31But they replied, ‘Should he have treated our sister like a prostitute?’