Mwanzo 34 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 34:1-31

Dina Na Washekemu

134:1 Mwa 30:21Basi Dina, binti wa Yakobo aliyezaliwa na Lea, akatoka nje kuwatembelea wanawake wa nchi ile. 234:2 Mwa 33:19Ikawa Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mtawala wa eneo lile alipomwona, akamchukua na kumnajisi. 3Moyo wake ukavutwa sana kwa Dina binti Yakobo, akampenda huyu msichana na akazungumza naye kwa kumbembeleza. 434:4 Mwa 21:21Shekemu akamwambia baba yake Hamori, “Nipatie msichana huyu awe mke wangu.”

534:5 Mwa 34:2-3Yakobo aliposikia kwamba binti yake Dina amenajisiwa, wanawe walikuwa mashambani wakichunga mifugo yake, kwa hiyo akalinyamazia jambo hilo mpaka waliporudi nyumbani.

634:6 Amu 14:2-5Kisha Hamori baba yake Shekemu akaenda kuzungumza na Yakobo. 734:7 Kum 22:21; Amu 20:6Basi wana wa Yakobo walikuwa wamerudi kutoka mashambani mara tu waliposikia kilichotokea. Walikuwa wamejawa na huzuni na ghadhabu, kwa sababu Shekemu alikuwa amefanya jambo la aibu katika Israeli kwa kukutana kimwili na binti wa Yakobo, kitu ambacho hakingepasa kufanyika.

834:8 Mwa 21:21Lakini Hamori akawaambia, “Moyo wa mwanangu Shekemu umeelekea kwa binti yenu. Tafadhali mpeni awe mke wake. 934:9 Kum 7:3Oaneni na sisi, tupeni binti zenu, nanyi mchukue binti zetu. 1034:10 Mwa 47:6, 27; 13:9Mwaweza kuishi katikati yetu, nchi ni wazi kwenu. Ishini ndani yake, fanyeni biashara humu na mjipatie mali.”

1134:11 Mwa 32:5Kisha Shekemu akamwambia baba yake Dina pamoja na ndugu zake, “Na nipate kibali machoni penu, nami nitawapa chochote mtakachosema. 1234:12 Kum 22:29; 1Sam 18:25Niambieni kiasi cha mahari na zawadi nitakayoileta, hata iwe kubwa kiasi gani, nami nitawalipa chochote mtakachodai. Nipeni tu huyu msichana awe mke wangu.”

1334:13 Mwa 27:36Kwa sababu ndugu yao Dina alikuwa amenajisiwa, wana wa Yakobo wakajibu kwa udanganyifu walipozungumza na Shekemu pamoja na baba yake Hamori. 1434:14 Mwa 17:14; Isa 31:4Wakawaambia, “Hatuwezi kufanya jambo kama hili, hatuwezi kumtoa dada yetu kwa mtu ambaye hakutahiriwa. Hiyo itakuwa aibu kwetu. 1534:15 1Sam 11:2; Kut 12:48Tutakuruhusu kwa sharti moja tu, kwamba mtakuwa kama sisi kwa kuwatahiri wanaume wenu wote. 1634:16 Mwa 33:19Kisha tutawapa binti zetu na sisi tutawachukua binti zenu. Tutaishi kwenu na tutakuwa watu wamoja nanyi. 17Lakini mkikataa kutahiriwa, tutamchukua ndugu yetu na kuondoka.”

18Pendekezo lao likawa jema kwa Hamori na Shekemu mwanawe. 19Kijana mdogo, ambaye alikuwa ameheshimiwa kati ya wote walioishi nyumbani mwa baba yake, hakupoteza muda kufanya waliyoyasema, kwa sababu alikuwa amependezwa sana na binti Yakobo. 2034:20 Mwa 18:1Kwa hiyo Hamori na Shekemu mwanawe walikwenda kwenye lango la mji kuzungumza na wenzao wa mjini. 2134:21 Mwa 33:19Wakasema, “Hawa watu ni marafiki kwetu, tuwaruhusu waishi katika nchi yetu na kufanya biashara ndani yake, nchi ina nafasi tele kwa ajili yao. Tunaweza kuoa binti zao. Nao wanaweza kuoa binti zetu. 2234:22 Mwa 34:15Lakini watu hao watakuwa tayari kukubali kuishi nasi kama watu wamoja nao kwa sharti kwamba wanaume wetu watahiriwe, kama wao. 2334:23 Mwa 34:28Je, si mifugo yao, mali zao na wanyama wao wengine wote watakuwa wetu? Basi na tuwape kibali, nao wataishi miongoni mwetu.”

2434:24 Mwa 18:1Wanaume wote waliotoka nje ya lango la mji walikubaliana na Hamori na Shekemu mwanawe na kila mwanaume katika mji ule akatahiriwa.

2534:25 Mwa 49:5; 49:7Baada ya siku tatu, wakati wote wakiwa wangali katika maumivu, wana wawili wa Yakobo, yaani Simeoni na Lawi, ndugu zake Dina, wakachukua panga zao na kuvamia mji ambao haukutazamia vita, wakaua kila mwanaume. 26Wakawaua Hamori na Shekemu mwanawe kwa upanga kisha wakamchukua Dina kutoka nyumba ya Shekemu na kuondoka. 27Wana wa Yakobo walipita juu ya maiti katika kuteka nyara mji ule ambamo dada yao alikuwa amenajisiwa. 28Wakachukua kondoo na mbuzi, ngʼombe, punda na kila kitu kilichokuwa chao ndani ya mji ule na mashambani. 29Walichukua utajiri wao wote pamoja na wanawake na watoto wao, wakachukua nyara kila kitu ndani ya nyumba zao.

30Kisha Yakobo akawaambia Simeoni na Lawi, “Mmeleta taabu kwangu kwa kunifanya ninuke kama uvundo kwa Wakanaani na Waperizi, watu waishio katika nchi hii. Sisi ni wachache, kama wakiunganisha nguvu zao dhidi yangu na kunishambulia, mimi na nyumba yangu tutaangamizwa.”

31Lakini wakamjibu, “Je, ilikuwa vyema kumtendea dada yetu kama kahaba?”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

创世记 34:1-31

底娜受辱

1一天,利亚雅各所生的女儿底娜到外面去见当地的女子。 2当地首领希未哈抹的儿子示剑看到她,就抓住她,强行玷污了她。 3他恋慕雅各的女儿底娜,就用甜言蜜语讨她欢心。 4他求父亲哈抹为他说亲,把底娜娶过来。 5消息传到雅各耳中时,他的儿子们正在田野放牧。他只好忍气吞声,等儿子们回来再作打算。 6示剑的父亲哈抹来和雅各商议。 7雅各的儿子们一听说这事,就从田野赶回来。大家都非常愤怒,因为示剑不该对以色列家做这丑事——玷污雅各的女儿。

8哈抹跟他们商议说:“我儿子示剑爱慕你们家的女儿,请你们把女儿嫁给他吧! 9我们可以互相通婚,你们可以把女儿嫁给我们的儿子,也可以娶我们的女儿为妻。 10你们可以在我们这里安顿下来,这片土地就在你们面前,住在这里做买卖、置产业吧。” 11示剑底娜的父亲和她的弟兄们说:“请你们恩待我,你们要什么,我都给你们。 12只要你们答应把女儿嫁给我,无论你们要多少聘金和礼物,我必如数奉上。”

雅各之子计杀示剑人

13雅各的儿子们因为示剑玷污了他们的妹妹底娜,就假意对示剑和他的父亲哈抹说: 14“我们不能把妹妹嫁给没有受过割礼的人,这对我们是一种羞辱。 15除非你们所有的男子都跟我们一样受割礼, 16我们才能答应和你们通婚,共同生活,结成一个民族。 17如果你们不肯这样做,我们就把妹妹带走。”

18哈抹父子欣然答应。 19示剑毫不迟延地照办,因为他热恋底娜。在哈抹家族中,他最受人尊重。 20哈抹父子来到城门口,对那城的居民说: 21“这些人跟我们相处和睦,就让他们在这里定居、做买卖吧。我们这里有足够的地方可以容纳他们,我们可以和他们通婚。 22可是,他们有一个条件,就是要我们所有的男子和他们一样接受割礼,他们才答应和我们一起生活,结成一个民族。 23到时候,他们的财产和牛羊等所有牲畜不全归我们了吗?我们同意他们吧,这样他们就会在我们这里定居。” 24在城门进出的人听了哈抹父子的话,都表示赞同。于是,城里的男子都接受了割礼。

25到了第三天,他们伤口正疼痛的时候,雅各的两个儿子——底娜的哥哥西缅利未拿着利剑,乘众人没有防备,潜入城中,杀掉了所有的男子, 26包括哈抹示剑,从示剑家里带走了底娜27雅各的儿子又到城里掳掠,因为他们的妹妹在那里被人玷污。 28他们抢走牛群、羊群、驴群和城里城外所有的东西, 29并带走所有财物、妇孺以及房屋里的一切。 30雅各责备西缅利未说:“你们为什么要给我惹麻烦,使我在当地的迦南人和比利洗人中留下臭名呢?我们人数很少,要是他们联手来攻击我们,我们全家必遭灭门之祸。” 31他们说:“他怎么能把我们的妹妹当妓女对待?”