Mwanzo 31 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 31:1-55

Yakobo Akimbia Kutoka Kwa Labani

1Yakobo akawasikia wana wa Labani wakisema, “Yakobo amechukua kila kitu kilichokuwa cha baba yetu naye amepata utajiri huu wote kutokana na vile vilivyokuwa mali ya baba yetu.” 2Yakobo akatambua kwamba moyo wa Labani kwake haukuwa kama ulivyokuwa mwanzo.

331:3 Mwa 32:9; 21:22Ndipo Bwana akamwambia Yakobo, “Rudi katika nchi ya baba zako na kwa watu wako, nami nitakuwa pamoja nawe.”

4Hivyo Yakobo akatuma ujumbe kwa Raheli na Lea waje machungani yalikokuwa makundi yake. 531:5 Mwa 21:22; 26:3Akawaambia, “Naona moyo wa baba yenu kwangu sivyo kama ulivyokuwa mwanzoni, lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami. 631:6 Mwa 30:29Mnajua kwamba nimemtumikia baba yenu kwa nguvu zangu zote, 731:7 Mwa 31:41hata hivyo baba yenu amenidanganya kwa kubadilisha ujira wangu mara kumi. Hata hivyo, Mungu hakumruhusu kunidhuru. 831:8 Mwa 30:32Kama alisema, ‘Wenye madoadoa watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye madoadoa, kama alisema, ‘Wenye mistari watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye mistari. 9Hivyo Mungu amechukua mifugo ya baba yenu na amenipa mimi.

10“Wakati fulani majira ya kuzaliana niliota ndoto ambayo niliinua macho na kuona kwamba wale mabeberu waliokuwa wakipanda kundi walikuwa wa mistari, madoadoa na mabakabaka. 11Malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, ‘Yakobo.’ Nikamjibu, ‘Mimi hapa.’ 1231:12 Kut 3:7Akasema, ‘Inua macho yako uone wale mabeberu wote wanaopanda kundi wana mistari, madoadoa au mabakabaka, kwa maana nimeona yale yote ambayo Labani amekuwa akikutendea. 1331:13 Mwa 28:10-22Mimi ndiye Mungu wa Betheli, ulikomiminia ile nguzo mafuta na pale mahali uliponiwekea nadhiri. Sasa ondoka katika nchi hii mara moja urudi katika nchi uliyozaliwa.’ ”

14Ndipo Raheli na Lea wakajibu, “Je bado tu tunalo fungu lolote katika urithi wa nyumba ya baba yetu? 1531:15 Mwa 29:20Je, yeye hatuhesabu sisi kama wageni? Sio kwamba ametuuza tu, bali ametumia hata na vile vilivyolipwa kwa ajili yetu. 16Hakika utajiri wote ambao Mungu ameuchukua kutoka kwa baba yetu ni mali yetu na watoto wetu. Hivyo fanya lolote lile Mungu alilokuambia.”

17Ndipo Yakobo akawapandisha watoto wake na wake zake juu ya ngamia, 1831:18 Mwa 35:27naye akawaswaga wanyama wote mbele yake pamoja na vitu vyote alivyokuwa amechuma huko Padan-Aramu kwenda kwa baba yake Isaki katika nchi ya Kanaani.

1931:19 Amu 17:5; Hos 3:4Labani alipokuwa amekwenda kukata kondoo wake manyoya, Raheli aliiba miungu ya nyumba ya baba yake. 2031:20 Mwa 27:36Zaidi ya hayo, Yakobo alimdanganya Labani Mwaramu kwa kutokumwambia kwamba anakimbia. 2131:21 Kut 2:15Hivyo akakimbia pamoja na vitu vyote alivyokuwa navyo na kuvuka Mto Frati akaelekea nchi ya vilima katika Gileadi.

Labani Amfuatilia Yakobo

2231:22 Mwa 30:36Siku ya tatu Labani akaambiwa kwamba Yakobo amekimbia. 2331:23 Kut 14:9Akiwachukua jamaa zake, akamfuatia Yakobo kwa siku saba na kumkuta kwenye nchi ya vilima katika Gileadi. 2431:24 Mwa 20:3; 24:50Ndipo Mungu akamjia Labani Mwaramu katika ndoto usiku na kumwambia, “Jihadhari usiseme neno lolote kwa Yakobo, liwe zuri au baya.”

2531:25 Mwa 31:21Yakobo alikuwa amepiga hema lake katika nchi ya vilima katika Gileadi wakati Labani alipomkuta, Labani na jamaa yake wakapiga kambi huko pia. 2631:26 1Sam 30:23Ndipo Labani akamwambia Yakobo, “Umefanya nini? Umenidanganya na umewachukua binti zangu kama mateka katika vita. 2731:27 Mwa 31:20Kwa nini ulikimbia kwa siri na kunidanganya? Kwa nini hukuniambia ili nikuage kwa furaha na nyimbo za matari na vinubi? 2831:28 Mwa 27:27Hata hukuniruhusu niwabusu wajukuu zangu na kuwaaga binti zangu. Umefanya kitu cha kipumbavu. 29Nina uwezo wa kukudhuru, lakini usiku uliopita Mungu wa baba yako alisema nami, akaniambia, ‘Jihadhari, usiseme neno lolote kwa Yakobo liwe zuri au baya.’ 3031:30 Mwa 31:19Sasa umeondoka kwa sababu umetamani kurudi nyumbani kwa baba yako. Lakini kwa nini umeiba miungu yangu?”

31Yakobo akamjibu Labani, “Niliogopa, kwa sababu nilifikiri ungeweza kuninyangʼanya binti zako kwa nguvu. 3231:32 Mwa 44:9Lakini kama ukimkuta yeyote aliye na miungu yako, hataishi. Mbele ya jamaa yetu, angalia mwenyewe uone kama kuna chochote chako hapa nilicho nacho, kama kipo, kichukue.” Basi Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameiba hiyo miungu.

33Kwa hiyo Labani akaingia ndani ya hema la Yakobo na ndani ya hema la Lea na ndani ya hema la watumishi wawili wa kike, lakini hakukuta chochote. Baadaye alipotoka katika hema la Lea, akaingia hema la Raheli. 34Basi Raheli ndiye alikuwa amechukua ile miungu ya nyumbani kwao na kuiweka katika matandiko ya ngamia na kukalia. Labani akatafuta kila mahali kwenye hema lakini hakupata chochote.

3531:35 Law 19:3, 32Raheli akamwambia baba yake, “Usikasirike, bwana wangu kwa kuwa siwezi kusimama ukiwepo, niko katika hedhi.” Labani akatafuta lakini hakuweza kuipata miungu ya nyumbani kwake.

36Yakobo akakasirika na kumshutumu Labani, akisema, “Uhalifu wangu ni nini?” Akamuuliza Labani, “Ni dhambi gani niliyofanya hata unaniwinda? 3731:37 Mwa 31:23Sasa kwa kuwa umepekua vitu vyangu vyote umepata nini kilicho cha nyumbani mwako? Kiweke hapa mbele ya jamaa yako na yangu, nao waamue kati yetu sisi wawili.

38“Mpaka sasa nimekuwa pamoja nawe miaka ishirini. Kondoo wako na mbuzi wako hawajaharibu mimba, wala sijala kondoo dume kutoka makundi yako. 3931:39 Kut 22:13Sikukuletea mfugo aliyeraruliwa na wanyama pori, nilibeba hasara mimi mwenyewe. Tena ulinidai malipo kwa chochote kilichoibwa mchana au usiku. 40Hii ndiyo iliyokuwa hali yangu: Niliumia kwa joto la mchana na baridi usiku, pia usingizi ulinipa. 4131:41 Mwa 29:30; 31:7Ilikuwa hivi kwa miaka ile ishirini niliyokuwa nyumbani kwako. Nilikutumikia miaka ile kumi na minne kwa ajili ya binti zako wawili, miaka sita kwa ajili ya makundi yako, nawe ulibadilisha ujira wangu mara kumi. 4231:42 Mwa 31:53Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Abrahamu na Hofu ya Isaki, hakuwa pamoja nami, hakika ungenifukuza mikono mitupu. Lakini Mungu ameona taabu yangu na kazi ngumu ya mikono yangu, naye usiku uliopita amekukemea.”

43Labani akamjibu Yakobo, “Wanawake hawa ni binti zangu, watoto hawa ni watoto wangu na makundi haya ni makundi yangu. Vyote unavyoviona ni vyangu. Lakini hata hivyo ninaweza kufanya nini kuhusu hawa binti zangu, au kuhusu watoto waliowazaa? 4431:44 Mwa 21:27Njoo sasa na tufanye agano, wewe na mimi, na liwe kama shahidi kati yetu.”

4531:45 Mwa 28:18Hivyo Yakobo akachukua jiwe, akalisimamisha kama nguzo. 4631:46 Mwa 31:48, 52Akawaambia jamaa yake, “Kusanyeni mawe.” Hivyo wakachukua mawe na kuyakusanya yakawa lundo, wakala chakula hapo karibu na hilo lundo. 4731:47 Mwa 21:30Labani akaliita Yegar-Sahadutha31:47 Yegar-Sahadutha maana yake ni Lundo la ushahidi kwa Kiaramu. na Yakobo akaliita Galeedi.31:47 Galeedi maana yake ni Lundo la ushahidi kwa Kiebrania.

4831:48 Mwa 31:46Labani akasema, “Lundo hili ni shahidi kati yako na mimi leo.” Ndiyo maana likaitwa Galeedi. 4931:49 Amu 11:29Pia liliitwa Mispa,31:49 Mispa maana yake Mnara wa ulinzi. kwa sababu alisema, “Bwana na aweke ulinzi kati yako na mimi wakati kila mmoja akiwa mbali na mwingine. 5031:50 Yer 29:23; 42:5Kama ukiwatenda mabaya binti zangu au ukioa wake wengine zaidi ya binti zangu, hata ingawa hakuna hata mmoja aliye pamoja nasi, kumbuka kwamba Mungu ni shahidi kati yako na mimi.”

5131:51 Mwa 28:18Pia Labani akamwambia Yakobo, “Hili ndilo lundo, na hii ndiyo nguzo niliyoisimamisha kati yako na mimi. 5231:52 Mwa 21:30Lundo hili ni shahidi na nguzo hii ni shahidi, kwamba sitavuka lundo hili kuja upande wako kukudhuru, nawe kwamba hutavuka lundo hili na nguzo hii kuja upande wangu kunidhuru. 5331:53 Mwa 16:5; 31:42Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Nahori, Mungu wa baba zao, aamue kati yetu.”

Hivyo Yakobo akaapa kwa jina la Hofu ya baba yake Isaki. 54Yakobo akatoa dhabihu juu ya kilima na akawaalika jamaa zake kula chakula. Baada ya kula, wakalala huko.

55Kesho yake asubuhi na mapema, Labani akawabusu wajukuu zake, binti zake na kuwabariki. Kisha akaondoka, akarudi nyumbani.

La Bible du Semeur

Genèse 31:1-54

Le départ de Jacob

1Jacob apprit que les fils de Laban disaient : Jacob s’est emparé de tout ce qui appartenait à notre père et c’est avec le bien de notre père qu’il s’est acquis toute cette richesse.

2Il remarqua que l’attitude de Laban envers lui n’était plus comme avant. 3L’Eternel lui dit : Retourne au pays de tes pères, auprès de ta parenté, et je serai avec toi.

4Alors Jacob fit venir Rachel et Léa aux champs où il était avec ses troupeaux 5et il leur dit : Je vois que votre père n’a plus envers moi la même attitude qu’auparavant. Mais le Dieu de mon père a été avec moi. 6Vous savez vous-mêmes que j’ai servi votre père de toutes mes forces, 7tandis que lui m’a trompé : par dix fois, il a changé les conditions de mon salaire. Heureusement, Dieu ne lui a pas permis de me causer du tort. 8Quand votre père affirmait : « Les bêtes tachetées constitueront ton salaire », toutes les bêtes mettaient bas des petits tachetés. Et quand il affirmait : « Les mouchetés seront ton salaire », toutes les bêtes faisaient des petits mouchetés. 9Ainsi, c’est Dieu qui a pris le bétail de votre père et qui me l’a donné. 10En effet, à l’époque où les bêtes s’accouplent, j’ai vu en songe que les boucs qui couvraient les brebis étaient mouchetés, tachetés, ou marquetés. 11L’ange de Dieu m’appela dans ce rêve : « Jacob ! » Et j’ai répondu : « J’écoute. » 12« Lève les yeux, dit-il, et regarde : tous les boucs qui couvrent le troupeau sont mouchetés, tachetés, ou marquetés, car j’ai vu tout ce que te fait Laban. 13Je suis le Dieu de Béthel, où tu as répandu de l’huile sur une pierre dressée en stèle, et où tu m’as fait un vœu. Maintenant, lève-toi, quitte ce pays et retourne dans ton pays natal. »

14Rachel et Léa lui répondirent : Avons-nous encore quelque chose, ou un héritage, chez notre père ? 15Ne nous a-t-il pas traitées comme des étrangères puisqu’il nous a vendues ? Et, de plus, il a mangé notre argent31.15 Normalement, le père donnait à ses filles la dot qu’il recevait de ses gendres, alors que Laban seul a profité du travail de Jacob remplaçant la dot.. 16Tous les biens que Dieu a sauvés de notre père nous appartiennent, à nous et à nos enfants. Maintenant, donc, fais tout ce que Dieu t’a demandé.

17Alors Jacob se mit en route : il fit monter ses enfants et ses femmes sur les chameaux ; 18il emmena tout son bétail et tous les biens qu’il avait acquis, en particulier, le cheptel qu’il avait amassé pendant son séjour à Paddân-Aram, pour rentrer chez son père Isaac au pays de Canaan. 19Quant à Laban, il était parti tondre ses moutons. En partant, Rachel vola les idoles domestiques31.19 Litt. « les théraphim », petites statuettes à figures humaines. de son père. 20Ainsi Jacob partit à la dérobée sans informer Laban l’Araméen de sa fuite. 21Il s’enfuit avec tout ce qui lui appartenait, il traversa l’Euphrate, puis se dirigea vers les monts de Galaad.

Jacob rejoint par Laban

22Le troisième jour, on avertit Laban que Jacob s’était enfui. 23Il prit avec lui des hommes de sa famille, le poursuivit pendant sept jours et le rattrapa dans les monts de Galaad. 24Mais, pendant la nuit, Dieu vint parler à Laban l’Araméen dans un rêve. Il lui dit : Garde-toi de dire quoi que ce soit à Jacob, en bien ou en mal.

25Quand Laban atteignit Jacob, celui-ci avait dressé sa tente dans la montagne. Laban et ses hommes s’installèrent eux aussi dans les monts de Galaad. 26Laban interpella Jacob : Qu’est-ce qui t’a pris ? Pourquoi m’as-tu trompé ? Tu as emmené mes filles comme des captives de guerre ! 27Pourquoi t’es-tu enfui en cachette ? Tu es parti comme un voleur sans me prévenir ! Je t’aurais laissé partir dans la joie avec des chants, au son du tambourin et de la lyre. 28Tu ne m’as même pas laissé embrasser mes petits-enfants et mes filles ! Vraiment, tu as agi de façon stupide ! 29Je pourrais vous faire du mal, mais le Dieu de votre père m’a parlé la nuit dernière et m’a dit : « Garde-toi de ne rien dire à Jacob ni en bien ni en mal. » 30Maintenant, si tu es parti parce que tu languissais après la maison de ton père, pourquoi m’as-tu volé mes dieux ?

31Jacob répliqua : J’avais peur que tu m’enlèves tes filles. 32Quant à celui chez qui tu trouveras tes dieux, il ne vivra pas. Fouille en présence de nos gens ! Ce qui sera chez moi, reprends-le !

Jacob ignorait en effet que Rachel avait volé les idoles domestiques.

33Laban fouilla la tente de Jacob, celle de Léa, puis celle des deux servantes, et ne trouva rien. En sortant de la tente de Léa, il entra dans celle de Rachel. 34Or Rachel avait pris les idoles et les avait cachées dans la selle du chameau et s’était assise dessus. Laban fouilla toute la tente sans rien trouver. 35Elle dit à son père : Que mon seigneur ne se fâche pas si je ne peux pas me lever devant toi car j’ai ce qui arrive habituellement aux femmes.

Il fouilla, mais ne trouva pas les idoles. 36Alors Jacob se mit en colère et fit de violents reproches à Laban : Quelle faute ai-je commise, s’écria-t-il, qu’ai-je fait de mal pour que tu t’acharnes ainsi contre moi ? 37Tu as fouillé toutes mes affaires. As-tu rien trouvé qui t’appartienne ? Produis-le ici en présence de mes gens et des tiens, et qu’ils servent d’arbitres entre nous deux. 38Voilà vingt années que je suis chez toi ; tes brebis et tes chèvres n’ont pas avorté, et je n’ai jamais mangé les béliers de ton troupeau. 39Si une bête se faisait déchirer par une bête sauvage, je ne te la rapportais pas31.39 Si le berger rapportait au propriétaire les restes d’un mouton emporté par un fauve, il n’avait pas besoin de le restituer (voir Ex 22.12 ; Am 3.12). : c’est moi qui t’en dédommageais. Tu me réclamais ce qu’on m’avait volé de jour et ce qui m’avait été volé la nuit. 40Le jour, j’étais dévoré par la chaleur ; la nuit, par le froid, et je ne pouvais pas dormir. 41Voilà vingt ans que je suis chez toi : pendant quatorze ans, je t’ai servi pour tes deux filles, puis pendant six ans pour ton bétail ; dix fois, tu as changé mon salaire. 42Si le Dieu de mon père, le Dieu d’Abraham et celui que redoute Isaac, n’avait été de mon côté, tu m’aurais renvoyé aujourd’hui les mains vides. Mais Dieu a vu ma misère et avec quelle peine j’ai travaillé. La nuit dernière, il a prononcé son verdict.

Jacob fait alliance avec Laban

43– Ces filles sont mes filles, répondit Laban, ces fils mes fils, ces troupeaux sont miens et tout ce que tu vois est à moi. Et que puis-je faire aujourd’hui pour mes filles et pour les enfants qu’elles ont mis au monde ? 44Maintenant donc, viens, concluons une alliance, toi et moi, et laissons ici un signe qui nous serve de témoin à tous deux.

45Alors Jacob prit une pierre et l’érigea en stèle. 46Puis il dit aux siens : Ramassez des pierres !

Ils ramassèrent des pierres, les entassèrent et, tous ensemble, ils mangèrent31.46 Les alliances étaient souvent scellées par un repas (26.30 ; Ex 24.11). là sur ce tas de pierres. 47Laban le nomma Yegar-Sahadouta (Le tas de pierres du témoignage) et Jacob l’appela Galed (Le tas de pierres-témoin).

48Laban déclara : Ce tas de pierres sert aujourd’hui de témoin entre toi et moi.

C’est pourquoi on le nomma Galed. 49On l’appelle aussi Mitspa (Le lieu du guet), car Laban avait dit encore : Que l’Eternel fasse le guet entre nous deux quand nous nous serons perdus de vue l’un et l’autre. 50Si tu maltraites mes filles et si tu prends d’autres femmes en plus d’elles, ce n’est pas un homme qui nous servira d’arbitre, prends-y garde : c’est Dieu qui sera témoin entre moi et toi. 51Puis il ajouta : Vois ce tas de pierres et cette stèle que j’ai dressés entre moi et toi. 52Ce tas de pierres et cette stèle nous serviront de témoins. Je ne dois pas dépasser ce tas de pierres et cette stèle dans ta direction, et tu ne dois pas les dépasser dans ma direction avec de mauvaises intentions. 53Le Dieu d’Abraham et le dieu de Nahor31.53 Nahor était le frère d’Abraham (11.26) et le grand-père de Laban (24.24, 29). Laban était polythéiste. Jacob ne prêtera serment qu’au nom du Dieu d’Isaac (v. 42). – c’était le Dieu de leur père31.53 Les mots : le Dieu (ou les dieux) de leur père manquent dans certains manuscrits hébreux et dans la version grecque. – seront juges entre nous !

Jacob prêta serment par le Dieu que redoutait son père Isaac. 54Puis il offrit un sacrifice sur la montagne et invita sa parenté à un repas. Ils mangèrent ensemble et passèrent la nuit sur la montagne.