Mwanzo 3 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 3:1-24

Kuanguka Kwa Mwanadamu

13:1 Ay 1:7; 2:2; 2Kor 11:3; Ufu 12:9; 20:2; Mwa 2:17Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa porini ambao Bwana Mungu aliwafanya. Nyoka akamwambia mwanamke, “Ati kweli Mungu alisema, ‘Kamwe msile matunda ya mti wowote wa bustanini’?”

23:2 Mwa 2:16-17Mwanamke akamjibu nyoka, “Tunaweza kula matunda ya miti iliyoko bustanini, 3lakini Mungu alisema, ‘Kamwe msile tunda la mti ulio katikati ya bustani, wala kuugusa, la sivyo mtakufa.’ ”

43:4 Yn 8:44; 2Kor 11:3Lakini nyoka akamwambia mwanamke, “Hakika hamtakufa. 53:5 Mwa 1:26; 14:18-19; Za 7:8; Isa 14:14; Eze 28:2Kwa maana Mungu anajua ya kuwa wakati mtakapoyala, macho yenu yatafumbuliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”

63:6 Yak 1:14-15; 1Yn 2:16; Hes 30:7-8; Yer 44:15, 19, 24; 2Kor 11:3; 1Tim 2:14Mwanamke alipoona ya kuwa tunda la mti huo lilikuwa zuri kwa chakula na la kupendeza macho, tena linatamanika kwa kujipatia hekima, basi akachuma katika matunda yake, akala, pia akampa mumewe, aliyekuwa pamoja naye, naye akala. 73:7 Mwa 2:25Ndipo macho yao wote wawili yakafumbuliwa, wakajiona kwamba walikuwa uchi; hivyo wakashona majani ya mtini, wakajifunika.

83:8 Law 26:12; Kum 23:14; Ay 13:16; 23:7; 34:22-23; Isa 29:15; Za 139:7-12; Yer 16:17; 23:24; 49:10; Ufu 6:15-16Ndipo yule mwanaume na mkewe, waliposikia sauti ya Bwana Mungu alipokuwa akitembea bustanini jioni, wakajificha kutoka mbele za Bwana Mungu katikati ya miti ya bustani. 93:9 Mwa 4:9; 16:8; 18:9; 1Fal 19:9-13Lakini Bwana Mungu akamwita Adamu, “Uko wapi?”

103:10 Kut 19:16; 20:18; Kum 5:5; Mwa 2:25; 1Sam 12:18Naye akajibu, “Nilikusikia katika bustani nikaogopa kwa sababu nilikuwa uchi, hivyo nikajificha.”

113:11 Mwa 2:17, 25Mungu akamuuliza, “Ni nani aliyekuambia ya kuwa ulikuwa uchi? Je, umekula matunda ya mti niliokuamuru usile?”

123:12 Mwa 2:22Adamu akasema, “Huyu mwanamke uliyenipa awe pamoja nami alinipa sehemu ya tunda kutoka kwenye huo mti, nami nikala.”

133:13 Rum 7:11; 2Kor 11:3; 1Tim 2:14Ndipo Bwana Mungu akamuuliza mwanamke, “Ni nini hili ambalo umelifanya?” Mwanamke akajibu, “Nyoka alinidanganya, nami nikala.”

143:14 Za 72:9; Mik 7:17; Kum 28:15-20; Isa 49:23; 65:25Hivyo Bwana Mungu akamwambia nyoka, “Kwa kuwa umefanya hili,

“Umelaaniwa kuliko wanyama wote

wa kufugwa na wa porini!

Utatambaa kwa tumbo lako

na kula mavumbi

siku zote za maisha yako.

153:15 Yn 8:44; 1Yn 3:8; Mdo 13:10; Mwa 16:11; Amu 13:5; Ebr 2:14; Isa 7:14; 8:3; 9:6; Mt 1:23; Lk 1:31; Gal 4:4; Ufu 12:17; Rum 16:20Nami nitaweka uadui

kati yako na huyo mwanamke,

na kati ya uzao wako na wake,

yeye atakuponda kichwa,

nawe utamuuma kisigino.”

163:16 Za 48:5-6; Isa 13:8; 21:3; 26:17; Yer 4:31; 6:24; Mik 4:9; 1Kor 11:3; Efe 5:22; 1Tim 2:15Kwa mwanamke akasema,

“Nitakuzidishia sana utungu wakati wa kuzaa kwako;

kwa utungu utazaa watoto.

Tamaa yako itakuwa kwa mumeo

naye atakutawala.”

173:17 Mwa 2:17; 5:29; 6:13; 8:21; 47:9; 29:32; 31:42; Hes 35:33; Za 66:11; 106:39; 127:2; Isa 24:5; Rum 8:20-22; Isa 54:9; Kut 3:7; Mhu 1:13; 2:23; Ay 5:7; 14:1; Yer 20:18Kwa Adamu akasema, “Kwa sababu umemsikiliza mke wako na ukala kutoka kwenye mti niliokuamuru, ‘Msile tunda lake,’

“Ardhi imelaaniwa kwa sababu yako,

kwa kazi ngumu utakula chakula kitokacho humo

siku zote za maisha yako.

183:18 Za 104:14; Ay 31:40; Isa 5:6; Ebr 6:8Itazaa miiba na mibaruti kwa ajili yako,

nawe utakula mimea ya shambani.

193:19 Mwa 2:7; 14:18; Kum 8:3, 9; 23:4; Rum 1:6; 2:14; 2The 3:10; Ay 7:21; Ebr 9:27; Za 146:4; 104:23; Rut 1:6; 2:14; 1Kor 15:47Kwa jasho la uso wako

utakula chakula chako

hadi utakaporudi ardhini,

kwa kuwa ulitwaliwa kutoka humo,

kwa kuwa wewe u mavumbi

na mavumbini wewe utarudi.”

203:20 Mwa 2:20; 2Kor 11:3; 1Tim 2:13Adamu akamwita mkewe Eva, kwa kuwa atakuwa mama wa wote walio hai.

21Bwana Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika. 223:22 Mwa 2:9; 1:26; Ufu 2:7Kisha Bwana Mungu akasema, “Sasa mtu huyu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya. Sharti asiruhusiwe kunyoosha mkono wake na kuchuma pia kutoka mti wa uzima akala, naye akaishi milele.” 233:23 Mwa 2:7-8Hivyo Bwana Mungu akamfukuzia mbali kutoka Bustani ya Edeni, akalime ardhi ambamo alitolewa. 243:24 Kut 25:18-22; 1Sam 4:4; 2Sam 6:2; 22:11; 1Fal 6:27; 8:6; 2Fal 19:15; 2Nya 5:8; Za 18:10; 104:4; Isa 27:1; 37:16; Eze 10:1; Mwa 2:9; Ay 40:19Baada ya kumfukuzia mbali Adamu, Mungu akaweka makerubi mashariki ya Bustani ya Edeni, pamoja na upanga wa moto ukimulika huku na huko kulinda njia ya kuuendea mti wa uzima.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

创世记 3:1-24

始祖犯罪

1在耶和华上帝所造的田野的各种动物中,蛇最狡猾。蛇对女人说:“上帝真的说过不许你们吃园中所有树上的果子吗?” 2女人回答说:“我们可以吃园中树上的果子, 3只是不可以吃园子中间那棵树的果子。上帝曾经吩咐说,‘你们不可吃那果子,也不可摸,否则你们就会死。’” 4蛇对女人说:“你们一定不会死! 5上帝那样说是因为祂知道你们吃了那树的果子以后,眼睛就会明亮,像上帝一样懂得分辨善恶。” 6女人见那棵树上的果子可口,赏心悦目,可以使人有智慧,就摘下来吃了。她也把果子给跟她在一起的丈夫,他也吃了。 7二人的眼睛果然明亮起来,这才发觉自己原来赤身露体,便把无花果树的叶子编起来遮体。

8傍晚天凉时,夫妇二人听见耶和华上帝在园中行走的声音,就藏在园子的树丛中,想躲开耶和华上帝。 9耶和华上帝呼唤那人说:“你在哪里?” 10那人说:“我听见你在园中行走的声音,就害怕得躲了起来,因为我赤身露体!” 11耶和华上帝问:“谁说你赤身露体?难道你吃了我吩咐你不可吃的果子吗?” 12那人说:“你赐给我作伴的女人摘了那树上的果子给我,我就吃了。” 13耶和华上帝对女人说:“你这做的是什么事?”女人说:“是蛇诱骗我,我才吃的。”

上帝的审判

14耶和华上帝对蛇说:

“你既然做了这事,

你要比一切的牲畜和野兽受更重的咒诅,

你要用肚子爬行,

一生都要吃尘土。

15我要使你和女人结仇,

你的后代和女人的后代也要彼此为仇,

女人的后代必伤你的头,

你必伤他的脚跟。”

16耶和华上帝对女人说:

“我必大大加重你怀孕的痛苦,

你分娩时必受痛苦。

你必恋慕3:16 恋慕”或译“想控制”。自己的丈夫,

你的丈夫必管辖你。”

17耶和华上帝又对亚当说:

“因为你听从妻子的话,

吃了我吩咐你不可吃的果子,

地必因你而受咒诅。

你必终生艰辛劳苦,

才能吃到地里出产的食物。

18地必给你长出荆棘和蒺藜,

你要吃田间长出来的菜蔬。

19你必汗流满面,才有饭吃,

一直到你归回尘土。

因为你是尘土造的,

也必归回尘土。”

20亚当给他的妻子取名叫夏娃,因为她是众生之母。 21耶和华上帝做了皮衣给他们夫妇穿。 22耶和华上帝说:“看啊,那人已经与我们相似,能分辨善恶。现在,恐怕他会伸手去摘生命树的果子吃,那样他就会永远活着。” 23因此,耶和华上帝就把亚当赶出伊甸园,让他去开垦土地——他的本源。 24上帝赶走了亚当以后,就派遣基路伯天使驻守在伊甸园东边,又用一把旋转的火剑守护在通往生命树的路上。