Mwanzo 24 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 24:1-67

Isaki Na Rebeka

124:1 Mwa 17:17; Yos 23:1; Mwa 12:2; Gal 3:9Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia. 224:2 Mwa 15:3; 39:4-6; 47:29Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu, 324:3 Mwa 10:15-19; 47:31; 50:25; 14:19; Hes 20:14; 2Kor 6:14-17Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao, 424:4 Mwa 12:1; 21:21; Amu 14:3bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”

524:5 Ebr 11:15Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”

6Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko. 724:7 Mwa 12:1, 7; 16:7; Rum 4:15; Gal 3:16Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko. 824:8 Yos 2:12-20; 9:20Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.” 924:9 Mwa 32:4; 33:8Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.

1024:10 1Fal 10:2; 1Nya 12:40; Isa 30:6; Mwa 11:29; 43:11; 45:25; Hes 23:7; Kum 23:4; Amu 3:8Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu24:10 Yaani Mesopotamia ya Kaskazini-Magharibi. na kushika njia kwenda mji wa Nahori. 1124:11 Kut 2:15-16; 1Sam 9:11; Yn 4:7; Mwa 29:2, 9-10Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.

1224:12 Mwa 19:19; 26:24; 27:20; 28:13; 31:42, 53; 32:9; 43:23; 46:3; Kut 3:6; 1Fal 18:36; Za 75:9; 94:7; Neh 1:11; Yos 2:12; Ay 10:12Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu. 13Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji. 1424:14 Amu 6:17, 37; 1Sam 14:10; 1Fal 13:3; Za 86:17; Isa 38:7; Yer 44:29Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”

1524:15 Mwa 22:22-23; 11:29Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu. 1624:16 Mwa 12:11; Kum 22:15-21Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.

1724:17 1Fal 17:10; Yn 4:7Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”

18Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.

19Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.” 20Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote. 21Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.

2224:22 Mwa 41:42; Isa 3:21; Eze 16:11-12Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja24:22 Beka moja ya dhahabu ni sawa na gramu 5.5. na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.24:22 Shekeli 10 za dhahabu ni sawa na gramu 110. 2324:23 Amu 19:15; 20:4Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”

2424:24 Mwa 11:29Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.” 2524:25 Amu 19:19Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”

2624:26 Kut 4:31; 12:27; 1Nya 29:20; 2Nya 20:18Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana, 2724:27 Mwa 14:20; 32:10; 47:29; Kut 18:20; Rut 4:14; 1Sam 25:32; 2Sam 18:28; 1Fal 8:56; Za 28:6; 41:13; 68:19; 98:3; 106:48; Yos 2:14; Lk 1:68akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”

2824:28 Mwa 29:12Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya. 2924:29 Mwa 25:20; 27:43; 28:2-5; 29:5, 12-13Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani. 3024:30 Eze 23:42Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima. 3124:31 Mwa 26:29; Rut 3:10; Za 115:15Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”

3224:32 Mwa 18:4; Amu 19:21Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu. 33Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.”

Labani akasema, “Basi tuambie.”

3424:34 Mwa 15:3Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu. 3524:35 Mwa 12:2, 16; 23:6Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda. 3624:36 Mwa 17:17; 25:5; 26:14Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho. 3724:37 Mwa 50:5Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao, 3824:38 Mwa 21:21ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’

39“Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’

4024:40 Mwa 5:22; 12:1; 16:7“Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu. 41Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’

42“Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia. 4324:43 Mit 30:19; Isa 7:14Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako, 44naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’

4524:45 1Sam 1:13; Yn 4:7“Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’

46“Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.

4724:47 Mwa 22:22; Isa 3:19; Eze 16:11-12“Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’

“Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’

“Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake, 48nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake. 49Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”

5024:50 Za 118:23; Mwa 22:22; 31:24-29; 48:16Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema. 51Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”

52Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana. 5324:53 Mwa 45:22; Kut 3:22; 12:35; 2Fal 5:5Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye. 5424:54 Mwa 30:25Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale.

Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”

5524:55 Amu 19:3-4Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”

56Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”

57Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.” 5824:58 Rum 1:16Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?”

Akasema, “Nitakwenda.”

5924:59 Mwa 35:8Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake. 6024:60 Mwa 17:16; 22:17; 27:4; 31:55; 48:9, 15, 20; Yos 22:6; Mit 27:11Wakambariki Rebeka, wakamwambia,

“Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu,

mara elfu nyingi,

nao wazao wako wamiliki

malango ya adui zao.”

6124:61 Mwa 16:1; 30:3; 46:25Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.

6224:62 Mwa 16:14; 12:9Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu. 6324:63 Za 77:12; 119:15, 27; 143:5; 145:5; Mwa 18:2Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja. 6424:64 Mwa 31:17, 34; 1Sam 30:17Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake 6524:65 Mwa 38:14; Wim 4:1-3; 6:7; Isa 47:2na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?”

Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.

66Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda. 6724:67 Mwa 31:33; 18:9; 25:20; 49:31; 29:18-20; 23:1-2; 34:3; Amu 16:4Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.

King James Version

Genesis 24:1-67

1And Abraham was old, and well stricken in age: and the LORD had blessed Abraham in all things.24.1 well…: Heb. gone into days 2And Abraham said unto his eldest servant of his house, that ruled over all that he had, Put, I pray thee, thy hand under my thigh: 3And I will make thee swear by the LORD, the God of heaven, and the God of the earth, that thou shalt not take a wife unto my son of the daughters of the Canaanites, among whom I dwell: 4But thou shalt go unto my country, and to my kindred, and take a wife unto my son Isaac. 5And the servant said unto him, Peradventure the woman will not be willing to follow me unto this land: must I needs bring thy son again unto the land from whence thou camest? 6And Abraham said unto him, Beware thou that thou bring not my son thither again.

7¶ The LORD God of heaven, which took me from my father’s house, and from the land of my kindred, and which spake unto me, and that sware unto me, saying, Unto thy seed will I give this land; he shall send his angel before thee, and thou shalt take a wife unto my son from thence. 8And if the woman will not be willing to follow thee, then thou shalt be clear from this my oath: only bring not my son thither again. 9And the servant put his hand under the thigh of Abraham his master, and sware to him concerning that matter.

10¶ And the servant took ten camels of the camels of his master, and departed; for all the goods of his master were in his hand: and he arose, and went to Mesopotamia, unto the city of Nahor.24.10 for: or, and 11And he made his camels to kneel down without the city by a well of water at the time of the evening, even the time that women go out to draw water.24.11 that…: Heb. that women who draw water go forth 12And he said, O LORD God of my master Abraham, I pray thee, send me good speed this day, and shew kindness unto my master Abraham. 13Behold, I stand here by the well of water; and the daughters of the men of the city come out to draw water: 14And let it come to pass, that the damsel to whom I shall say, Let down thy pitcher, I pray thee, that I may drink; and she shall say, Drink, and I will give thy camels drink also: let the same be she that thou hast appointed for thy servant Isaac; and thereby shall I know that thou hast shewed kindness unto my master.

15¶ And it came to pass, before he had done speaking, that, behold, Rebekah came out, who was born to Bethuel, son of Milcah, the wife of Nahor, Abraham’s brother, with her pitcher upon her shoulder. 16And the damsel was very fair to look upon, a virgin, neither had any man known her: and she went down to the well, and filled her pitcher, and came up.24.16 very…: Heb. good of countenance 17And the servant ran to meet her, and said, Let me, I pray thee, drink a little water of thy pitcher. 18And she said, Drink, my lord: and she hasted, and let down her pitcher upon her hand, and gave him drink. 19And when she had done giving him drink, she said, I will draw water for thy camels also, until they have done drinking. 20And she hasted, and emptied her pitcher into the trough, and ran again unto the well to draw water, and drew for all his camels. 21And the man wondering at her held his peace, to wit whether the LORD had made his journey prosperous or not. 22And it came to pass, as the camels had done drinking, that the man took a golden earring of half a shekel weight, and two bracelets for her hands of ten shekels weight of gold;24.22 earring: or, jewel for the forehead 23And said, Whose daughter art thou? tell me, I pray thee: is there room in thy father’s house for us to lodge in? 24And she said unto him, I am the daughter of Bethuel the son of Milcah, which she bare unto Nahor. 25She said moreover unto him, We have both straw and provender enough, and room to lodge in. 26And the man bowed down his head, and worshipped the LORD. 27And he said, Blessed be the LORD God of my master Abraham, who hath not left destitute my master of his mercy and his truth: I being in the way, the LORD led me to the house of my master’s brethren. 28And the damsel ran, and told them of her mother’s house these things.

29¶ And Rebekah had a brother, and his name was Laban: and Laban ran out unto the man, unto the well. 30And it came to pass, when he saw the earring and bracelets upon his sister’s hands, and when he heard the words of Rebekah his sister, saying, Thus spake the man unto me; that he came unto the man; and, behold, he stood by the camels at the well. 31And he said, Come in, thou blessed of the LORD; wherefore standest thou without? for I have prepared the house, and room for the camels.

32¶ And the man came into the house: and he ungirded his camels, and gave straw and provender for the camels, and water to wash his feet, and the men’s feet that were with him. 33And there was set meat before him to eat: but he said, I will not eat, until I have told mine errand. And he said, Speak on. 34And he said, I am Abraham’s servant. 35And the LORD hath blessed my master greatly; and he is become great: and he hath given him flocks, and herds, and silver, and gold, and menservants, and maidservants, and camels, and asses. 36And Sarah my master’s wife bare a son to my master when she was old: and unto him hath he given all that he hath. 37And my master made me swear, saying, Thou shalt not take a wife to my son of the daughters of the Canaanites, in whose land I dwell: 38But thou shalt go unto my father’s house, and to my kindred, and take a wife unto my son. 39And I said unto my master, Peradventure the woman will not follow me. 40And he said unto me, The LORD, before whom I walk, will send his angel with thee, and prosper thy way; and thou shalt take a wife for my son of my kindred, and of my father’s house: 41Then shalt thou be clear from this my oath, when thou comest to my kindred; and if they give not thee one, thou shalt be clear from my oath. 42And I came this day unto the well, and said, O LORD God of my master Abraham, if now thou do prosper my way which I go: 43Behold, I stand by the well of water; and it shall come to pass, that when the virgin cometh forth to draw water, and I say to her, Give me, I pray thee, a little water of thy pitcher to drink; 44And she say to me, Both drink thou, and I will also draw for thy camels: let the same be the woman whom the LORD hath appointed out for my master’s son. 45And before I had done speaking in mine heart, behold, Rebekah came forth with her pitcher on her shoulder; and she went down unto the well, and drew water: and I said unto her, Let me drink, I pray thee. 46And she made haste, and let down her pitcher from her shoulder, and said, Drink, and I will give thy camels drink also: so I drank, and she made the camels drink also. 47And I asked her, and said, Whose daughter art thou? And she said, The daughter of Bethuel, Nahor’s son, whom Milcah bare unto him: and I put the earring upon her face, and the bracelets upon her hands. 48And I bowed down my head, and worshipped the LORD, and blessed the LORD God of my master Abraham, which had led me in the right way to take my master’s brother’s daughter unto his son. 49And now if ye will deal kindly and truly with my master, tell me: and if not, tell me; that I may turn to the right hand, or to the left. 50Then Laban and Bethuel answered and said, The thing proceedeth from the LORD: we cannot speak unto thee bad or good. 51Behold, Rebekah is before thee, take her, and go, and let her be thy master’s son’s wife, as the LORD hath spoken. 52And it came to pass, that, when Abraham’s servant heard their words, he worshipped the LORD, bowing himself to the earth. 53And the servant brought forth jewels of silver, and jewels of gold, and raiment, and gave them to Rebekah: he gave also to her brother and to her mother precious things.24.53 jewels: Heb. vessels

54And they did eat and drink, he and the men that were with him, and tarried all night; and they rose up in the morning, and he said, Send me away unto my master. 55And her brother and her mother said, Let the damsel abide with us a few days, at the least ten; after that she shall go.24.55 a few…: or, a full year, or ten months 56And he said unto them, Hinder me not, seeing the LORD hath prospered my way; send me away that I may go to my master. 57And they said, We will call the damsel, and enquire at her mouth. 58And they called Rebekah, and said unto her, Wilt thou go with this man? And she said, I will go. 59And they sent away Rebekah their sister, and her nurse, and Abraham’s servant, and his men. 60And they blessed Rebekah, and said unto her, Thou art our sister, be thou the mother of thousands of millions, and let thy seed possess the gate of those which hate them.

61¶ And Rebekah arose, and her damsels, and they rode upon the camels, and followed the man: and the servant took Rebekah, and went his way.

62And Isaac came from the way of the well Lahai-roi; for he dwelt in the south country. 63And Isaac went out to meditate in the field at the eventide: and he lifted up his eyes, and saw, and, behold, the camels were coming.24.63 to meditate: or, to pray 64And Rebekah lifted up her eyes, and when she saw Isaac, she lighted off the camel. 65For she had said unto the servant, What man is this that walketh in the field to meet us? And the servant had said, It is my master: therefore she took a vail, and covered herself. 66And the servant told Isaac all things that he had done. 67And Isaac brought her into his mother Sarah’s tent, and took Rebekah, and she became his wife; and he loved her: and Isaac was comforted after his mother’s death.