Mwanzo 22 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 22:1-24

Kujua Uthabiti Wa Abrahamu

122:1 Kut 15:25; 16:4; 20:20; Kum 8:2, 16; 13:3; Amu 2:22; 3:1; 2Nya 32:31; Za 66:10; Ebr 11:17; Yak 1:12-13; Mwa 31:11; 46:2; 1Sam 3:4-8; Isa 6:8Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!”

Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”

222:2 Yn 3:16; Ebr 11:17; 1Yn 4:9; Mwa 8:20Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”

322:3 Yos 8:10Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia. 4Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali. 522:5 Kut 24:14Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”

622:6 Yn 19:17; Amu 19:29Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja, 722:7 Kut 29:38-42; Law 1:10; Ufu 13:8Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!”

Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.”

Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”

822:8 Yn 1:29Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.

922:9 Mwa 4:26; 8:20; Law 1:7; 1Fal 18:33; Ebr 11:17-19; Yak 2:21Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni. 1022:10 Mwa 18:19Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe. 1122:11 Mwa 16:7; 21:17; 46:2Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!”

Akajibu, “Mimi hapa.”

1222:12 Mwa 18:19; 42:18; Kut 18:21; 1Sam 15:22; Ay 1:1; 37:24; Mit 8:13; Yak 2:21-23; Yn 3:16; 1Yn 4:9Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”

1322:13 Mwa 8:20; Rum 8:32Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe. 1422:14 Kut 17:15; Amu 6:24; Isa 30:29Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire.22:14 Yehova-Yire maana yake Bwana atatupa. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”

1522:15 Mwa 21:17Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili, 1622:16 Kut 13:11; 32:13; 33:1; Isa 45:23; 62:8; Yer 22:5; 44:26; 49:13; 51:14; Amo 6:8; Ebr 6:13; Lk 1:73akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee, 1722:17 Mwa 12:2; 15:5; 26:24; 24:60; Ebr 6:14; Kut 32:13; Kum 7:7; 28:62; Hos 1:10; Rum 9:27; Ebr 11:12; Es 9:2hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao, 1822:18 Mwa 12:2-3; 17:2, 9; Mdo 3:25; Gal 3:8; Za 105:9na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”

1922:19 Mwa 21:14; 26:23; 28:10Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.

Wana Wa Nahori

2022:20 Mwa 11:29Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana: 2122:21 Mwa 10:23; Ay 32:2; Yer 25:23Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu), 2222:22 Mwa 24:15, 47; 25:20Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.” 2322:23 Mwa 24:15; 11:29Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane. 2422:24 Mwa 25:6; 35:22; 36:12; Amu 8:31; 2Sam 3:7; 1Fal 2:22; 11:3; 1Nya 1:32; Wim 6:8Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.

New International Version

Genesis 22:1-24

Abraham Tested

1Some time later God tested Abraham. He said to him, “Abraham!”

“Here I am,” he replied.

2Then God said, “Take your son, your only son, whom you love—Isaac—and go to the region of Moriah. Sacrifice him there as a burnt offering on a mountain I will show you.”

3Early the next morning Abraham got up and loaded his donkey. He took with him two of his servants and his son Isaac. When he had cut enough wood for the burnt offering, he set out for the place God had told him about. 4On the third day Abraham looked up and saw the place in the distance. 5He said to his servants, “Stay here with the donkey while I and the boy go over there. We will worship and then we will come back to you.”

6Abraham took the wood for the burnt offering and placed it on his son Isaac, and he himself carried the fire and the knife. As the two of them went on together, 7Isaac spoke up and said to his father Abraham, “Father?”

“Yes, my son?” Abraham replied.

“The fire and wood are here,” Isaac said, “but where is the lamb for the burnt offering?”

8Abraham answered, “God himself will provide the lamb for the burnt offering, my son.” And the two of them went on together.

9When they reached the place God had told him about, Abraham built an altar there and arranged the wood on it. He bound his son Isaac and laid him on the altar, on top of the wood. 10Then he reached out his hand and took the knife to slay his son. 11But the angel of the Lord called out to him from heaven, “Abraham! Abraham!”

“Here I am,” he replied.

12“Do not lay a hand on the boy,” he said. “Do not do anything to him. Now I know that you fear God, because you have not withheld from me your son, your only son.”

13Abraham looked up and there in a thicket he saw a ram22:13 Many manuscripts of the Masoretic Text, Samaritan Pentateuch, Septuagint and Syriac; most manuscripts of the Masoretic Text a ram behind him caught by its horns. He went over and took the ram and sacrificed it as a burnt offering instead of his son. 14So Abraham called that place The Lord Will Provide. And to this day it is said, “On the mountain of the Lord it will be provided.”

15The angel of the Lord called to Abraham from heaven a second time 16and said, “I swear by myself, declares the Lord, that because you have done this and have not withheld your son, your only son, 17I will surely bless you and make your descendants as numerous as the stars in the sky and as the sand on the seashore. Your descendants will take possession of the cities of their enemies, 18and through your offspring22:18 Or seed all nations on earth will be blessed,22:18 Or and all nations on earth will use the name of your offspring in blessings (see 48:20) because you have obeyed me.”

19Then Abraham returned to his servants, and they set off together for Beersheba. And Abraham stayed in Beersheba.

Nahor’s Sons

20Some time later Abraham was told, “Milkah is also a mother; she has borne sons to your brother Nahor: 21Uz the firstborn, Buz his brother, Kemuel (the father of Aram), 22Kesed, Hazo, Pildash, Jidlaph and Bethuel.” 23Bethuel became the father of Rebekah. Milkah bore these eight sons to Abraham’s brother Nahor. 24His concubine, whose name was Reumah, also had sons: Tebah, Gaham, Tahash and Maakah.