Mwanzo 11 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 11:1-32

Mnara Wa Babeli

1Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja. 211:2 Mwa 10:10Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari11:2 Shinari ndio Babeli. nao wakaishi huko.

311:3 Kut 1:14; 5:7; Yer 43:9; Isa 9:10; Amo 5:11; Mwa 14:10Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali. 411:4 Kum 1:28; 6:10; 9:1; Ay 20:6; Yer 51:53; 31:10; 40:15; Mwa 6:4; 9:19; Kum 30:3; 4:27; 1Fal 22:17; Es 3:8; Za 44:11; Eze 6:8; Yoe 3:2Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”

511:5 Mwa 18:21; Kut 3:6-8; 19:11, 18-20; Za 18:9; 144:5Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga. 6Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao. 711:7 Mwa 1:26; 42:23; Kum 28:49; Isa 28:11; 33:19; Yer 5:15; 1Kor 2:11Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”

811:8 Mwa 9:19; Kum 32:8; Lk 1:51Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji. 911:9 Mwa 10:10; Za 55:9; Mdo 2:5-11; Isa 2:10, 21; 13:14; 24:1Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.

Shemu Hadi Abramu

(1 Nyakati 1:24-27)

1011:10 Mwa 2:4; Lk 3:36Hivi ndivyo vizazi vya Shemu.

Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi. 11Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

1211:12 Lk 3:35Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela. 13Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

14Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi. 15Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

16Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi. 17Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

18Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu. 19Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

2011:20 Lk 3:35Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi. 21Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

2211:22 Lk 3:34Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori. 23Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

2411:24 Lk 3:34Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera. 25Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

2611:26 Lk 3:34; Yos 24:2; 2Fal 19:12; Isa 37:12; Eze 27:23Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.

Wazao Wa Tera

2711:27 Mwa 2:4; 31:53; 12:4; 13:1-5, 8, 12; 14:12; 19:1; Lk 17:28; 2Pet 2:5-7Hawa ndio wazao wa Tera.

Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti. 2811:28 Mwa 15:7; Neh 9:7; Ay 1:17; 16:11; Eze 23:23; Mdo 7:4Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa. 2911:29 Mwa 22:20-23; 24:10-24; 29:5; 12:5; 16:1; 17:15Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani. 3011:30 Mwa 16:1; 18:11; 25:21; 29:31; 30:1, 22; Amu 13:2; 1Sam 1:5; Za 113:9Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.

3111:31 Mwa 38:11; 10:19; 12:4; 27:43; 28:5-10; 29:4; Law 18:15; 20:21; Rut 1:6, 22; 2:20; 4:15; 1Sam 4:19; 1Nya 2:4; Mik 7:6; Eze 22:11; 27:23; Mdo 7:4; 2Fal 19:12Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.

3211:32 Yos 24:2Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.

New International Version – UK

Genesis 11:1-32

The tower of Babel

1Now the whole world had one language and a common speech. 2As people moved eastward,11:2 Or from the east; or in the east they found a plain in Shinar11:2 That is, Babylonia and settled there.

3They said to each other, ‘Come, let’s make bricks and bake them thoroughly.’ They used brick instead of stone, and bitumen for mortar. 4Then they said, ‘Come, let us build ourselves a city, with a tower that reaches to the heavens, so that we may make a name for ourselves; otherwise we will be scattered over the face of the whole earth.’

5But the Lord came down to see the city and the tower the people were building. 6The Lord said, ‘If as one people speaking the same language they have begun to do this, then nothing they plan to do will be impossible for them. 7Come, let us go down and confuse their language so they will not understand each other.’

8So the Lord scattered them from there over all the earth, and they stopped building the city. 9That is why it was called Babel11:9 That is, Babylon; Babel sounds like the Hebrew for confused. – because there the Lord confused the language of the whole world. From there the Lord scattered them over the face of the whole earth.

From Shem to Abram

10This is the account of Shem’s family line.

Two years after the flood, when Shem was 100 years old, he became the father11:10 Father may mean ancestor; also in verses 11-25. of Arphaxad. 11And after he became the father of Arphaxad, Shem lived 500 years and had other sons and daughters.

12When Arphaxad had lived 35 years, he became the father of Shelah. 13And after he became the father of Shelah, Arphaxad lived 403 years and had other sons and daughters.11:12,13 Hebrew; Septuagint (see also Luke 3:35,36 and note at Gen. 10:24) 35 years, he became the father of Cainan. 13 And after he became the father of Cainan, Arphaxad lived 430 years and had other sons and daughters, and then he died. When Cainan had lived 130 years, he became the father of Shelah. And after he became the father of Shelah, Cainan lived 330 years and had other sons and daughters

14When Shelah had lived 30 years, he became the father of Eber. 15And after he became the father of Eber, Shelah lived 403 years and had other sons and daughters.

16When Eber had lived 34 years, he became the father of Peleg. 17And after he became the father of Peleg, Eber lived 430 years and had other sons and daughters.

18When Peleg had lived 30 years, he became the father of Reu. 19And after he became the father of Reu, Peleg lived 209 years and had other sons and daughters.

20When Reu had lived 32 years, he became the father of Serug. 21And after he became the father of Serug, Reu lived 207 years and had other sons and daughters.

22When Serug had lived 30 years, he became the father of Nahor. 23And after he became the father of Nahor, Serug lived 200 years and had other sons and daughters.

24When Nahor had lived 29 years, he became the father of Terah. 25And after he became the father of Terah, Nahor lived 119 years and had other sons and daughters.

26After Terah had lived 70 years, he became the father of Abram, Nahor and Haran.

Abram’s family

27This is the account of Terah’s family line.

Terah became the father of Abram, Nahor and Haran. And Haran became the father of Lot. 28While his father Terah was still alive, Haran died in Ur of the Chaldeans, in the land of his birth. 29Abram and Nahor both married. The name of Abram’s wife was Sarai, and the name of Nahor’s wife was Milkah; she was the daughter of Haran, the father of both Milkah and Iskah. 30Now Sarai was childless because she was not able to conceive.

31Terah took his son Abram, his grandson Lot son of Haran, and his daughter-in-law Sarai, the wife of his son Abram, and together they set out from Ur of the Chaldeans to go to Canaan. But when they came to Harran, they settled there.

32Terah lived 205 years, and he died in Harran.