Mithali 7 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 7:1-27

Onyo Dhidi Ya Mwanamke Mzinzi

17:1 Mt 1:8Mwanangu, shika maneno yangu

na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.

27:2 Mit 4:4; Law 18:5; Kum 32:10Shika amri zangu nawe utaishi;

linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.

37:3 Kum 6:8; Mit 3:3; Isa 30:8; 2Kor 3:3Yafunge katika vidole vyako;

yaandike katika kibao cha moyo wako.

4Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”

uite ufahamu jamaa yako;

57:5 Ay 31:9; Mit 2:16watakuepusha na mwanamke mzinzi,

kutokana na mwanamke mpotovu

na maneno yake ya kubembeleza.

6Kwenye dirisha la nyumba yangu

nilitazama nje kupitia upenyo

kwenye mwimo wa dirisha.

77:7 Mit 6:32Niliona miongoni mwa wajinga,

nikagundua miongoni mwa wanaume vijana,

kijana asiye na akili.

8Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake,

akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke

97:9 Ay 24:15wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake,

giza la usiku lilipokuwa likiingia.

107:10 1Tim 2:9Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki,

hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.

117:11 Mit 9:13; 1Tim 5:13(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi,

miguu yake haitulii nyumbani;

127:12 Mit 8:1-36; 23:26-28mara kwenye barabara za mji,

mara kwenye viwanja vikubwa,

kwenye kila pembe huvizia.)

137:13 Mwa 39:12; Mit 1:20Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu,

na kwa uso usio na haya akamwambia:

147:14 Law 7:11-18“Nina sadaka za amani nyumbani;

leo nimetimiza nadhiri zangu.

15Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki;

nimekutafuta na nimekupata!

167:16 Isa 19:9Nimetandika kitanda changu

kwa kitani za rangi kutoka Misri.

177:17 Amo 6:4; Mwa 37:25Nimetia manukato kitanda changu

kwa manemane, udi na mdalasini.

187:18 Mwa 39:7Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi;

tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!

19Mume wangu hayupo nyumbani;

amekwenda safari ya mbali.

20Amechukua mkoba uliojazwa fedha

na hatakuwepo nyumbani karibuni.”

217:21 Mit 1:8-9; 8:32Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha;

alimshawishi kwa maneno yake laini.

227:22 Ay 18:10Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke

kama fahali aendaye machinjoni,

kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,

237:23 Ay 15:22; 16:13; Mit 6:26; Mhu 9:12mpaka mshale umchome ini lake,

kama ndege anayenaswa kwenye mtego,

bila kujua itamgharimu maisha yake.

247:24 Mit 1:8-9; 8:32Sasa basi wanangu, nisikilizeni;

sikilizeni kwa makini nisemalo.

257:25 Mit 5:7-8Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke,

wala usitangetange katika mapito yake.

267:26 Neh 13:26Aliowaangusha ni wengi;

aliowachinja ni kundi kubwa.

277:27 Amu 16:19; Ufu 22:15Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini,7:27 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti.

King James Version

Proverbs 7:1-27

1My son, keep my words, and lay up my commandments with thee. 2Keep my commandments, and live; and my law as the apple of thine eye. 3Bind them upon thy fingers, write them upon the table of thine heart. 4Say unto wisdom, Thou art my sister; and call understanding thy kinswoman: 5That they may keep thee from the strange woman, from the stranger which flattereth with her words.

6¶ For at the window of my house I looked through my casement, 7And beheld among the simple ones, I discerned among the youths, a young man void of understanding,7.7 the youths: Heb. the sons 8Passing through the street near her corner; and he went the way to her house, 9In the twilight, in the evening, in the black and dark night:7.9 in the evening: Heb. in the evening of days 10And, behold, there met him a woman with the attire of an harlot, and subtil of heart. 11(She is loud and stubborn; her feet abide not in her house: 12Now is she without, now in the streets, and lieth in wait at every corner.) 13So she caught him, and kissed him, and with an impudent face said unto him,7.13 with…: Heb. she strengthened her face and said 14I have peace offerings with me; this day have I payed my vows.7.14 I have…: Heb. Peace offerings are upon me 15Therefore came I forth to meet thee, diligently to seek thy face, and I have found thee. 16I have decked my bed with coverings of tapestry, with carved works, with fine linen of Egypt. 17I have perfumed my bed with myrrh, aloes, and cinnamon. 18Come, let us take our fill of love until the morning: let us solace ourselves with loves. 19For the goodman is not at home, he is gone a long journey: 20He hath taken a bag of money with him, and will come home at the day appointed.7.20 with…: Heb. in his hand7.20 the day…: or, the new moon 21With her much fair speech she caused him to yield, with the flattering of her lips she forced him. 22He goeth after her straightway, as an ox goeth to the slaughter, or as a fool to the correction of the stocks;7.22 straightway: Heb. suddenly 23Till a dart strike through his liver; as a bird hasteth to the snare, and knoweth not that it is for his life.

24¶ Hearken unto me now therefore, O ye children, and attend to the words of my mouth. 25Let not thine heart decline to her ways, go not astray in her paths. 26For she hath cast down many wounded: yea, many strong men have been slain by her. 27Her house is the way to hell, going down to the chambers of death.