Mithali 6 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 6:1-35

Maonyo Dhidi Ya Upumbavu

16:1 Mwa 43:9; Ebr 7:22; Ezr 10:27; Mit 17:18Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako,

ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi

kwa ajili ya mwingine,

2kama umetegwa na ulichosema,

umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,

3basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru,

kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako:

Nenda ukajinyenyekeshe kwake;

msihi jirani yako!

46:4 Rut 3:18; Za 132:4Usiruhusu usingizi machoni pako,

usiruhusu kope zako zisinzie.

56:5 Za 91:3; 2Sam 2:18; Isa 13:14; Za 91:3Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji,

kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.

66:6 Mit 6:11Ewe mvivu, mwendee mchwa;

zitafakari njia zake ukapate hekima!

7Kwa maana yeye hana msimamizi,

wala mwangalizi, au mtawala,

86:8 Mit 30:24-25; 10:4lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi

na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.

96:9 Mit 24:30-34; 26:13-16Ewe mvivu, utalala hata lini?

Utaamka lini kutoka usingizi wako?

106:10 Mit 24:33; Mhu 4:5Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,

bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:

116:11 Mit 6:10-11; 20:13; 24:30-34hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi,

na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

12Mtu mbaya sana na mlaghai,

ambaye huzungukazunguka

na maneno ya upotovu,

136:13 Za 35:19; Mit 16:30ambaye anakonyeza kwa jicho lake,

anayetoa ishara kwa miguu yake

na kuashiria kwa vidole vyake,

146:14 Za 36:4; 140:2; Mik 2:1; Isa 32:7ambaye hupanga ubaya

kwa udanganyifu moyoni mwake:

daima huchochea fitina.

15Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula;

ataangamizwa mara, pasipo msaada.

166:16 Mit 3:32; 8:13; 15:8, 9, 26; 16:5Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana,

naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:

176:17 Za 120:2; Mit 12:22; Yer 2:34; Mik 7:2; Hos 4:1-2macho ya kiburi,

ulimi udanganyao,

mikono imwagayo damu isiyo na hatia,

186:18 Mwa 6:5; Ay 15:31; Rum 3:15moyo uwazao mipango miovu,

miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,

196:19 Kum 19:16; Za 27:12; Mit 15:18; Zek 8:17shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo,

na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.

Onyo Dhidi Ya Uasherati

206:20 Mit 3:21; 1:8Mwanangu, zishike amri za baba yako,

wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

216:21 Kum 6:8; Mit 3:3Yafunge katika moyo wako daima,

yakaze kuizunguka shingo yako.

226:22 Mit 3:23; 2:11Wakati utembeapo, yatakuongoza;

wakati ulalapo, yatakulinda;

wakati uamkapo, yatazungumza nawe.

236:23 Za 19:8; 10:17Kwa maana amri hizi ni taa,

mafundisho haya ni mwanga

na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,

246:24 Mwa 39:8; Za 55:21yakikulinda na mwanamke aliyepotoka,

kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.

256:25 2Sam 11:2-5; Mt 5:28Moyo wako usitamani uzuri wake

wala macho yake yasikuteke,

266:26 Mit 27:22-23; 29:3; Eze 13:18kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini,

hata ukose kipande cha mkate,

naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.

27Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake

bila nguo zake kuungua?

28Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka

bila miguu yake kuungua?

296:29 Kut 20:14; Mit 2:16-19Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine;

hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.

30Watu hawamdharau mwizi kama akiiba

kukidhi njaa yake wakati ana njaa.

316:31 Kut 22:1-14Pamoja na hayo, kama akikamatwa,

lazima alipe mara saba,

ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.

326:32 Kut 20:14; Mit 7:7; 9:4, 16Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa;

yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.

336:33 Mit 5:9-14Mapigo na aibu ni fungu lake

na aibu yake haitafutika kamwe;

346:34 Hes 5:14; Mwa 34:7kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume,

naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.

356:35 Ay 31:9-11; Wim 8:7Hatakubali fidia yoyote;

atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.

Korean Living Bible

잠언 6:1-35

어리석음에 대한 경고

1내 아들아, 네가 만일 이웃을 위해 담보물을 잡히고 다른 사람의 빚 보증을 섰 다가

2네가 한 말로 함정에 빠졌으면

3이것은 네가 네 이웃에게 걸려든 것이니 너는 이렇게 하여라: 그에게 속히 가서 겸손한 태도로 네가 보증 선 것을 취소시켜 달라고 부탁하여 가능한 한 거기서 빠져나오도록 하라.

4너는 그 일을 미루지 말며 그 문제를 해결할 때까지 잠을 자거나 긴장을 풀지 말고

5노루가 사냥꾼의 손에서, 새가 그물을 치는 자의 손에서 벗어나는 것처럼 그 함정에서 빠져나오도록 하라.

6게으른 자여, 개미에게 가서 그 하는 일을 보고 지혜를 얻어라.

7개미는 두목이나 지도자나 감독관이 없어도

8여름 동안에 부지런히 일하여 추수 때에 겨울철에 먹을 양식을 모은다.

9게으른 자여, 네가 언제까지 누워 있을 작정이냐? 언제나 네가 깨어서 일어나겠느냐?

10“좀더 자자. 좀더 졸자. 손을 모으고 좀더 쉬자” 하면

11네가 자는 동안에 가난이 강도같이 너에게 찾아들 것이다.

12불량하고 악한 자는 거짓말만 하고 돌아다니며

13남을 속이려고 눈짓, 손짓, 발짓을 하고

14그 마음은 비뚤어지고 잘못되어 항상 악한 음모를 꾸미며 어디를 가나 말썽만 일으킨다.

15그래서 이런 자는 재난이 갑자기 밀어닥치면 피하지 못하고 망하고 말 것이다.

16여호와께서 미워하고 싫어하는 것이 일곱 가지가 있는데 그것은

17교만한 눈과, 거짓말하는 혀와, 죄 없는 자를 죽이는 손과,

18악한 계획을 세우는 마음과, 악을 행하려고 빨리 달려가는 발과,

19거짓말을 토하는 거짓 증인과, 형제 사이를 이간하는 자이다.

간음에 대한 경고

20내 아들아, 네 아버지의 명령을 지키며 네 어머니의 가르침을 저버리지 말고

21그 말을 항상 네 마음에 새기고 깊이 간직하라.

22그것은 네가 다닐 때에 너를 인도하며 밤에는 너를 보호하고 낮에는 너에게 조언을 해 줄 것이다.

23네 부모의 명령은 등불이며 그 가르침은 빛이요 교육적인 책망은 생명의 길이다.

24이것이 너를 지켜 음란한 여자들의 유혹에 빠지지 않게 할 것이다.

25너는 그들의 아름다움을 보고 색욕을 품지 말며 그들의 눈짓에 홀리지 말아라.

26음란한 여자는 사람의 재산뿐 아니라 사람의 귀중한 생명까지 도둑질해 간다.

27사람이 옷을 태우지 않고 어떻게 불을 품에 품고 다니겠으며

28발을 데지 않고 어떻게 숯불을 밟겠느냐?

29이와 마찬가지로 남의 아내와 잠을 자는 것도 위험한 일이다. 그러므로 누구든지 남의 아내를 만지는 자는 벌을 면치 못할 것이다.

30도둑이 배가 고파 굶주린 배를 채우려고 도둑질하면 사람들이 그를 멸시하지는 않을 것이다.

31하지만 그가 들키면 칠 배를 갚아야 하며 갚을 돈이 없을 때는 자기 집 재산을 다 털어서라도 갚아야 한다.

32그러나 간음하는 자는 지각이 없는 자이다. 그는 자신을 망치고 있을 뿐만 아니라

33얻어 맞아 상처를 입고 모욕을 당하며 언제나 부끄러움을 씻을 수 없을 것이다.

34그 남편이 질투함으로 분노하여 복수하는 날에는 그가 용서받지 못할 것이며

35아무리 많은 위자료나 선물을 준다고 해도 그가 받지 않을 것이다.