Mithali 5 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 5:1-23

Onyo Dhidi Ya Uzinzi

15:1 Mit 1:8Mwanangu, sikiliza kwa makini hekima yangu,

sikiliza vizuri maneno yangu ya busara,

25:2 Mwa 2:7ili uweze kutunza busara

na midomo yako ihifadhi maarifa.

35:3 Za 55:21; Mit 2:16Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba

hudondoza asali,

na maneno ya kinywa chake

ni laini kuliko mafuta;

45:4 Mhu 7:26; Ebr 4:12lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo,

mkali kama upanga ukatao kuwili.

55:5 Za 9:17; Mit 2:18Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo;

hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.5:5 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

65:6 Mit 9:13; 30:20Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima;

njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.

75:7 Mit 1:8-9Sasa basi wanangu, nisikilizeni;

msiache ninalowaambia.

85:8 Mit 6:20-29; 7:1-27Njia zenu ziwe mbali naye,

msiende karibu na mlango wa nyumba yake,

9usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine

na miaka yako kwa aliye mkatili,

105:10 Mit 29:3wageni wasije wakasherehekea utajiri wako

na jitihada yako ikatajirisha

nyumba ya mwanaume mwingine.

11Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu,

wakati nyama na mwili wako vimechakaa.

12Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu!

Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!

13Sikuwatii walimu wangu

wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.

145:14 Mit 1:24-27; 6:33; 31:3Nimefika ukingoni mwa maangamizi kabisa

katikati ya kusanyiko lote.”

15Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe,

maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.

16Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji

na vijito vyako vya maji viwanjani?

17Na viwe vyako mwenyewe,

kamwe visishirikishwe wageni.

185:18 Wim 4:12-15; Kum 20:7; Mal 2:14Chemchemi yako na ibarikiwe

na umfurahie mke wa ujana wako.

195:19 Wim 2:9; 8:14Kulungu jike apendaye, kulungu mzuri:

matiti yake na yakutosheleze siku zote,

nawe utekwe daima na upendo wake.

205:20 Mit 2:16; 7:5Kwa nini mwanangu, utekwe na mwanamke kahaba?

Kwa nini ukumbatie kifua cha mke wa mwanaume mwingine?

215:21 Za 119:168; Hos 7:2; Yer 16:17; Ay 10:4; Ebr 4:13Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele za Bwana,

naye huyapima mapito yake yote.

225:22 Za 9:16; Hes 32:23; Ay 18:9Matendo mabaya ya mtu mwovu humnasa yeye mwenyewe;

kamba za dhambi yake humkamata kwa nguvu.

235:23 Ay 4:21; 36:12Atakufa kwa kukosa nidhamu,

akipotoshwa kwa upumbavu wake mwenyewe.

Korean Living Bible

잠언 5:1-23

간음에 대한 경고

1내 아들아, 내가 지혜와 통찰력으로 가르치는 말을 잘 귀담아 듣고

2모든 일을 신중하게 하며 네 말에 지식이 깃들여 있음을 보여 주어라.

3방탕한 여인의 입술은 꿀보다 달고 그 입은 기름보다 더 미끄러우나

4나중에는 쓰라림과 고통만을 남겨 줄 뿐이다.

5그런 여자는 지옥을 향해 죽음의 길을 치닫고 있으면서도

6생명의 길을 생각하지 못하며 자기 길이 비뚤어져도 그것을 깨닫지 못한다.

7내 아들들아, 이제 너희는 내 말을 잘 듣고 잊지 말며

8그런 여자를 멀리하고 그녀의 집 문에도 가까이 가지 말아라.

9그렇지 않으면 한때 네가 누리던 영예를 다른 사람에게 빼앗기게 되고 너는 난폭한 자들의 손에 죽음을 당할 것이며

10낯선 사람들이 네 재물로 배를 채우고 네 수고한 것이 다른 사람의 집으로 갈 것이다.

11그럴 경우 결국 네 육체는 병들어 못 쓰게 되고 너는 이렇게 탄식하게 될 것이다.

12“내가 왜 훈계를 싫어하며 어째서 내 마음이 꾸지람을 가볍게 여겼는가?

13내가 내 스승의 말을 듣지 않았고 나를 가르치는 사람에게 귀를 기울이지 않았더니

14이제 많은 사람들 앞에서 수치를 당하게 되었구나.”

15너는 5:15 원문에는 ‘네 우물에서 물을 마시며 네 샘에서 흐르는 물을 마시라’네 아내에게 성실하고 그녀만 사랑하여라.

16네가 다른 여인에게 정을 주어 자식을 낳게 할 이유가 무엇이냐?

17너는 네 자녀를 얻는 복을 다른 사람과 나누지 못하게 하라.

185:18 15-18절까지는 의역하였음.네가 젊어서 얻은 아내를 행복하게 하고 그녀와 함께 즐거워하라.

19너는 암사슴처럼 그녀를 사랑스럽고 아름답게 여겨 그 품을 항상 만족하게 여기며 그녀의 사랑을 항상 연모하라.

20내 아들아, 네가 무엇 때문에 음란한 여자에게 정을 주어야 하며 남의 아내 가슴을 안아야 하겠느냐?

21여호와께서는 사람이 하는 일을 다 지켜 보시므로 네가 무엇을 하든지 다 알고 계신다.

22악인은 자기 악에 스스로 걸려 넘어지며 자기 죄의 줄에 자기가 매인다.

23그는 진리의 교훈을 듣지 않으므로 죽을 것이며 너무 어리석은 탓으로 길을 잃고 방황할 것이다.