Mithali 4 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 4:1-27

Hekima Ni Bora Kupita Vitu Vyote

14:1 Mit 1:8; 19:20; Ay 8:10Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu;

sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.

2Ninawapa mafundisho ya maana,

kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.

34:3 1Nya 29:1; 2Sam 12:24Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu,

ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,

44:4 Mit 7:2; 1Nya 28:9baba alinifundisha akisema,

“Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote;

yashike maagizo yangu na wewe utaishi.

54:5 Mit 3:13-18; 16:16Pata hekima, pata ufahamu;

usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.

64:6 2The 2:10; Mit 2:11Usimwache hekima naye atakuweka salama;

mpende, naye atakulinda.

74:7 Mt 13:44-46; Mit 23:23Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima.

Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.

84:8 1Sam 2:30; Mit 3:18Mstahi, naye atakukweza;

mkumbatie, naye atakuheshimu.

94:9 Mit 1:8-9Atakuvika shada la neema kichwani mwako

na kukupa taji ya utukufu.”

104:10 Kum 11:21; Mit 3:2Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia,

nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.

114:11 1Sam 12:23; 2Sam 22:37; Za 5:8Ninakuongoza katika njia ya hekima

na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.

124:12 Ay 18:7; Yer 13:16; Za 18:36Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa;

ukimbiapo, hutajikwaa.

134:13 Mit 3:22Mkamate sana elimu, usimwache aende zake;

mshike, maana yeye ni uzima wako.

144:14 Za 1:1; Mit 1:15Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu

wala usitembee katika njia ya watu wabaya.

15Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo;

achana nayo, na uelekee njia yako.

164:16 Za 36:4; Mik 7:3Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu;

wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.

174:17 Mwa 49:5; Za 73:6; Mit 1:10-19; Isa 59:6; Yer 22:3; Hab 1:2; Mal 2:16Wanakula mkate wa uovu,

na kunywa mvinyo wa jeuri.

184:18 Mt 5:14; Ay 17:9; Isa 26:7; Dan 12:3; Yn 8:12Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko,

ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.

194:19 Ay 18:5; Yn 12:35Lakini njia ya waovu ni kama giza nene;

hawajui kinachowafanya wajikwae.

204:20 Za 34:11-16; Mit 1:8-9; 5:1Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia;

sikiliza kwa makini maneno yangu.

214:21 Mit 3:21Usiruhusu yaondoke machoni pako,

yahifadhi ndani ya moyo wako;

224:22 Mit 3:8kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata

na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.

234:23 Mit 10:11; Mt 12:34Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo,

maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

24Epusha kinywa chako na ukaidi;

weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.

254:25 Ay 31:1Macho yako na yatazame mbele,

kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.

264:26 Ebr 12:13Sawazisha mapito ya miguu yako

na njia zako zote ziwe zimethibitika.

274:27 Law 10:11; Kum 28:14Usigeuke kulia wala kushoto;

epusha mguu wako na ubaya.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

箴言 4:1-27

父親的教誨

1孩子們啊,

你們要聽從父親的教誨,

留心學習,以便領悟,

2因為我給你們的訓誨是美好的,

不可背棄我的教導。

3我年幼時在父親身邊,

是母親唯一的寵兒。

4父親教導我說:

「要牢記我的話,

遵守我的誡命,就必存活。

5你要尋求智慧和悟性,

不要忘記或違背我的吩咐。

6不可離棄智慧,智慧必護佑你;

你要熱愛智慧,智慧必看顧你。

7智慧至上,要尋求智慧,

要不惜一切,求得悟性。

8高舉智慧,她必使你受尊崇;

擁抱智慧,她必使你得尊榮。

9她必為你戴上華冠,

加上榮冕。」

10孩子啊,你要聽從我的教導,

就必延年益壽。

11我已經指示你走智慧之道,

引導你行正確的路。

12你行走,必不受妨礙;

你奔跑,絕不會跌倒。

13你要持守教誨,不要鬆懈;

要守護好,因為那是你的生命。

14不要涉足惡人的道,

不要行走壞人的路;

15要避開,不可踏足,

要繞道而行。

16因為他們不作惡就無法入睡,

不絆倒人就無法安眠;

17他們吃的是邪惡餅,

喝的是殘暴酒。

18義人的道路好像黎明的曙光,

越照越亮,直到大放光明。

19惡人的道路一片幽暗,

他們不知被何物絆倒。

20孩子啊,你要聆聽我的吩咐,

側耳聽我的訓言;

21不要讓它們離開你的視線,

要牢記在心。

22因為得到它們就得到生命,

全身也必康健。

23要一絲不苟地守護你的心,

因為生命之泉從心中湧出。

24不講欺詐之言,

不說荒謬的話。

25眼睛要正視前方,

雙目要向前直看。

26要鋪平腳下的路,

使所行之道穩妥。

27不可偏右偏左,

要遠離惡事。