Mithali 3 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 3:1-35

Faida Nyingine Za Hekima

13:1 Kum 30:16; Za 44:17; Mit 4:5Mwanangu, usisahau mafundisho yangu,

bali zitunze amri zangu moyoni mwako,

23:2 Mit 9:6; 4:10kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako

na kukuletea mafanikio.

33:3 Kum 6:8; Mit 6:21; 2Kor 3:3Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe;

vifunge shingoni mwako,

viandike katika ubao wa moyo wako.

43:4 1Sam 2:26; Lk 2:52; Mdo 2:47Ndipo utapata kibali na jina zuri

mbele za Mungu na mwanadamu.

53:5 Za 4:5; Yer 9:23Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote

wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

63:6 1Nya 28:9; Ay 33:11; Yer 42:3katika njia zako zote mkiri yeye,

naye atayanyoosha mapito yako.

73:7 Isa 5:21; Rum 12:16; Kum 4:6Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe;

mche Bwana ukajiepushe na uovu.

83:8 Za 38:3; Mit 4:22; Ay 21:24Hii itakuletea afya mwilini mwako,

na mafuta kwenye mifupa yako.

93:9 Kut 23:19; 26:1-15Mheshimu Bwana kwa mali zako na

kwa malimbuko ya mazao yako yote;

103:10 Kum 28:8; Za 144:13; Ay 22:21; Mal 3:10-12ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika,

viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.

113:11 Mit 1:8-9; Ay 5:17Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana

na usichukie kukaripiwa naye,

123:12 Mit 13:24; Ufu 3:19; Ay 3:19; 5:17; Ebr 12:5-6kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao,

kama vile baba afanyavyo

kwa mwana apendezwaye naye.

133:13 Mit 8:34, 35Heri mtu yule aonaye hekima,

mtu yule apataye ufahamu,

143:14 Ay 28:15; Mit 16:16kwa maana hekima ana faida kuliko fedha

na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.

153:15 Ay 28:17-19Hekima ana thamani kuliko marijani;

hakuna chochote unachokitamani

kinachoweza kulinganishwa naye.

163:16 1Fal 3:13-14; Mit 8:18Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume;

katika mkono wake wa kushoto

kuna utajiri na heshima.

173:17 Mit 16:7; Mt 11:28-30Njia zake zinapendeza,

mapito yake yote ni amani.

183:18 Mwa 2:9; Ufu 2:7Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia;

wale wamshikao watabarikiwa.

193:19 Ay 28:25-27; Za 104:24; Mit 8:27-29Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia,

kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;

203:20 Kum 33:28; Ay 36:28kwa maarifa yake vilindi viligawanywa,

nayo mawingu yanadondosha umande.

213:21 Mit 1:8-9; 6:20; 4:20-22Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara,

usiache vitoke machoni pako;

223:22 Kum 30:20; Mit 4:20-22ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako

na pambo la neema shingoni mwako.

23Kisha utaenda katika njia yako salama,

wala mguu wako hautajikwaa;

243:24 Law 26:6; Za 3:5; Ay 11:18; Yer 31:25ulalapo, hautaogopa;

ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.

253:25 Za 91:5; 112:7Usiogope maafa ya ghafula

au maangamizi yanayowapata waovu,

263:26 1Sam 2:9kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako

na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.

273:27 Rum 13:7; Gal 6:10Usizuie wema kwa wale wanaostahili

ikiwa katika uwezo wako kutenda.

283:28 Law 19:13; Lk 10:25-37; Kum 24:15Usimwambie jirani yako,

“Njoo baadaye, nitakupa kesho”:

wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.

293:29 Zek 8:17Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako,

ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.

303:30 Rum 12:18Usimshtaki mtu bila sababu,

wakati hajakutenda dhara lolote.

313:31 Za 37:1; Mit 24:1-2Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri

wala kuchagua njia yake iwayo yote,

323:32 Za 101:4; Ay 29:4kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu,

lakini siri yake iko kwa mwenye haki.

333:33 Ay 5:3; Mal 2:2; Zek 5:4Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu,

lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.

343:34 Za 18:25-27; Mt 23:12Huwadhihaki wale wanaodhihaki,

lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.

35Wenye hekima hurithi heshima,

bali huwaaibisha wapumbavu.

New International Version – UK

Proverbs 3:1-35

Wisdom bestows well-being

1My son, do not forget my teaching,

but keep my commands in your heart,

2for they will prolong your life many years

and bring you peace and prosperity.

3Let love and faithfulness never leave you;

bind them round your neck,

write them on the tablet of your heart.

4Then you will win favour and a good name

in the sight of God and man.

5Trust in the Lord with all your heart

and lean not on your own understanding;

6in all your ways submit to him,

and he will make your paths straight.3:6 Or will direct your paths

7Do not be wise in your own eyes;

fear the Lord and shun evil.

8This will bring health to your body

and nourishment to your bones.

9Honour the Lord with your wealth,

with the firstfruits of all your crops;

10then your barns will be filled to overflowing,

and your vats will brim over with new wine.

11My son, do not despise the Lord’s discipline,

and do not resent his rebuke,

12because the Lord disciplines those he loves,

as a father the son he delights in.3:12 Hebrew; Septuagint loves, / and he chastens everyone he accepts as his child

13Blessed are those who find wisdom,

those who gain understanding,

14for she is more profitable than silver

and yields better returns than gold.

15She is more precious than rubies;

nothing you desire can compare with her.

16Long life is in her right hand;

in her left hand are riches and honour.

17Her ways are pleasant ways,

and all her paths are peace.

18She is a tree of life to those who take hold of her;

those who hold her fast will be blessed.

19By wisdom the Lord laid the earth’s foundations,

by understanding he set the heavens in place;

20by his knowledge the watery depths were divided,

and the clouds let drop the dew.

21My son, do not let wisdom and understanding out of your sight,

preserve sound judgment and discretion;

22they will be life for you,

an ornament to grace your neck.

23Then you will go on your way in safety,

and your foot will not stumble.

24When you lie down, you will not be afraid;

when you lie down, your sleep will be sweet.

25Have no fear of sudden disaster

or of the ruin that overtakes the wicked,

26for the Lord will be at your side

and will keep your foot from being snared.

27Do not withhold good from those to whom it is due,

when it is in your power to act.

28Do not say to your neighbour,

‘Come back tomorrow and I’ll give it to you’ –

when you already have it with you.

29Do not plot harm against your neighbour,

who lives trustfully near you.

30Do not accuse anyone for no reason –

when they have done you no harm.

31Do not envy the violent

or choose any of their ways.

32For the Lord detests the perverse

but takes the upright into his confidence.

33The Lord’s curse is on the house of the wicked,

but he blesses the home of the righteous.

34He mocks proud mockers

but shows favour to the humble and oppressed.

35The wise inherit honour,

but fools get only shame.