Mithali 27 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 27:1-27

127:1 Lk 12:19-20; Yak 4:13; Mt 6:34; 1Fal 20:11Usijisifu kwa ajili ya kesho,

kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.

227:2 Mit 25:27Mwache mwingine akusifu,

wala si kinywa chako mwenyewe;

mtu mwingine afanye hivyo

na si midomo yako mwenyewe.

327:3 Ay 6:3; Es 1:12Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo,

lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.

427:4 1Yn 3:12Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika,

lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?

527:5 Gal 2:14Afadhali karipio la wazi

kuliko upendo uliofichika.

627:6 Za 141:5; Mit 28:23Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu,

bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.

727:7 Ay 6:7Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali,

bali kwa mwenye njaa

hata kile kilicho kichungu

kwake ni kitamu.

827:8 Isa 16:2; Ay 39:14Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake,

ndivyo alivyo mtu atangatangaye

mbali na nyumbani mwake.

927:9 Es 2:12; Za 45:8Manukato na uvumba huleta furaha moyoni,

nao uzuri wa rafiki huchipuka

kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.

1027:10 Mit 17:17Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako,

tena usiende nyumbani mwa ndugu yako

wakati umepatwa na maafa.

Bora jirani wa karibu

kuliko ndugu aliye mbali.

1127:11 Mit 10:1; 23:15-16; Mwa 24:60Mwanangu, uwe na hekima,

nawe ulete furaha moyoni mwangu,

ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote

anitendaye kwa dharau.

1227:12 Mit 22:3Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha,

bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.

1327:13 Mit 20:16Chukua vazi la yule awekaye dhamana

kwa ajili ya mgeni;

lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo

kwa ajili ya mwanamke mpotovu.

1427:14 Za 12:2Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu

asubuhi na mapema,

itahesabiwa kama ni laana.

1527:15 Es 1:18; Mit 19:13Mke mgomvi ni kama

matone yasiyokoma ya siku ya mvua.

16Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo

au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.

17Kama vile chuma kinoavyo chuma,

ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.

1827:18 1Kor 9:7; Lk 19:12-27; Kum 20:6Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake,

naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.

19Kama uso uonekanavyo kwenye maji,

ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.

2027:20 Mit 30:15-16; Hab 2:5; Mhu 6:7Kuzimu na Uharibifu havishibi

kadhalika macho ya mwanadamu.

2127:21 Mit 17:3Kalibu ni kwa ajili ya fedha

na tanuru kwa ajili ya dhahabu,

bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.

2227:22 Isa 1:5; Yer 5:3; Mit 23:35Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu,

ukimtwanga kama nafaka kwa mchi,

hutauondoa upumbavu wake.

2327:23 Mit 12:10; Yer 5:3Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako

ya kondoo na mbuzi,

angalia kwa bidii ngʼombe zako.

2427:24 Mit 23:5Kwa kuwa utajiri haudumu milele,

nayo taji haidumu vizazi vyote.

2527:25 Za 104:14Wakati majani makavu yameondolewa

na mapya yamechipua,

nayo majani toka milimani yamekusanywa,

26wana-kondoo watakupatia mavazi

na mbuzi thamani ya shamba.

27Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi

kukulisha wewe na jamaa yako,

na kuwalisha watumishi wako wa kike.

Hoffnung für Alle

Sprüche 27:1-27

Liebe, die offen zurechtweist

1Brüste dich nicht mit dem, was du morgen tun willst, denn du weißt nicht, was der Tag dir bringt!

2Überlass es anderen, dich zu loben! Es ist besser, ein Fremder rühmt dich, als du selbst!

3Schon ein Stein oder eine Karre Sand sind sehr schwer, aber der Ärger über einen Dummkopf wiegt mehr als beide zusammen!

4Zorn und Wut sind so zerstörerisch wie ein reißender Strom – gegen die Eifersucht aber verblassen sie beide!

5Liebe, die offen zurechtweist, ist besser als Liebe, die sich ängstlich zurückhält.

6Ein Freund meint es gut, selbst wenn er dich verletzt; ein Feind aber schmeichelt dir mit übertrieben vielen Küssen.

7Wer satt ist, will auch den besten Honig nicht mehr sehen; dem Hungrigen aber schmeckt sogar das Bittere süß.

8Wer seine Heimat verlässt, ist wie ein Vogel, der seinem Nest entflieht.

9Duftendes Öl und Weihrauch erfreuen das Herz, genauso wohltuend ist der gute Rat eines Freundes.

10Verlass niemals deinen Freund oder den Freund deines Vaters! Wenn du in Not gerätst, dann geh nicht bis zum Haus deines Bruders! Ein Nachbar in der Nähe kann dir besser helfen als der Bruder in der Ferne.

11Sei verständig, mein Sohn, und mach mir diese Freude! Dann habe ich eine passende Antwort für jeden, der mich verachtet und beschimpft.

12Der Kluge sieht das Unglück voraus und bringt sich in Sicherheit; ein Unerfahrener rennt mitten hinein und muss die Folgen tragen.

13Wenn jemand so leichtsinnig war, für die Schulden eines Fremden zu bürgen, dann leihe ihm nur etwas gegen Pfand!

14Wenn jemand seinen Nachbarn frühmorgens mit lauter Stimme begrüßt, dann wird es ihm als Verwünschung ausgelegt.

15Eine nörgelnde Frau ist so unerträglich wie ein undichtes Dach bei Dauerregen!

16Sie zum Schweigen zu bringen ist so sinnlos, wie den Wind zu fangen oder Öl mit den Händen zu halten!

17Wie man Eisen durch Eisen schleift, so schleift ein Mensch den Charakter eines anderen.

18Wer seinen Feigenbaum pflegt, kann die Früchte ernten; wer sich für seinen Herrn einsetzt, der findet Anerkennung.

19Im Wasser spiegelt sich dein Gesicht, und durch die Menschen um dich herum erkennst du dich selbst27,19 Oder: und in deinen Gedanken und Gefühlen erkennst du dich selbst.!

20Der Abgrund des Totenreichs ist unersättlich – ebenso die Augen des Menschen: Sie haben nie genug!

21Gold und Silber prüft man durch Schmelzen, der Prüfstein eines Menschen ist sein Ruf.

22Du könntest einen Unverständigen wie Getreide stampfen und mahlen – seine Dummheit wirst du doch nicht aus ihm herausbekommen!

23Kümmere dich gut um deine Viehherden, sorge für deine Schafe und Ziegen, 24denn Reichtum bleibt nicht für immer, und selbst Königreiche vergehen! 25Mähe die Wiesen, damit frisches Gras nachwachsen kann, und hole das Heu von den Bergen! 26Aus der Wolle der Schafe kannst du Kleider anfertigen, und von dem Geld, das du für die Ziegenböcke bekommst, neues Land kaufen. 27Die Ziegen geben Milch für dich und deine Familie und für alle deine Mägde.