Mithali 25 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 25:1-28

Mithali Zaidi Za Solomoni

125:1 1Fal 4:32Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:

225:2 Kum 29:29; Rum 11:33; Mit 10:10-15Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo,

bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.

3Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini,

ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.

425:4 2Tim 2:21Ondoa takataka kwenye madini ya fedha,

nako ndani yake kutatokea chombo

cha mfua fedha.

525:5 2Sam 7:13; Mit 20:8; 29:14Ondoa waovu mbele ya mfalme,

nacho kiti chake cha enzi

kitaimarishwa kwa njia ya haki.

6Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme,

wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;

725:7 Lk 14:7-10ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,”

kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu.

Kile ulichokiona kwa macho yako

825:8 Mit 17:14; Mt 5:25-26usiharakishe kukipeleka mahakamani,

maana utafanya nini mwishoni

kama jirani yako atakuaibisha?

925:9 Mt 5:25; 18:15Kama ukifanya shauri na jirani yako,

usisaliti siri ya mtu mwingine,

10ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha

na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.

1125:11 Mit 15:23; Isa 50:4Neno lisemwalo kwa wakati ufaao

ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu

yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.

1225:12 Za 141:5; Mit 15:31Kama vile kipuli cha dhahabu

au pambo la dhahabu safi,

ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima

kwa sikio lisikilizalo.

1325:13 Mit 13:17; 10:26Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno

ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao,

huburudisha roho za bwana zake.

1425:14 Mit 20:6; Yud 12Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua

ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.

1525:15 Mhu 10:4; Mit 15:1; Mwa 32:4; 1Sam 25:24Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa,

nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.

1625:16 Mit 25:27Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha,

ukila zaidi, utatapika.

17Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache,

ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.

1825:18 Za 57:4; Mit 12:18Kama vile rungu au upanga au mshale mkali

ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.

1925:19 Ay 6:14-20; 2Tim 4:16Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa,

ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.

2025:20 Dan 6:18; Rum 12:15Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi,

au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi,

ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.

2125:21 Kut 23:4; Mt 5:44; Rum 12:20Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale;

kama ana kiu, mpe maji anywe.

2225:22 2Sam 16:22; Mt 5:44; Za 18:8Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake,

naye Bwana atakupa thawabu.

2325:23 Ay 37:22; Za 105:5Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua,

ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.

2425:24 Mit 19:13; 21:9, 19Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba,

kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.

25Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka

ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.

2625:26 Mik 7:8Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au

kisima kilichotiwa taka

ndivyo alivyo mtu mwenye haki

akishiriki na waovu.

2725:27 Mit 27:2; Mt 23:12; Lk 14:11Si vyema kula asali nyingi sana,

wala si heshima

kujitafutia heshima yako mwenyewe.

2825:28 Mit 16:32Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka

ndivyo alivyo mtu

ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.

New International Reader’s Version

Proverbs 25:1-28

More Proverbs of Solomon

1These are more proverbs of Solomon. They were gathered together by the men of Hezekiah, the king of Judah.

2When God hides a matter, he gets glory.

When kings figure out a matter, they get glory.

3The heavens are high and the earth is deep.

In the same way, the minds of kings are impossible to figure out.

4Remove the scum from the silver.

Then the master worker can make something out of it.

5Remove ungodly officials from where the king is.

Then the king can make his throne secure because of the godliness around him.

6Don’t brag in front of the king.

Don’t claim a place among his great men.

7Let the king say to you, “Come up here.”

That’s better than for him to shame you in front of his nobles.

What you have seen with your own eyes

8don’t bring too quickly to court.

What will you do in the end

if your neighbor puts you to shame?

9If you take your neighbor to court,

don’t tell others any secrets you promised to keep.

10If you do, someone might hear it and put you to shame.

And the charge against you will stand.

11The right ruling at the right time

is like golden apples in silver jewelry.

12A wise judge’s warning to a listening ear

is like a gold earring or jewelry made of fine gold.

13A messenger trusted by the one who sends him

is like a drink cooled by snow at harvest time.

He renews the spirit of his master.

14A person who brags about gifts never given

is like wind and clouds that don’t produce rain.

15If you are patient, you can win an official over to your side.

And gentle words can break a bone.

16If you find honey, eat just enough.

If you eat too much of it, you will throw up.

17Don’t go to your neighbor’s home very often.

If they see too much of you, they will hate you.

18A person who is a false witness against a neighbor

is like a club, a sword or a sharp arrow.

19Trusting someone who is not faithful when trouble comes

is like a broken tooth or a disabled foot.

20You may sing songs to a troubled heart.

But that’s like taking a coat away on a cold day.

It’s like pouring vinegar on a wound.

21If your enemy is hungry, give him food to eat.

If he is thirsty, give him water to drink.

22By doing these things, you will pile up burning coals on his head.

And the Lord will reward you.

23Like a north wind that brings rain you didn’t expect

is a crafty tongue that brings looks of shock.

24It is better to live on a corner of a roof

than to share a house with a nagging wife.

25Hearing good news from a land far away

is like drinking cold water when you are tired.

26Sometimes godly people give in to those who are evil.

Then they become like a muddy spring of water or a polluted well.

27It isn’t good for you to eat too much honey.

And you shouldn’t try to search out matters too deep for you.

28A person without self-control

is like a city whose walls are broken through.