Mithali 24 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 24:1-34

124:1 Mit 3:31-32; 23:17-18Usiwaonee wivu watu waovu,

usitamani ushirika nao;

224:2 Za 2:1; 10:7; Isa 32:6; 55:7-8; 59:7; 65:2; Hos 4:1kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri,

nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.

324:3 Mit 14:1Kwa hekima nyumba hujengwa,

nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa

424:4 Mit 8:21kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa

vitu vya thamani na vya kupendeza.

524:5 Mit 21:22Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa,

naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,

624:6 Mit 11:14; Lk 14:31kwa kufanya vita unahitaji uongozi

na kwa ushindi washauri wengi.

724:7 Za 10:5; Mit 14:6Hekima i juu mno kwa mpumbavu,

katika kusanyiko langoni

hana lolote la kusema.

824:8 Rum 1:30Yeye apangaye mabaya

atajulikana kama mtu wa hila.

924:9 Mwa 6:5; Za 119:113; Mt 9:4; Mdo 8:22; 2Kor 10:524:9 Mwa 6:5; Mdo 8:22; 2Kor 10:5Mipango ya upumbavu ni dhambi,

watu huchukizwa na mwenye dhihaka.

1024:10 Yer 51:46; Ebr 12:3Ukikata tamaa wakati wa taabu,

jinsi gani nguvu zako ni kidogo!

1124:11 Isa 58:6-7; 1Yn 3:16; Za 82:4Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo;

wazuie wote wanaojikokota

kuelekea machinjoni.

1224:12 Za 139:2; Mit 16:24; 21:2; Yer 32:19; Mt 16:24Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,”

je, yule apimaye mioyo halitambui hili?

Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili?

Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?

1324:13 Wim 5:1Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri;

asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.

1424:14 Za 119:103; Mit 16:24; 23:18Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako,

kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo,

nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.

1524:15 Za 10:9, 10Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia

makao ya mwenye haki,

wala usiyavamie makazi yake,

1624:16 Ay 5:19; Mik 7:8; Za 34:19Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena,

lakini waovu huangushwa chini na maafa.

1724:17 Oba 1:12; Ay 31:29Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo;

wakati ajikwaapo,

usiruhusu moyo wako ushangilie.

1824:18 Ay 31:29Bwana asije akaona na kuchukia

akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.

1924:19 Za 37:1Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya

wala usiwaonee wivu waovu,

2024:20 Ay 18:5; Mit 13:9; Isa 3:11kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo,

nayo taa ya waovu itazimwa.

2124:21 Rum 13:1-7; 1Pet 2:17Mwanangu, mche Bwana na mfalme,

wala usijiunge na waasi,

2224:22 Za 73:19kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao,

naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?

Misemo Zaidi Ya Wenye Hekima

2324:23 Kut 18:16; Law 19:15; 2Nya 19:7; Za 72:2; Yer 22:16; Yn 7:24Hii pia ni misemo ya wenye hekima:

Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:

2424:24 Isa 5:23; Mit 17:15Yeyote amwambiaye mwenye hatia,

“Wewe huna hatia,”

Kabila zitamlaani

na mataifa yatamkana.

25Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia,

nazo baraka tele zitawajilia juu yao.

26Jawabu la uaminifu

ni kama busu la midomoni.

2724:27 1Fal 5:17, 18; Lk 14:28Maliza kazi zako za nje,

nawe uweke mashamba yako tayari,

baada ya hayo, jenga nyumba yako.

2824:28 Za 7:4; Efe 4:25Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu,

au kutumia midomo yako kudanganya.

2924:29 Mit 20:22; Rum 12:17; Mt 5:39Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi;

nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”

3024:30 Mit 6:6-11; 26:13-16Nilipita karibu na shamba la mvivu,

karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,

3124:31 Yer 4:3; Ebr 6:8miiba ilikuwa imeota kila mahali,

ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na

ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.

32Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona,

nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:

3324:33 Mit 6:10Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,

bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:

3424:34 Mit 10:4; Mhu 10:18hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi,

na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

Japanese Contemporary Bible

箴言 知恵の泉 24:1-34

24

1神を信じない人々をうらやんではいけません。

仲間になろうと思ってもいけません。

2彼らは毎日毎日、人に乱暴し、

だますことに明け暮れているのです。

3-4事業を始めるときは、

よく考えてきちんと計画を立て、

しっかり基礎を固めなさい。

こうして実際をしっかり見ながら進めば、

成功は間違いなしです。

5知恵のある人は力のある人より強く、

知恵は力より優れています。

6戦いに出かけるときは、

知恵のある人の意見を聞いてからにしなさい。

助言する人が大ぜいいれば安心です。

7神に背く者には、知恵は高すぎて買えません。

だから、人前で意見を言わせてもらえません。

8悪いことを企むのも、それを実行するのも、

同じように悪いことです。

9神に背く者は悪い計画ばかり立て、

人をさげすむ者は世界中の人にきらわれます。

10逆境のとき、苦しみに耐えられない者は弱い者です。

11-12無実の罪で死刑を宣告された人を助けなさい。

その人が殺されるのを、

黙って眺めていてはいけません。

「全く知らなかった」ととぼけても、

神の目はごまかせません。

神はそれぞれの行いにふさわしく報いられるのです。

13-14わが子よ。はちみつが食欲をそそるように、

知恵はあなたの心に

賢くなりたいという意欲を起こさせます。

それがあれば、

希望にあふれた将来が約束されます。

15-16悪者よ。正しい人に手出しをしてはいけません。

正しい人は七度倒れても、

そのたびに起き上がることを知らないのですか。

しかし悪者は、一度つまずくと滅びるのです。

17敵が苦しむのを喜んではいけません。

敵が失敗したからといって、

うれしがってはいけません。

18そんなことをしたら主が心を痛め、

彼らを罰するのをやめるかもしれません。

19-20悪人をうらやみ、

その財産を欲しがってはいけません。

悪人の最後は目に見えているからです。

21-22わが子よ。主と王の前では注意深く行動しなさい。

過激な者たちとつき合ってはいけません。

彼らのいのちは短く、

思いもよらない災いに会うからです。

知恵のことば(2)

23貧しい人を有罪とし、

金持ちを赦すのはよくありません。

24悪者に向かって「無罪だ」と言う者は、

大ぜいの人にのろわれます。

25逆に、悪者の罪をはっきりと指摘する人は、

だれからも感謝されます。

26率直に答えてもらえることは、

ありがたいことだと思いなさい。

27家を建てるのは、仕事がうまくいってからにしなさい。

28-29無実の人について、

わざと不利な証言やうその証言をしてはいけません。

「いい機会だから、これまでの仕返しをしてやろう」と

考えてはいけません。

30-31怠け者の畑のそばを通ったら、

いばらと雑草だらけで柵も壊れています。

32-33これを見て学びました。

「もうちょっと眠り、もうちょっと昼寝し、

もうちょっと休もう。」

34こんな生活をしていると、どんどん貧しくなり、

どうにもならなくなります。