Mithali 23 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 23:1-35

1Uketipo kula chakula na mtawala,

angalia vyema kile kilicho mbele yako,

2na utie kisu kooni mwako

kama ukiwa mlafi.

323:3 Za 141:4Usitamani vyakula vyake vitamu

kwa kuwa chakula hicho ni cha hila.

423:4 Yn 6:27; 1Tim 6:9; Rum 12:16Usijitaabishe ili kuupata utajiri,

uwe na hekima kuonyesha kujizuia.

523:5 Mt 6:19; Mit 27:24Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka,

huwa kama umepata mabawa ghafula,

ukaruka na kutoweka angani kama tai.

623:6 Za 141:4; Kum 15:9Usile chakula cha mtu mchoyo,

usitamani vyakula vyake vitamu,

723:7 Za 12:2kwa maana yeye ni aina ya mtu

ambaye kila mara anafikiri juu ya gharama.

Anakuambia, “Kula na kunywa,”

lakini moyo wake hauko pamoja nawe.

8Utatapika kile kidogo ulichokula,

nawe utakuwa umepoteza bure

maneno yako ya kumsifu.

923:9 Mit 9:7Usizungumze na mpumbavu,

kwa maana atadhihaki hekima ya maneno yako.

1023:10 Kum 19:14; Mit 22:28Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani

wala kunyemelea kwenye mashamba ya yatima,

1123:11 Ay 19:25; Kut 22:22-24; Yer 50:34; Mit 15:25kwa kuwa Mtetezi wao ni mwenye nguvu,

atalichukua shauri lao dhidi yako.

1223:12 Mit 2:2Elekeza moyo wako kwenye mafundisho

na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.

1323:13 Mit 13:24; 19:18; 22:18; 22:15; 29:15, 16Usimnyime mtoto adhabu,

ukimwadhibu kwa fimbo, hatakufa.

1423:14 Mit 13:24; 19:18Mwadhibu kwa fimbo

na kuiokoa nafsi yake kutoka mautini.23:14 Mautini maana yake ni Kuzimu.

1523:15 Mit 23:24, 25; 29:3Mwanangu, kama moyo wako una hekima,

basi moyo wangu utafurahi,

1623:16 Mit 23:24utu wangu wa ndani utafurahi,

wakati midomo yako

itakapozungumza lililo sawa.

1723:17 Za 73:3; Mit 28:14Usiuruhusu moyo wako kuwaonea wivu wenye dhambi,

bali kila mara uwe na bidii katika kumcha Bwana.

1823:18 Za 37:1-4; Mit 24:14-20Hakika kuna tumaini la baadaye kwa ajili yako,

nalo tarajio lako halitakatiliwa mbali.

1923:19 Kum 4:9; Mit 28:7Sikiliza, mwanangu na uwe na hekima,

weka moyo wako kwenye njia iliyo sawa.

2023:20 Hab 2:15; Rum 13:13; Isa 5:22Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo,

au wale walao nyama kwa pupa,

2123:21 Mit 21:17; 19:23; 19:15kwa maana walevi na walafi huwa maskini,

nako kusinzia huwavika matambara.

2223:22 Law 19:32; Efe 6:1-2Msikilize baba yako, aliyekuzaa,

wala usimdharau mama yako atakapokuwa mzee.

2323:23 Mit 4:7; 17:16; Mt 13:44Nunua kweli wala usiiuze,

pata hekima, adabu na ufahamu.

2423:24 Mit 23:15-16; 10:1; 15:20Baba wa mwenye haki ana furaha kubwa,

naye aliye na mwana mwenye hekima humfurahia.

2523:25 Mit 10:1Baba yako na mama yako na wafurahi,

mama aliyekuzaa na ashangilie!

2623:26 Mit 5:1-6; Za 18:21Mwanangu, nipe moyo wako,

macho yako na yafuate njia zangu,

2723:27 Mit 22:14kwa maana kahaba ni shimo refu

na mwanamke mpotovu ni kisima chembamba.

2823:28 Mit 7:11-12; Mhu 7:26Kama mnyangʼanyi, hungojea akivizia,

naye huzidisha wasio waaminifu miongoni mwa wanaume.

2923:29 1Fal 20:16; Mit 20:1; Isa 5:11; Nah 1:10; Mt 24:49, 50; Efe 5:18Ni nani mwenye ole?

Ni nani mwenye huzuni?

Ni nani mwenye ugomvi?

Ni nani mwenye malalamiko?

Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu?

Ni nani mwenye macho mekundu?

3023:30 Za 75:8; Efe 5:18; Mit 20:1; Efe 5:18; Za 75:8; Mit 9:2Ni hao wakaao sana kwenye mvinyo,

hao waendao kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa.

31Usiukodolee macho mvinyo wakati ukiwa mwekundu,

wakati unapometameta kwenye bilauri,

wakati ushukapo taratibu!

32Mwishowe huuma kama nyoka

na kutia sumu yake kama nyoka mwenye sumu.

33Macho yako yataona mambo mageni

na moyo wako kuwazia mambo yaliyopotoka.

34Utakuwa kama alalaye katikati ya bahari,

alalaye juu ya kamba ya merikebu.

3523:35 Mit 27:22; Yer 5:3; Kum 29:19; Isa 56:12; 2Pet 2:22Utasema, “Wamenipiga lakini sikuumia!

Wamenichapa, lakini sisikii!

Nitaamka lini

ili nikanywe tena?”

Korean Living Bible

잠언 23:1-35

1네가 관리와 함께 식사하게 될 때 네 앞에 앉은 자가 누구인지 주시하라.

2아무리 입맛이 당겨도 절제하여라.

3그가 베푼 것이 진수 성찬이라도 탐하지 말아라. 그것은 너를 속이는 미끼가 될 수도 있다.

4부자가 되려고 너무 애쓰지 말고 자제하는 지혜를 가져라.

5재물은 사라지는 법, 독수리처럼 날개가 돋쳐 날아가 버릴 것이다.

623:6 또는 ‘악한 눈이 있는 자의’인색한 사람의 음식을 얻어먹지 말며 그가 베푼 것이 진수 성찬이라도 탐하지 말아라.

7그는 언제나 비용부터 먼저 생각하는 자이다. 그가 말로는 너에게 와서 먹으라고 하지만 실제로 그의 마음은 그렇지 않다.

8너는 조금 먹은 것도 토하게 될 것이며 너의 고맙다는 찬사도 헛된 데로 돌아갈 것이다.

9미련한 자에게 말하지 말아라. 그는 너의 지혜로운 말을 업신여길 것이다.

10옛 경계석을 옮기지 말며 고아들의 밭을 침범하지 말아라.

11그들의 구원자가 되시는 여호와는 강하시니 그가 너를 대적하여 그들의 억울함을 풀어 주실 것이다.

12가르침에 유의하며 지식의 말씀에 귀를 기울여라.

13자식을 훈계하는 데 주저하지 말아라. 채찍으로 때려도 죽지 않는다.

14오히려 그를 채찍으로 벌하면 그의 영혼을 23:14 또는 ‘음부에서’죽음에서 구하게 된다.

15내 아들아, 네가 지혜로우면 내 마음이 기쁠 것이며

16네가 옳은 말을 하면 내가 정말 즐거워할 것이다.

17너는 죄인을 부러워하지 말고 두려운 마음으로 여호와를 섬기는 일에 항상 열심을 다하여라.

18분명히 너에게 밝은 미래가 있을 것이며 너의 희망이 끊어지지 않을 것이다.

19내 아들아, 너는 듣고 지혜를 얻어 네 마음을 바른 길로 인도하여라.

20술을 많이 마시는 자와 고기를 탐하는 자를 사귀지 말아라.

21술주정꾼과 대식가는 가난하게 되고 잠자기를 좋아하면 누더기를 걸치게 된다.

22너를 낳아 준 아버지에게 순종하고 늙은 너의 어머니를 업신여기지 말아라.

23진리를 사서 팔지 말아라. 지혜와 훈계와 총명도 마찬가지이다.

24의로운 자식을 둔 부모는 크게 즐거울 것이며 지혜로운 자식을 둔 부모도 즐거울 것이다.

25그러므로 너의 부모를 기쁘게 하고 즐겁게 하여라.

26내 아들아, 네 마음을 나에게 주고 내 길을 지켜 보아라.

27창녀는 깊은 구렁이며 음란한 여자는 좁은 함정이다.

28이런 여자들은 강도처럼 숨어 기다리다가 많은 남자들을 성실치 못한 사람으로 만들어 버린다.

29화를 입는 사람이 누구이며 슬픔을 당하는 사람이 누구인가? 다투는 자가 누구이며 불평하는 자가 누구인가? 이유 없이 상처를 입는 사람이 누구이며 눈이 충혈된 사람이 누구인가?

30바로 이들은 술집에 틀어박혀서 계속 술타령만 하는 자들이다.

31포도주가 아무리 붉고 잔에서 번쩍이며 잘 넘어갈 것처럼 보여도 너는 그것을 쳐다보지 말아라.

32결국 그 술이 뱀같이 너를 물 것이며 독사처럼 너를 쏠 것이다.

33네 눈에는 이상한 것이 보이고 정신이 혼미하여 괴상한 소리를 지껄일 것이니

34너는 돛단배에 몸을 싣고 바다 한가운데서 이리저리 밀려다니는 사람 같을 것이다.

35그리고 너는 “나를 때려도 아프지 않고 나를 쳐도 감각이 없다. 내가 깨면 다시 술을 찾겠다” 하고 말할 것이다.