Mithali 22 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 22:1-29

122:1 Mhu 7:1Heri kuchagua jina jema kuliko utajiri mwingi,

kuheshimiwa ni bora kuliko fedha au dhahabu.

222:2 Ay 31:15; Mt 5:45; Za 49:1-2Tajiri na maskini wanafanana kwa hili:

Bwana ni Muumba wao wote.

322:3 Mit 14:16; 27:12; Isa 26:20Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha,

bali mjinga huendelea mbele kama kipofu nayo ikamtesa.

422:4 Mit 15:33; 10:27; Dan 4:36Unyenyekevu na kumcha Bwana

huleta utajiri, heshima na uzima.

522:5 Mit 15:19; 1Yn 5:18Katika mapito ya waovu kuna miiba na mitego,

bali yeye ailindaye nafsi yake hukaa mbali nayo.

622:6 Efe 6:4Mfundishe mtoto njia impasayo kuiendea,

naye hataiacha hata akiwa mzee.

722:7 Yak 2:6Matajiri huwatawala maskini

naye akopaye ni mtumwa wa akopeshaye.

822:8 Hos 10:13; 8:7; Kut 1:20; Gal 6:7-8; Za 125:3Yeye aupandaye uovu huvuna taabu,

nayo fimbo ya ghadhabu yake itaangamizwa.

922:9 Kum 14:29; 2Kor 9:6; Mit 11:25; 28:27Mtu mkarimu yeye mwenyewe atabarikiwa

kwa kuwa hushiriki chakula chake na maskini.

1022:10 Mit 26:20; Mwa 21:9, 10; Za 101:5Mfukuze mwenye dhihaka,

na mvutano utatoweka;

ugomvi na matukano vitakoma.

1122:11 Mit 16:13; Mt 5:8Yeye apendaye moyo safi na yeye ambaye maneno yake ni ya neema,

mfalme atakuwa rafiki yake.

12Macho ya Bwana hulinda maarifa,

bali huyapinga maneno ya asiye mwaminifu.

1322:13 Mit 26:13Mvivu husema, “Yuko simba nje!”

au, “Nitauawa katika mitaa!”

1422:14 Mit 6:12; Mhu 7:26Kinywa cha mwanamke kahaba ni shimo refu;

yeye aliye chini ya ghadhabu ya Bwana

atatumbukia ndani yake.

1522:15 Mit 13:24; 20:30Upumbavu umefungwa ndani ya moyo wa mtoto,

bali fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali naye.

1622:16 Ay 20:19-23; Amo 2:6-8; Isa 3:14-15; Yak 2:13Yeye amwoneaye maskini ili kujiongezea mali,

naye ampaye tajiri zawadi, wote huwa maskini.

Misemo Ya Wenye Hekima

1722:17 Mit 1:8; 1:6; 30:1; 31:1; 2:2Tega sikio na usikie misemo ya wenye hekima,

elekeza moyo wako kwenye yale nifundishayo,

18kwa maana inapendeza unapoyahifadhi moyoni mwako

na kuwa nayo yote tayari midomoni mwako.

19Ili tumaini lako liwe katika Bwana,

hata wewe, ninakufundisha leo.

2022:20 Mit 8:6Je, sijakuandikia misemo thelathini,

misemo ya mashauri na maarifa,

2122:21 1Pet 3:15; Mhu 12:10kukufundisha maneno ya kweli na ya kuaminika,

ili uweze kutoa majibu sahihi

kwake yeye aliyekutuma?

2222:22 Law 25:17; Zek 7:10; Kut 23:6; Mal 3:5Usiwadhulumu maskini kwa sababu ni maskini,

wala kumdhulumu mhitaji mahakamani,

2322:23 Ay 29:16; Za 12:5; 1Sam 25:39kwa sababu Bwana atalichukua shauri lao

naye atawateka wao waliowateka.

24Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira ya haraka,

usishirikiane na yule aliye mwepesi kukasirika,

2522:25 1Kor 15:33la sivyo utajifunza njia zake

na kujiingiza mwenyewe kwenye mtego.

2622:26 Kum 19:14; Mit 23:10Usiwe mwenye kupana mikono katika rehani,

au kuweka dhamana kwa ajili ya madeni.

2722:27 Mit 11:15; 17:18Kama ukikosa njia ya kulipa,

kitanda chako

kitachukuliwa ukiwa umekilalia.

2822:28 Kum 19:14Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani

lililowekwa na baba zako.

2922:29 1Fal 11:28; Mwa 41:46; Mhu 9:10Je, unamwona mtu stadi katika kazi yake?

Atahudumu mbele ya wafalme;

hatahudumu mbele ya watu duni.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

箴言 22:1-29

1美名胜过巨富,

恩宠比金银宝贵。

2富人和穷人相同:

都由耶和华所造。

3明哲人遇祸躲避,

愚昧人前往受害。

4心存谦卑、敬畏耶和华,

必得财富、尊荣和生命。

5奸徒之道有荆棘和陷阱,

想保全生命的必须远避。

6教导孩童走正路,

他到老也不偏离。

7富人管辖穷人,

欠债的是债主的仆人。

8播种不义的必收灾祸,

他的恶势力终必瓦解。

9慷慨的人必蒙福,

因他给穷人食物。

10赶走嘲讽者,纷争平息,

争吵和羞辱也会消除。

11喜爱清心、口吐恩言的人,

必与君王为友。

12耶和华的眼目护卫真理,

祂必推翻奸徒的言论。

13懒惰人说:“外面有狮子,

我会丧命街头。”

14淫妇的口是深坑,

耶和华憎恶的人必陷进去。

15愚昧缠住孩童的心,

教棍能远远赶走它。

16靠压榨穷人敛财和送礼给富人的,

都必穷困潦倒。

智者之言

17你要侧耳听智者之言,

专心领受我的教诲,

18铭记在心、随时诵咏,

方为美事。

19今天我将这些指示你,

为要使你倚靠耶和华。

20关于谋略和知识,

我已写给你三十条,

21要使你认识真理,

能准确答复差你来的人。

22不可仗势剥削贫穷人,

法庭上不可欺凌弱者,

23因为耶和华必为他们申冤,

夺去掠夺他们之人的性命。

24不可结交脾气暴躁者,

不要跟易怒之人来往,

25免得你沾染他们的恶习,

不能自拔。

26不要为人击掌作保,

不要为欠债的抵押。

27如果你还不起,

连你的床也会被抬走。

28不可移动祖先定下的界石。

29你看那精明能干的人,

他必侍立在君王面前,

不会效力于泛泛之辈。