Mithali 21 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 21:1-31

121:1 Es 5:1; Yer 39:11-12Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana;

huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.

221:2 Mit 24:12; Lk 16:15; Yer 17:10; 1Sam 16:7Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake,

bali Bwana huupima moyo.

321:3 Hos 6:6; Mik 6:6-8Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika

zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.

421:4 Ay 41:34; Mit 6:17Macho ya kudharau na moyo wa kiburi,

ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!

521:5 Mit 10:4Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida,

kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.

621:6 Mit 10:2; 2Pet 2:3Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo

ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.

721:7 Mit 11:5Jeuri ya waovu itawaburuta mbali,

kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.

821:8 Mit 2:15Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu,

bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.

921:9 Mit 21:19; 19:13; 25:24Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba,

kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.

1021:10 Yak 4:5Mtu mwovu hutamani sana ubaya,

jirani yake hapati huruma kutoka kwake.

1121:11 Mit 19:25Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa,

mjinga hupata hekima;

wakati mtu mwenye hekima afundishwapo,

hupata maarifa.

1221:12 1Kor 10:10; Rum 2:8; Mit 14:11Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu,

naye atawaangamiza waovu.

1321:13 Ay 29:12; Zek 7:11; Mdo 7:57; Yak 2:13Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini,

yeye pia atalia, wala hatajibiwa.

1421:14 Mwa 32:20; Mit 18:16Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira

na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.

1521:15 Mit 21:9Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki,

bali kitisho kwa watenda mabaya.

1621:16 Za 49:14; Eze 18:24Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu,

hupumzika katika kundi la waliokufa.

1721:17 Mit 23:20-21, 29-35Mtu apendaye anasa atakuwa maskini,

yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.

1821:18 Isa 43:3-4; Mit 11:8Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki,

nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.

1921:19 Mit 21:9Ni afadhali kuishi jangwani

kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.

2021:20 Za 112:3; Mit 10:22; Mt 25:3Katika nyumba ya mwenye hekima

kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta,

lakini mtu mpumbavu

hutafuna vyote alivyo navyo.

2121:21 1Kor 15:58; Za 25:13; Mt 5:6Yeye afuatiaye haki na upendo

hupata uzima, mafanikio na heshima.

2221:22 Mit 8:14; Mhu 9:15-16Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu,

na kuangusha ngome wanazozitegemea.

2321:23 Za 34:13; Yak 3:2; Mit 12:13Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake

hujilinda na maafa.

2421:24 Yer 43:2Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake;

hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.

2521:25 Mit 13:4Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake,

kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.

2621:26 Law 25:35; Mt 5:42Mchana kutwa hutamani zaidi,

lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.

2721:27 1Fal 14:24; Amo 5:22; Mit 15:8Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo,

si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!

2821:28 Isa 29:21; Mit 19:5Shahidi wa uongo ataangamia,

bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.

2921:29 Mit 14:8Mtu mwovu ana uso wa ushupavu,

bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.

3021:30 Ay 12:13; Yer 9:23; 2Nya 13:12; Mdo 5:39Hakuna hekima, wala akili, wala mpango

unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.

3121:31 Isa 31:1; Za 3:8Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita,

bali ushindi huwa kwa Bwana.

King James Version

Proverbs 21:1-31

1The king’s heart is in the hand of the LORD, as the rivers of water: he turneth it whithersoever he will. 2Every way of a man is right in his own eyes: but the LORD pondereth the hearts. 3To do justice and judgment is more acceptable to the LORD than sacrifice. 4An high look, and a proud heart, and the plowing of the wicked, is sin.21.4 An…: Heb. Haughtiness of eyes21.4 the plowing: or, the light 5The thoughts of the diligent tend only to plenteousness; but of every one that is hasty only to want. 6The getting of treasures by a lying tongue is a vanity tossed to and fro of them that seek death. 7The robbery of the wicked shall destroy them; because they refuse to do judgment.21.7 destroy…: Heb. saw them, or, dwell with them 8The way of man is froward and strange: but as for the pure, his work is right. 9It is better to dwell in a corner of the housetop, than with a brawling woman in a wide house.21.9 a brawling…: Heb. a woman of contentions21.9 a wide…: Heb. an house of society 10The soul of the wicked desireth evil: his neighbour findeth no favour in his eyes.21.10 findeth…: Heb. is not favoured 11When the scorner is punished, the simple is made wise: and when the wise is instructed, he receiveth knowledge. 12The righteous man wisely considereth the house of the wicked: but God overthroweth the wicked for their wickedness. 13Whoso stoppeth his ears at the cry of the poor, he also shall cry himself, but shall not be heard. 14A gift in secret pacifieth anger: and a reward in the bosom strong wrath. 15It is joy to the just to do judgment: but destruction shall be to the workers of iniquity. 16The man that wandereth out of the way of understanding shall remain in the congregation of the dead. 17He that loveth pleasure shall be a poor man: he that loveth wine and oil shall not be rich.21.17 pleasure: or, sport 18The wicked shall be a ransom for the righteous, and the transgressor for the upright. 19It is better to dwell in the wilderness, than with a contentious and an angry woman.21.19 in…: Heb. in the land of the desert 20There is treasure to be desired and oil in the dwelling of the wise; but a foolish man spendeth it up. 21He that followeth after righteousness and mercy findeth life, righteousness, and honour. 22A wise man scaleth the city of the mighty, and casteth down the strength of the confidence thereof. 23Whoso keepeth his mouth and his tongue keepeth his soul from troubles. 24Proud and haughty scorner is his name, who dealeth in proud wrath.21.24 in proud…: Heb. in the wrath of pride

25The desire of the slothful killeth him; for his hands refuse to labour. 26He coveteth greedily all the day long: but the righteous giveth and spareth not. 27The sacrifice of the wicked is abomination: how much more, when he bringeth it with a wicked mind?21.27 with…: Heb. in wickedness? 28A false witness shall perish: but the man that heareth speaketh constantly.21.28 A…: Heb. A witness of lies 29A wicked man hardeneth his face: but as for the upright, he directeth his way.21.29 directeth: or, considereth

30There is no wisdom nor understanding nor counsel against the LORD. 31The horse is prepared against the day of battle: but safety is of the LORD.21.31 safety: or, victory