121:1 Es 5:1; Yer 39:11-12Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana;
huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
221:2 Mit 24:12; Lk 16:15; Yer 17:10; 1Sam 16:7Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake,
bali Bwana huupima moyo.
321:3 Hos 6:6; Mik 6:6-8Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika
zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
421:4 Ay 41:34; Mit 6:17Macho ya kudharau na moyo wa kiburi,
ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
521:5 Mit 10:4Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida,
kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
621:6 Mit 10:2; 2Pet 2:3Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo
ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
721:7 Mit 11:5Jeuri ya waovu itawaburuta mbali,
kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
821:8 Mit 2:15Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu,
bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
921:9 Mit 21:19; 19:13; 25:24Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba,
kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
1021:10 Yak 4:5Mtu mwovu hutamani sana ubaya,
jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
1121:11 Mit 19:25Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa,
mjinga hupata hekima;
wakati mtu mwenye hekima afundishwapo,
hupata maarifa.
1221:12 1Kor 10:10; Rum 2:8; Mit 14:11Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu,
naye atawaangamiza waovu.
1321:13 Ay 29:12; Zek 7:11; Mdo 7:57; Yak 2:13Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini,
yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
1421:14 Mwa 32:20; Mit 18:16Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira
na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
1521:15 Mit 21:9Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki,
bali kitisho kwa watenda mabaya.
1621:16 Za 49:14; Eze 18:24Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu,
hupumzika katika kundi la waliokufa.
1721:17 Mit 23:20-21, 29-35Mtu apendaye anasa atakuwa maskini,
yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
1821:18 Isa 43:3-4; Mit 11:8Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki,
nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
1921:19 Mit 21:9Ni afadhali kuishi jangwani
kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
2021:20 Za 112:3; Mit 10:22; Mt 25:3Katika nyumba ya mwenye hekima
kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta,
lakini mtu mpumbavu
hutafuna vyote alivyo navyo.
2121:21 1Kor 15:58; Za 25:13; Mt 5:6Yeye afuatiaye haki na upendo
hupata uzima, mafanikio na heshima.
2221:22 Mit 8:14; Mhu 9:15-16Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu,
na kuangusha ngome wanazozitegemea.
2321:23 Za 34:13; Yak 3:2; Mit 12:13Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake
hujilinda na maafa.
2421:24 Yer 43:2Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake;
hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
2521:25 Mit 13:4Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake,
kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
2621:26 Law 25:35; Mt 5:42Mchana kutwa hutamani zaidi,
lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
2721:27 1Fal 14:24; Amo 5:22; Mit 15:8Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo,
si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
2821:28 Isa 29:21; Mit 19:5Shahidi wa uongo ataangamia,
bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
2921:29 Mit 14:8Mtu mwovu ana uso wa ushupavu,
bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
3021:30 Ay 12:13; Yer 9:23; 2Nya 13:12; Mdo 5:39Hakuna hekima, wala akili, wala mpango
unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
3121:31 Isa 31:1; Za 3:8Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita,
bali ushindi huwa kwa Bwana.
1耶和華掌管君王的心,
易如支配壟溝的流水。
2人自以為行事正確,
但耶和華衡量人心。
3秉公行義比獻祭更蒙耶和華喜悅。
4高傲的眼,狂妄的心,惡人的燈,
都是罪惡。
5勤勞者的計劃必致富足,
行事急躁的人必致貧困。
6騙來的財如過眼雲霧,
使人掉進死亡的陷阱。
7惡人的暴力必毀滅自己,
因為他們行事不公不義。
8犯罪的人行徑扭曲,
純潔的人行為正直。
9寧願住在房頂的一角,
也不跟爭鬧之妻同屋。
10惡人貪戀邪惡,
對鄰舍殘忍無情。
11懲罰嘲諷者,愚人得智慧;
訓誡智者,他便長見識。
12公義的上帝鑒察惡人的家,
祂必使他們滅亡。
13掩耳不聽窮人呼求的,
他將來求救也無人管。
14暗中送的禮物能平息憤怒,
塞進懷裡的賄賂止息盛怒。
15正義得到伸張,
義人喜、惡人怕。
16人偏離明智之道,
終必與陰魂為伍。
17貪圖享受必窮困,
奢華宴樂難富足。
18惡人作義人的贖價,
奸徒替正直人受苦。
19寧願獨居曠野,
不跟吵鬧易怒的女子同住。
20智者家中積存寶物和油,
愚人將所有的揮霍一空。
21追求公義與慈愛的,
必尋得生命、公義和尊榮。
22智者攀上勇士的城池,
摧毀他們倚仗的堅壘。
23管住口舌,免遭禍患。
24嘲諷者狂妄自大,
行事驕橫無比。
25懶人的慾望害死自己,
因為他的手不肯做工。
26懶人整天貪得無厭,
義人施捨毫不吝嗇。
27惡人的祭物已經可憎,
何況他懷著惡意來獻!
28作偽證的終滅亡,
道實情的常發言。
29惡人虛張聲勢,
正直人謹慎行事。
30任何智慧、悟性和謀略,
都不能對抗耶和華。
31馬為爭戰之日預備,
勝敗由耶和華決定。