Mithali 21 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 21:1-31

121:1 Es 5:1; Yer 39:11-12Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana;

huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.

221:2 Mit 24:12; Lk 16:15; Yer 17:10; 1Sam 16:7Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake,

bali Bwana huupima moyo.

321:3 Hos 6:6; Mik 6:6-8Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika

zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.

421:4 Ay 41:34; Mit 6:17Macho ya kudharau na moyo wa kiburi,

ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!

521:5 Mit 10:4Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida,

kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.

621:6 Mit 10:2; 2Pet 2:3Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo

ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.

721:7 Mit 11:5Jeuri ya waovu itawaburuta mbali,

kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.

821:8 Mit 2:15Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu,

bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.

921:9 Mit 21:19; 19:13; 25:24Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba,

kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.

1021:10 Yak 4:5Mtu mwovu hutamani sana ubaya,

jirani yake hapati huruma kutoka kwake.

1121:11 Mit 19:25Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa,

mjinga hupata hekima;

wakati mtu mwenye hekima afundishwapo,

hupata maarifa.

1221:12 1Kor 10:10; Rum 2:8; Mit 14:11Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu,

naye atawaangamiza waovu.

1321:13 Ay 29:12; Zek 7:11; Mdo 7:57; Yak 2:13Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini,

yeye pia atalia, wala hatajibiwa.

1421:14 Mwa 32:20; Mit 18:16Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira

na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.

1521:15 Mit 21:9Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki,

bali kitisho kwa watenda mabaya.

1621:16 Za 49:14; Eze 18:24Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu,

hupumzika katika kundi la waliokufa.

1721:17 Mit 23:20-21, 29-35Mtu apendaye anasa atakuwa maskini,

yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.

1821:18 Isa 43:3-4; Mit 11:8Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki,

nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.

1921:19 Mit 21:9Ni afadhali kuishi jangwani

kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.

2021:20 Za 112:3; Mit 10:22; Mt 25:3Katika nyumba ya mwenye hekima

kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta,

lakini mtu mpumbavu

hutafuna vyote alivyo navyo.

2121:21 1Kor 15:58; Za 25:13; Mt 5:6Yeye afuatiaye haki na upendo

hupata uzima, mafanikio na heshima.

2221:22 Mit 8:14; Mhu 9:15-16Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu,

na kuangusha ngome wanazozitegemea.

2321:23 Za 34:13; Yak 3:2; Mit 12:13Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake

hujilinda na maafa.

2421:24 Yer 43:2Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake;

hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.

2521:25 Mit 13:4Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake,

kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.

2621:26 Law 25:35; Mt 5:42Mchana kutwa hutamani zaidi,

lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.

2721:27 1Fal 14:24; Amo 5:22; Mit 15:8Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo,

si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!

2821:28 Isa 29:21; Mit 19:5Shahidi wa uongo ataangamia,

bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.

2921:29 Mit 14:8Mtu mwovu ana uso wa ushupavu,

bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.

3021:30 Ay 12:13; Yer 9:23; 2Nya 13:12; Mdo 5:39Hakuna hekima, wala akili, wala mpango

unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.

3121:31 Isa 31:1; Za 3:8Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita,

bali ushindi huwa kwa Bwana.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

箴言 21:1-31

1耶和華掌管君王的心,

易如支配壟溝的流水。

2人自以為行事正確,

但耶和華衡量人心。

3秉公行義比獻祭更蒙耶和華喜悅。

4高傲的眼,狂妄的心,惡人的燈,

都是罪惡。

5勤勞者的計劃必致富足,

行事急躁的人必致貧困。

6騙來的財如過眼雲霧,

使人掉進死亡的陷阱。

7惡人的暴力必毀滅自己,

因為他們行事不公不義。

8犯罪的人行徑扭曲,

純潔的人行為正直。

9寧願住在房頂的一角,

也不跟爭鬧之妻同屋。

10惡人貪戀邪惡,

對鄰舍殘忍無情。

11懲罰嘲諷者,愚人得智慧;

訓誡智者,他便長見識。

12公義的上帝鑒察惡人的家,

祂必使他們滅亡。

13掩耳不聽窮人呼求的,

他將來求救也無人管。

14暗中送的禮物能平息憤怒,

塞進懷裡的賄賂止息盛怒。

15正義得到伸張,

義人喜、惡人怕。

16人偏離明智之道,

終必與陰魂為伍。

17貪圖享受必窮困,

奢華宴樂難富足。

18惡人作義人的贖價,

奸徒替正直人受苦。

19寧願獨居曠野,

不跟吵鬧易怒的女子同住。

20智者家中積存寶物和油,

愚人將所有的揮霍一空。

21追求公義與慈愛的,

必尋得生命、公義和尊榮。

22智者攀上勇士的城池,

摧毀他們倚仗的堅壘。

23管住口舌,免遭禍患。

24嘲諷者狂妄自大,

行事驕橫無比。

25懶人的慾望害死自己,

因為他的手不肯做工。

26懶人整天貪得無厭,

義人施捨毫不吝嗇。

27惡人的祭物已經可憎,

何況他懷著惡意來獻!

28作偽證的終滅亡,

道實情的常發言。

29惡人虛張聲勢,

正直人謹慎行事。

30任何智慧、悟性和謀略,

都不能對抗耶和華。

31馬為爭戰之日預備,

勝敗由耶和華決定。