Mithali 20 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 20:1-30

120:1 Law 10:9; Hab 2:5; 1Sam 25:36; 1Fal 20:16; Mit 31:4Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi;

yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.

220:2 Mit 8:36; 19:12; Es 7:7Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba;

yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.

320:3 Mwa 13:8; Mit 17:14Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi,

bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.

420:4 Mit 6:6; Mhu 10:18Mvivu halimi kwa majira;

kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama

lakini hapati chochote.

520:5 Za 18:16Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina,

lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.

620:6 Za 12:1; Mt 6:2; Mhu 7:28; Lk 18:8Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma,

bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?

720:7 Za 26:1; 37:25-26; 112:2Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama,

wamebarikiwa watoto wake baada yake.

820:8 1Fal 7:7; Mit 25:4-5Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu,

hupepeta ubaya wote kwa macho yake.

920:9 Mhu 7:20; 1Fal 8:46; 1Yn 1:8Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi;

mimi ni safi na sina dhambi?”

1020:10 Mit 20:23; 11:1Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti,

Bwana huchukia vyote viwili.

1120:11 Za 39:1; Mt 7:16Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake,

kama tabia yake ni safi na adili.

1220:12 Kut 4:11; Rum 11:26; Za 94:9Masikio yasikiayo na macho yaonayo,

Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.

1320:13 Mit 6:11; 19:15; Rum 12:11Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini,

uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.

14“Haifai, haifai!” asema mnunuzi,

kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.

1520:15 Ay 28:12, 16, 17, 18, 19Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi,

lakini midomo inenayo maarifa

ni kito cha thamani kilicho adimu.

1620:16 Kut 22:26; Mit 27:13Chukua vazi la yule awekaye dhamana

kwa ajili ya mgeni;

lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo

kwa ajili ya mwanamke mpotovu.

17Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu,

bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.

1820:18 Mit 11:14; 24:6Fanya mipango kwa kutafuta mashauri,

ukipigana vita, tafuta maelekezo.

1920:19 Mit 11:13Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika,

kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.

2020:20 Kut 21:17; Mit 30:11; Ay 18:5; Law 20:9Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake,

taa yake itazimwa katika giza nene.

2120:21 Mit 28:8; Hab 2:6Urithi upatikanao haraka mwanzoni,

hautabarikiwa mwishoni.

2220:22 Mit 24:29; Yer 42:11; Kum 32:35; Rum 12:17-19Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!”

Mngojee Bwana, naye atakuokoa.

2320:23 Kum 25:13Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu,

nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.

2420:24 Mit 19:21; Yer 10:23; Rum 8:26Hatua za mtu huongozwa na Bwana.

Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?

2520:25 Mhu 5:2-5; Yer 44:25Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka

na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.

2620:26 Mit 20:8Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu,

hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.

2720:27 Za 119:105; Mit 16:2Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu,

huchunguza utu wake wa ndani.

2820:28 Mit 29:14; Isa 16:5Upendo na uaminifu humweka mfalme salama,

kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.

2920:29 Mit 16:31Utukufu wa vijana ni nguvu zao,

mvi ni fahari ya uzee.

3020:30 Za 51:2; Mit 22:15Mapigo na majeraha huusafisha ubaya,

nayo michapo hutakasa utu wa ndani.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Proverbios 20:1-30

1El vino lleva a la insolencia,

y la bebida embriagante al escándalo;

¡nadie bajo sus efectos se comporta sabiamente!

2Rugido de león es la furia del rey;

quien provoca su enojo se juega la vida.

3Honroso es al hombre evitar la contienda,

pero no hay necio que no inicie un pleito.

4El perezoso no labra la tierra en otoño;

en tiempo de cosecha buscará y no hallará.

5Los pensamientos humanos son aguas profundas;

el que es inteligente los capta fácilmente.

6Son muchos los que proclaman su lealtad,

¿pero quién puede hallar a alguien digno de confianza?

7Justo es quien lleva una vida sin tacha;

¡dichosos los hijos que sigan su ejemplo!20:7 los hijos … su ejemplo. Lit. sus hijos después de él.

8Cuando el rey se sienta en el tribunal,

con su sola mirada barre toda maldad.

9¿Quién puede afirmar: «Tengo puro el corazón;

estoy limpio de pecado»?

10Pesas falsas y medidas engañosas:

¡vaya pareja que el Señor detesta!

11Por sus hechos el niño deja entrever

si su conducta será pura y recta.

12Los oídos para oír y los ojos para ver:

¡hermosa pareja que el Señor ha creado!

13No te des al sueño, o te quedarás pobre;

mantente despierto y tendrás pan de sobra.

14«¡No sirve, no sirve!», dice el comprador,

pero luego va y se jacta de su compra.

15Oro hay, y abundan las piedras preciosas,

pero aún más valiosos son los labios del saber.

16Toma la prenda del que salga fiador de un extraño;

retenla en garantía si la da en favor de desconocidos.

17Tal vez sea agradable ganarse el pan con engaños,

pero uno acaba con la boca llena de arena.

18Afirma tus planes con buenos consejos;

entabla el combate con buena estrategia.

19El chismoso traiciona la confianza;

no te juntes con la gente que habla de más.

20Al que maldiga a su padre y a su madre,

su lámpara se le apagará en la más densa oscuridad.

21La herencia de fácil comienzo

no tendrá un final feliz.

22Nunca digas: «¡Me vengaré de ese daño!»

Confía en el Señor, y él actuará por ti.

23El Señor aborrece las pesas falsas

y reprueba el uso de medidas engañosas.

24Los pasos del hombre los dirige el Señor.

¿Cómo puede el hombre entender su propio camino?

25Trampa es consagrar algo sin pensarlo

y más tarde reconsiderar lo prometido.

26El rey sabio avienta como trigo a los malvados,

y los desmenuza con rueda de molino.

27El espíritu humano es la lámpara del Señor,

pues escudriña lo más recóndito del ser.

28La misericordia y la verdad sostienen al rey;

su trono se afirma en la misericordia.

29La gloria de los jóvenes radica en su fuerza;

la honra de los ancianos, en sus canas.

30Los golpes y las heridas curan la maldad;

los azotes purgan lo más íntimo del ser.